SI KWELI Kuna nyoka anawika kama jogoo

SI KWELI Kuna nyoka anawika kama jogoo

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Zipo stori kongwe kuhusu nyoka aina ya koboko kuwa kuna muda anawika kama jogoo. Hii ni kweli?
1743487213146.png
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa tovuti ya Saint Loius Zoo wanamtaja nyoka aina ya Black Mamba kama nyoka wakubwa, wenye kasi, wakali na wenye sumu kali, hivyo kuwafanya kuwa miongoni mwa wanyama wanaokamata nafasi ya juu kwenye mlolongo wa chakula katika mazingira wanayoishi. Wanaweza kufikia urefu wa takriban futi 14 (mita 4.2) na wana uwezo wa kutambaa kwa kasi ya maili 12 kwa saa katika umbali mfupi. Pia, wana uwezo wa kung’ata mara kwa mara, jambo linalowaruhusu kuingiza kiasi kikubwa cha sumu wanaposhambulia.

Madai

Kumekuwapo na madai kuwa kuna baadhi ya nyoka wanawika kama jogoo. Na baadhi ya wadau wamebainisha kuwa nyoka wa aina hiyo wanajulikana kama Black Mamba.

Uhalisia wa madai hayo

JamiiCheck imefanya ufutailiaji wa madai hayo na kubaini kuwa madai ya nyoka kuwika kama kuku si ya kweli.

JamiiCheck imewasiliana na mtaalamu kutoka chuo cha ukufunzi Mkufunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Wanyamapori Mweka, Tito Lanoy ameeleza kuwa dhana hiyo haina uhalisia kwani kutokana na muundo wa ulimi wa nyoka kugawanyika mara mbili huku wakiwa na meno madogo mbelel hivyo si rahisi kwa wao kuwika kama kuku.

"Sio kweli kuhusu dhana hiyo, ulimi wa nyoka ni kama kamba iliyogawanyika mara mbili kwa mbele na meno yake yanakuwa yameshikana na nyama, hakuna namna nyoka anaweza kutengeneza sauti kama jogoo".

Aidha mtaalamu amebainisha kuna baadhi ya aina ya nyoka wanaweza kutengeneza baadhi ya sauti ikiwemo kupuliza, au kuvuta kuvuta hewa ndani

"Kuna baadhi ya nyoka wanaweza kutengeneza sauti kama tatu hivi, mfano aina ya Kifutu ndio anaweza kupuliza na anafanya hivyo kama kutoa tahadhari.

Pia kuna nyoka wanafanya sauti kama ya kuvuta ndani, hiyo inaweza kufanywa na jamii ya koboko.

Aina nyingine ni sauti kama ya kuvuta kwa ndani hivi, hiyo inaweza kufanywa na nyoka jamii ya koboko, kobra n.k"
Ni kweli hata sasa hivi nimetoka kumsikia na huwa wanawika tu kipindi cha Masika! Uliza watu wa Tabora au wanaoishi kwenye mapori ya Miyombo ambako Nyoka aina hiyo wanapatikana kwa wingi.
 
Ni kweli.
Koboko ndiye huwika kwa mlio unaofanana na wa jogoo ingawa mfumo wa sauti kati ya kuku na huyo nyoka ni tofauti.

Wenyeji wote wanaoishi vijijini hasa mikoa ya kanda ya kati pamoja na kanda ya magharibi hakuna asiyeujua muungurumo wa koboko.
Ndiyo yupo na niliwahi kukutana naye anakaa juu ya mti ni jamii tofauti hii ya nyoka wanapatikana mapori ya hifadhi karibu na mito ya Kitibitibi kijiji cha zeze wilaya kasulu mkoa wa Kigoma wana rangi ya kahawia na huwika mara nyingi wakiwa wanajibana katikati ya mti kuvua gamba lao
 
Wanadai koboko ndo huwika kama jogoo
Sasa hawa Jamii check wanachokanusha sikielewi!

Utafiti gani wa kidwanzi namna hii walifanya kukanusha ukweli!

Mi nimeishi maporini huko, habari ya koboko kuwika siyo ya kusimuliwa, nimeshuhudia.

Tena ni mida ya alfajiri na jioni.

Maelezo ya mtoa mada sijui sauti ya kuvuta kwa ndani hayana ukweli wowote.

Koboko akianza kuunguruma ni anaunguruma kweli na sauti habanii wala kuivuta kwa ndani kama kupiga mluzi, hapana yeye anasanuka hasa akianza kuwika.
 
Sasa hawa Jamii check wanachokanusha sikielewi!

Utafiti gani wa kidwanzi namna hii walifanya kukanusha ukweli!

Mi nimeishi maporini huko, habari ya koboko kuwika siyo ya kusimuliwa, nimeshuhudia.

Tena ni mida ya alfajiri na jioni.

Maelezo ya mtoa mada sijui sauti ya kuvuta kwa ndani hayana ukweli wowote.

Koboko akianza kuunguruma ni anaunguruma kweli na sauti habanii wala kuivuta kwa ndani kama kupiga mluzi, hapana yeye anasanuka hasa akianza kuwika.
Ngoja jamii check waje
 
Wataalam wazidi kufanya tafiti ili tuwe na majibu ya pamoja.
 
Back
Top Bottom