DOKEZO Responded Kuna Kampuni inakamata magari kwa uonevu kwa kisingizio cha kuegesha vibaya Ubungo

DOKEZO Responded Kuna Kampuni inakamata magari kwa uonevu kwa kisingizio cha kuegesha vibaya Ubungo

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Kwa madereva kwani wamekuwa wakikamata kwa uonevu unakuta dereva kaegesha sehemu ambayo muhusika wa ku-scan anaku-scan ila wao wakipita wanakukamata wakati ushascaniwa. Na pia wanakuta dereva amepark gari kwa dharura kawasha double hazard bado wanakukamata.

Pia wakikukamata wakikupeleka ofisini kwao wanakupa form yenye maelezo ya kulipa faini isiyokuwa na control number ukiwaambia wakupe control number wanakuzungusha wakitaka ulipe pesa cash .

Na pia tunaomba Serikali iingilie kati kiwango cha faini wanayotoza kulingana na aina ya kosa lenyewe kwani faini inayosomeka kwenye form yao ni Tsh 80,000.
20250816_093232.png

Majibu ya Manispaa ya Ubungo haya hapa ~ Manispaa ya Ubungo: Faini ya wrong parking ni Tsh. 80,000, ukikutwa na kosa hautaruhusiwa kuondola hadi ulipe
 
Kwa madereva kwani wamekuwa wakikamata kwa uonevu unakuta dereva kaegesha sehemu ambayo muhusika wa ku-scan anaku-scan ila wao wakipita wanakukamata wakati ushascaniwa. Na pia wanakuta dereva amepark gari kwa dharura kawasha double hazard bado wanakukamata.

Pia wakikukamata wakikupeleka ofisini kwao wanakupa form yenye maelezo ya kulipa faini isiyokuwa na control number ukiwaambia wakupe control number wanakuzungusha wakitaka ulipe pesa cash .

Na pia tunaomba Serikali iingilie kati kiwango cha faini wanayotoza kulingana na aina ya kosa lenyewe kwani faini inayosomeka kwenye form yao ni Tsh 80,000.
Binafsi yalinikuta haya, wiki mbili nyuma. Nilikua nanunua maji dukani kugeuka washafunga gari kwa nyororo!

Ukifika kule ofisini kwao (Karibu na kituo cha polisi Mawasiliano) wanakuambia ukitaka kulipa kwa control number lazima uwe na nakala ya leseni na namba ya utambulisho wa mlipakodi (tin). Kampuni inayoendesha zoezi hili inaitwa 'Boss Kazi'

Zoezi hili limejaa uonevu mkubwa sana, ni uporaji kabisa.
 
Hizi kampuni ni jipu haswaa. Wanazunguka na Bajaj yao, kuwinda watu, kuna siku Nimesimama pia kituoni naongea na simu, mara hao wakanivamia Umefanya wrong parking.
Nikawauza maana ya wrong parking ni nini, na kama naongea na simu nilitakiwa nifanye nini?
Wakajibu ulitakiwa uwashe hazard, nikawauliza hazard kwa sababu gani na why hazard wakati sijamzuia yeyote kupita na nini kazi ya hivi vituo/Flash parking? Na kama mimi wa gari binafsi siruhusiwi kupak Mbona wakala wa barabara hajaniwekea kibao cha no parking?
Nikawauliza so nyie na bajaj yenu hapo mmefanya wrong parking sio Mbona mnanisemesha hapa mmesimamisha hapo Bajaj yenu na hamjawasha hazard?
Kiufupi niliwaka, wakawasha bajaj yao wakatimua kimya kimya!
Walowapa hii contract kwa kweli wajitafakari, wanakera sana na ni wapigaji mnoo
 
Huko Ubungo si tuliambiwa kuwa wamefunga kamera kwenye mataa na "wrong parking" sasa kampuni binafsi ya nini tena? Halafu wao si waandike faini mkosaji alipe kwa "control" namba pesa iingie serekalini kwa nini walazimishe "cash" kama sio ulaji wa watu binafsi?

Na si hivyo tu kuna kero nyingine kwenye lile soko pale Mbezi shule na soko la mahakama ya ndizi pale Mabibo ukipaki kufanya manunuzi lazima ulipe "cash". Ukiwaeleza kuwa nitalipa "online" pesa iingie serikalini hawataki. Sijui ni nani anafaidika na hii miradi. Na sijui nani alirudisha kulipa "cash" wakati awamu iliyopita hayo mambo yaliondolewa kila mahali.

Sasa upotevu huu wa pesa za serikali uanofanyika wazi wazi mchana kweupe ndio unafanya watu wathibitishe pasi na shaka maneno ya watu kama wakina Pole Pole kwamba kuna wahuni wamedukua mfumo. Nimuombe wakili msomi aachane na mambo madogo madogo ya kutumiana meseji na Pole Pole kubishana katiba ya chama hiyo akiachie chama chake kijibu au kupambana na waumini wa Gwajima hizo ni ishu ndogo sana na hazina faida za kiuchumi kwa taifa. Badala yake aende pale soko la Mbezi shule na mahakama ya ndizi mabibo akabadilishe mfumo wa kulipa "cash" watu walipe maegesho "online" ili serikali iongeze mapato yake na kupunguza uwezekano wa pesa ya serikali kupotea.

Na hata hao wanaojifanya sijui "wrong parking" wao waishie tu kuandika faini na kutoa "control" namba pesa iiipwe serikalini.

Ni mtizamo tu.
 
Hizi kampuni ni jipu haswaa. Wanazunguka na Bajaj yao, kuwinda watu, kuna siku Nimesimama pia kituoni naongea na simu, mara hao wakanivamia Umefanya wrong parking.
Nikawauza maana ya wrong parking ni nini, na kama naongea na simu nilitakiwa nifanye nini?
Wakajibu ulitakiwa uwashe hazard, nikawauliza hazard kwa sababu gani na why hazard wakati sijamzuia yeyote kupita na nini kazi ya hivi vituo/Flash parking? Na kama mimi wa gari binafsi siruhusiwi kupak Mbona wakala wa barabara hajaniwekea kibao cha no parking?
Nikawauliza so nyie na bajaj yenu hapo mmefanya wrong parking sio Mbona mnanisemesha hapa mmesimamisha hapo Bajaj yenu na hamjawasha hazard?
Kiufupi niliwaka, wakawasha bajaj yao wakatimua kimya kimya!
Walowapa hii contract kwa kweli wajitafakari, wanakera sana na ni wapigaji mnoo
Nilikutana na dereva wa pikipiki za gurudumu tatu 'bajaji', hawa wa mtandao, ameingia kituoni akawa anawasiliana na abiria, wakamkamata na kumtoza 80k!
Unawauliza kuna mtu anapaki na kuacha gari bila kufunga? Au dereva akiwa ndani ya gari?
Na hiyo kusema uwashe taa za tahadhari, huwa wanaweza kubadilisha tu, wakasema ungeweka na 'triangle'. Yaani wale watu ndo sheria! Wanatembea na maana ya parking mifukoni kwao.
Nafikiri pia kwenye kulipia kuna magumashi, kwani hawapendi ulipe kwa control number, bali fedha taslimu.
 
Back
Top Bottom