Kuna Mke na kuna Mwanamke

Kuna Mke na kuna Mwanamke

Kisai

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2018
Posts
29,126
Reaction score
29,333
Habari za usiku huu watoto, vijana na wavyele pia.

Sitaki kuelezea hadhi na jinsia ya Mwanamke, bali natafuta ithibati na uhakika wa kauli hii: "Kila Mke ni Mwanamke lakini si kila Mwanamke ni Mke"

Wanandoa wote karibuni sana, bila shaka kauli hii mnaweza kuipa haki yake katika maana sahihi. Kwa kunionyesha je ina ukweli ndani yake au ni kinyume chake?
 
Naombeni nilale na mke wangu kwanza alafu kesho asubuhi nikikutana na wanawake mtaani nitawajibu
 
Mke;
Ni mwanamke mwenye sifa za kike na matendo ya kike.
Mwanamke:
Ni mwenye jinsia ya kike.
Si kila mwanamke ni mke
Unajua unachoongelea? Kwa hiyo mke ana jinsia gani?
 
Unajua unachoongelea? Kwa hiyo mke ana jinsia gani?
Kama umelelewa na kupewa elimu na ccm huwezi kuelewa, tulia hadi tar 29 oktoba angalau akili itakukaa
 
Watu wengi wameoa lakini hawana wake bali wana wanawake.

Kuwa na mke ni kitu kingine acheni kabisa.

Narudi.....
 
Nikirudi narudi na busara za Wazee wetu na ukweli mchungu juu yetu.
 
Mke;
Ni mwanamke mwenye sifa za kike na matendo ya kike.
Mwanamke:
Ni mwenye jinsia ya kike.
Si kila mwanamke ni mke
Shukrani kwa maelezo mazuri.

Sasa hawa wanawake wanao fanya kazi zenye haiba ya kiume hawana sifa za kuwa mke bila shaka, kwa kuzingatia maelezo yako. Hili tunakubaliana sote au una kipingamizi katika hili ?
 
....mke ni cheo chenye hadhi yake maalumu,Ila sio kila mwanamke anafit Kwenye hcho cheo japo kila mwanamke anatamani apate hcho cheo...tatizo vigezo na masharti.
Swadaktaa. Sasa utamjuaje yupi anafaa kuwa mke na yupi ni kinyume chake ?
 
Habari za usiku huu watoto, vijana na wavyele pia.

Sitaki kuelezea hadhi na jinsia ya Mwanamke, bali natafuta ithibati na uhakika wa kauli hii: "Kila Mke ni Mwanamke lakini si kila Mwanamke ni Mke"

Wanandoa wote karibuni sana, bila shaka kauli hii mnaweza kuipa haki yake katika maana sahihi. Kwa kunionyesha je ina ukweli ndani yake au ni kinyume chake?
Ni sahihi.
Mfano usiku nimelala na mwanamke, lakini huwezi amini sijapata mke!
 
Shukrani kwa maelezo mazuri.

Sasa hawa wanawake wanao fanya kazi zenye haiba ya kiume hawana sifa za kuwa mke bila shaka, kwa kuzingatia maelezo yako. Hili tunakubaliana sote au una kipingamizi katika hili ?
Kuwa na sifa haitegemei kazi anayofanya bali sifa yake.
Mke ni mwanamke mwenye matendo yanayohitajika kwa jinsia ya kike.
Mfano ana tabia ya ulezi/mlezi, umama nk.
Kuna wenye jinsia ya kike lakini hawana sifa za kike.
 
Wazee wetu wanatuambia hivi, vijana wa siku hizi mmekosa vitu viwili toka kwa wanawake tulio waoa.

1. Vijana mmekosa mapenzi
2. Vijana mmekosa vyakula (Yaani Wanawake wa siku hizi hawajui kupika na mfano wa hayo)

Hapa wanamaanisha wao ndiyo walikuwa na wale ila siai tunaishi na wanawake.

Nimenukuu.

"Tumi hauwawi"
 
Back
Top Bottom