Chakaza
JF-Expert Member
- Mar 10, 2007
- 39,797
- 71,217
Musiba tena katumwa kutoa kiashiria what's coming next. Kitendo cha serikali kukamatiwa ndege yake kwa madeni ya mkulima iliyogoma kuyalipa na kumfukuza, kimeiaibisha serikali na kuiumiza sana pengine kuliko mambo mengi yaliyopata kutokea.
Na kama ilivyo kawaida Musiba, pamoja na malalamiko mengi ya kauli zake na matisho kutolewa ila imedhibitika pasipo shaka kuwa yeye in SAUTI KUU ya wasio onekana lakini wenye nguvu isiyo zuilika. Hivyo kila akisemacho yeye ni spika tuu na Redio iko mafichoni.
Ukisikiliza "tangazo" lake hapo juu ni kichinjio cha mwisho kwa LOWASSA na kummaliza ndani ya CCM alikorudi akidhani atatunzwa.
Kumtaja Karume na Nyalandu inafahamika "wanavyochukiwa" kwa sasa na wakubwa wa CCM ila inatafutwa strike back bado haijapatikana tuu.
Hofu yangu ni kwa kutajwa na kuhusishwa kwa mawakili wa Kitanzania na sakata hili. Jee wako salama au ndio wanatengenezewa zengwe kama la Tundu Lissu ili kupata uhalali wa "VITANI INAJULIKANA MSALITI ANAFANYWAJE?"
Watu tunachukulia kauli mbaya kama hizi kuwa ni kawaida na hii maana yake tunaona maisha ya watu haya fai kuchukuliwa tahadhari na kama Taifa tumepotea.
Oneni mtu kama mkuu wa mkoa Chalamila, ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama ngazi ya mkoa. Kada wa chama Tawala na mwakilishi wa taasisi ya Uraisi ndani ya mkoa anatangaza polisi na watu waue vibaka na kuwa yeye amewahi kuua MTU (maana hakukuwa na ushahidi ni kibaka) na akajipongeza kwa bia.
Au tumehalalisha kauli aliyoisema Zitto kuwa sasa hivi hii nchi yetu ni UNITED STATE OF GANGSTERS?
TLS msisubiri wanachama wenu kuwaokota kwenye viroba au wako hospitalini, kemeeni kauli hizi na ogomeni kumuwakilisha "msemaji" huyo kwenye kesi zake zote ili yatokee maajabu mtu binafsi kuwakilishwa na mawakili wa serikali.