Kuna kiongozi duniani amewahi kukataa kutandikiwa zulia jekundu?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,028
144,382
Tumewahi kusikia viongozi mbalimbali duniani wakikataa kufanyiwa mambo ya kutukuzwa na wengine hata kukataa kulipwa mishahara mikubwa ya anasa ili tu wajaribu kuishi kama raia wengine wa kawaida.

Lakini kuna hili la viongozi kutandikiwa zulia jekendu(red carpet) kuanzia kwenye ngazi za ndege,wakati wa kula kiapo,kuapisha,wanapopanda majukwaani,n.k.

Tunatetea na kunasema hili ni jambo la kawaida na lililozoeleka na ni heshima pia kwa viongozi kwahiyo ni sahihi tu ingawa mimi binafsi huwa naona ni moja ya mambo yanayowafanya baadhi ya watawala kujiona wao ni kama miungu watu au wao ni very special(kulewa madaraka).

Binafsi ningekuwa kiongozi ningekataa kabisa huu utamadani ndani ya nchi yangu labda tu pale napopokea wageni wa kimataifa au kutoka nje ya nchi ambako inaweza kuwa vigumu kukwepa jambo hili.

Swali langu ni je,katika viongozi ambao wameshawi kuonyesha "humility" hapa duniani kwa kauli na matendo yao,kuna kiongozi hata mmoja aliewahi kukataa kutandikiwa zulia hili?

Kwa mfano,unakataa kuitwa mtukufu /kutukuzwa alafu wakati huo huo unakubali kutembea kwenye zulia jekendu la gharama kubwa tu sasa hapo sijui unakataa nini na unafanya nini!
 
kuna rais 1 wanchi za ughaibuni huyu bwana amekataa katu katu kulindwa. Vingora, na Kuishi Ikulu.

yeye anatumia Bito yake ile ya kizamani kabisa na anaishi yeye na familia yake kwenye nyumba ya kawaida kwenye moja wapo ya shamba lake.

Mgoogle Utamjua huyu Utaratibu wa kitukufu na kutukuzwa alipiga marufuku na Anapendwa sana na wananchi wake.
 
Tumewahi kusikia viongozi mbalimbali duniani wakikataa kufanyiwa mambo ya kutukuzwa na wengine hata kukataa kulipwa mishahara mikubwa ya anasa ili tu wajaribu kuishi kama raia wengine wa kawaida.

Lakini kuna hili la viongozi kutandikiwa zulia jekendu(red carpet) kuanzia kwenye ngazi za ndege,wakati wa kula kiapo,kuapisha,wanapopanda majukwaani, n.k.

Tunatetea na kunasema hili ni jambo la kawaida na lililozoeleka na ni heshima pia kwa viongozi kwahiyo ni sahihi tu ingawa mimo binafsi huwa naona ni moja ya mambo yanayowafanya baadhi ya watawala kujiona wao ni kama miungu watu au wao ni very special(kulewa madaraka).

Binafsi ningekuwa kiongozi ningekataa kabisa huu utamadani ndani ya nchi yangu labda tu pale napopokea wageni wa kimataifa au kutoka nje ya nchi ambako inaweza kuwa vigumu kukwepa jambo hili.

Swali langu ni je,katika viongozi ambao wameshawi kuonyesha "humility" hapa duniani kwa kauli na matendo yao,kuna kiongozi hata mmoja aliewahi kukataa kutandikiwa zulia hili?
waulize chadema kwanza kuwa kuna mbunge yeyote aliyewahi kataa asiitwe mheshimiwa ili asionekane kama mungu mtu. Today You are too low mleta mada
 
waulize chadema kwanza kuwa kuna mbunge yeyote aliyewahi kataa asiitwe mheshimiwa ili asionekane kama mungu mtu. Today You are too low mleta mada
Hata hiyo ya kuitwa sijui muheshimiwa nako ni yale yale tu.Hawa wanatakiwa waitwe ndugu tu inatosha.

Usisahau ni Naibu Spika ndie alielilia kutaka kuitwa muheshimiwa.

Unatembe kwenye red carpet wakati wajawazito wanalala chini!!
 
Hata hiyo ya kuitwa sijui muheshimiwa nako ni yale yale tu.Hawa wanatakiwa waitwe ndugu tu inatosha.

Usisahau ni Naibu Spika ndie alielilia kutaka kuitwa muheshimiwa.

Unatembe kwenye red carpet wakati wajawazito wanalala chini!!
Ni mtu mwenye akili tu ndiyo anaweza kukuelewa lakini siyo team Lumumba wafia chama.
 
kuna rais 1 wanchi za ughaibuni huyu bwana amekataa katu katu kulindwa. Vingora, na Kuishi Ikulu.

yeye anatumia Bito yake ile ya kizamani kabisa na anaishi yeye na familia yake kwenye nyumba ya kawaida kwenye moja wapo ya shamba lake.

Mgoogle Utamjua huyu Utaratibu wa kitukufu na kutukuzwa alipiga marufuku na Anapendwa sana na wananchi wake.
Hawa ndio viongozi wanaoonyesha humbleness na ni vigumu sana kwa kiongozi wa aina hii kulewa madaraka/kuota mapembe.
 
Ni mtu mwenye akili tu ndiyo anaweza kukuelewa lakini siyo team Lumumba wafia chama.
Siku Magu akisema sitakiwa kutandikiwa red carpet ndio itaaonekana hoja na hawa hawa vijana wa Lumumba ndio watakuwa wa kwanza kumsifia.

Unaweza kuta gharama ya carpet kama hilo ni sawa ni vitanda kadhaa vya wagonjwa na yanabadilishwa kila wakati.
 
Kwa hiyo kwa akili yako red carpet ni kwa ajili ya wageni wa kimataifa?

Usipowawekea hilo zulia wamesema hawaji nchini mwako?
 
kuna rais 1 wanchi za ughaibuni huyu bwana amekataa katu katu kulindwa. Vingora, na Kuishi Ikulu.

yeye anatumia Bito yake ile ya kizamani kabisa na anaishi yeye na familia yake kwenye nyumba ya kawaida kwenye moja wapo ya shamba lake.

Mgoogle Utamjua huyu Utaratibu wa kitukufu na kutukuzwa alipiga marufuku na Anapendwa sana na wananchi wake.
Huyo ni rais wa Uruguay lakini amestaafu Mzee wa watu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom