Jana wanadiplomasia 4 wa Iran, kufika tu Lebanon, wote wakauawa! Unafikiri hicho ni kitu rahisi? Walijuaje kuwa wanadiplomasia wa Iran wanaenda Lebanon? Walijuaje watakuwa wapi muda huo? Kumfuatilia kiongozi hadi kumwua tena wakati na yeye anachukua tahadhari za kiusalama, siyo jambo rahisi. Lazima tukubali kuwa intelijensia ya Israel ipo mbali sana ukilinganisha na ile ya Iran.
Na kama Israel ingeamua kupiga ovyo kama inavyofanya Iran, sahizi ingekuwa ni maelfu ya Wairan wamekufa..
Israel na Marekani wanajifahidi sana kuepuka mauaji ya raia ili wawananchi wa Iran wawaunge mkono katika kuuondoa utawala dhalimu na katili wa Ayafollah. Hata hivyo, kama waswahili wasemavyo, vita haina macho, bado kuna raia wa Iran wameuawa.