Kuna mnyama anaitwa Jeep Cherokee Trackhawk

Kama ilivyo kwa kila wapenzi wa magari huwa na ndoto ya kumiliki gari ya ndoto yake, kwa kweli kuna mnyama anaitwa Jeep Trackhawk, huyu mnyama ni SUV lakini usilinganishe na upuuzi kama Landcruiser V8 ndio ni upuuzi tu, nafahamu Landcruiser ni gari ya heshima na ya maana lakini ni upuuzi mbele ya huyu mnyama, sitengui kauli.

Ukiniwekea hapo Audi R8 na Trackhawk nachukua Trackhawk, mnyama anakuja na 6.2-liter supercharged V8 engine(RIP mnaosema gari ya 2500cc ni jini). Ukimiliki huyu mnyama inapaswa uishi karibu na sheli, hii gari ina kiu muda wote.

Ukimiliki hii gari ujue una supercar na pia hapo hapo una family car.


Huyu mnyama ana launch control, ni kubofya tu unataka uanze na rpm ngapi, top speed ni 470km/h, gari inatembea vibaya mno.
Mnyama ana mziki wa maana, siti zipo 5, lakini unaweza seti wakati inapiga mziki sauti uongeze kwenye siti ipi na wapi upunguze, mfano siti 3 za nyuma unaweza ukampunguzia sauti mtu wa kushoto apokee simu then ukaongeza sauti kwa mtu wa kulia aendelee kula dundo.

Gari yenye 707 hp haiwezi kuwa na brake za kizembe ina high perfomance brembo brakes, hawa brembo ni noma kwenye disc brake technology, trackhawk almost zote utakuta zina yellow calliper na zina calliper kubwa.

Mnyama ana tembea 0-60 within 3.5 sec, sio mchezo hio ni SUV lakini amini usiamini inazichomoa supercar nyingi tu road, kuna moja niliona Lamborghini anasomeshwa plate number na huyu mnyama.

Trackhawk ni extraordinary SUV.



Huyu ni kaka yake na jeep SRT, ni ngumu kuelezea uwezo wa hii mashine, features zilizopo ukielezea naweza andika mpaka kesho, gari kama hili kuzungumzia comfortability ni kama kuuliza Samsung galaxy S20 ina bluetooth.

MY21-Grand-Cherokee-Interior-Overland-Desktop.jpg.image.1440.jpg

Katika vyote ambavyo vinanimaliza kabisa ni exhaust sound ya huyu mnyama, mnyama anatisha kwenye kila sector, sio speed, luxury, exhaust sound, nguvu n.k.

Kinachonishangaza ni kwamba hii mashine kimuonekano inafanana sana na hizi Jeep Cherokee za kawaida, sasa omba ligi na kisubaru chako cha turbo ndio utajua hii ni SUV au Supercar.

Wadau mnaomfahamu huyu mnyama nasema uwongo ndugu zangu?

Nimeipenda kwa kweli...
 
Kwa mtu aliyewahi kuendesha hata Jeep Grand Cherokee ile ya 5.7L Hemi au Cherokee yeyote ya petrol atakuwa anaelewa how hizi gari zina nguvu na huwa zinatembea kama zinataka kupaa.

Pia ni gari ngumu sana.

Nipo Zanzibar kuna mzungu namrekebishia Range Rover yake. Ila ana Jeep Grand Cherokee limited pia na anaikubali balaa.
Ila zanzibar kuwa gari kama hizo ni sawa na kuwa na shamba la robo ekar na tractor massey ferguson.
 
Ila zanzibar kuwa gari kama hizo ni sawa na kuwa na shamba la robo ekar na tractor massey ferguson.

Huyo mzungu wa Zanzibar hayoko mjini. Yupo nje sana ya mji. Karibu saa zima.

Hiyo 5.7L Hemi ndio ilikuwa bara ila ni mkoani. Gari ilikuwa inaondoka acha kabisa. Ukijisahau utajikuta mtaroni.

Ye mwenyewe mwenye gari alikuwa anasema akiwa anakuja dar hakuna gari inampita.
 
Trackhawk ukiwa ndani ya huo mnyama unajiona kabisa wewe ndo mkuu wa mashetani kwa mlio tu wa hilo ndinga inatosha kutemesha kila kitu. Wakuu nimefurahi sana kuona mnaliongelea huku
View attachment 1819509View attachment 1819511View attachment 1819513
Hilo ndinga unatoka mkoani au unaingia mikoani, hakuna takataka yeyote itanusa hapo, usipokuwa makini unaachia barabara, Lamborghini gallardo haifuatii hapo, ninapoipendea ni SUV halafu ni very powerful kingine ni muonekano wake wa kawaida, halafu mlio wake unanimaliza kabisa.
Toyota supra ambayo ni fastest kwa toyota bado inasubiri kwa hili SUV.
 
Hilo ndinga unatoka mkoani au unaingia mikoani, hakuna takataka yeyote itanusa hapo, usipokuwa makini unaachia barabara, Lamborghini gallardo haifuatii hapo, ninapoipendea ni SUV halafu ni very powerful kingine ni muonekano wake wa kawaida, halafu mlio wake unanimaliza kabisa.
Toyota supra ambayo ni fastest kwa toyota bado inasubiri kwa hili SUV.
mkuu uko sahihi supra nayo siyo mchezo ila me naikubali old model
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom