Kuna haja ya kumjulisha?

Kuna haja ya kumjulisha?

maimatha

Senior Member
Joined
Mar 2, 2013
Posts
129
Reaction score
162
Sina mawasiliano mazuri na my x na nibaada ya kuwa na ujauzito.

Hapo nyuma tulikua na mawasiliano mpaka ujauzito ulipofika miez 7 ndo akanitamkia hanipendi tena.. kisa nimemuuliza kwa nini anaficha simu yake na akiingia ndani anaizima au anaweka silent kifupi story ni ndefu.

Sasa basi tangu ujauzito unamiezi 7 hajawahi kunipigia simu wala message ya kuniuliza naendeleaje wala kujua afya yangu mpaka sasa miezi tisa nauliza wenzangu mungu akinisaidia nikajifungua salama kuna haja ya kumjulisha kama nimejifungua?
Nikae tu kimya maana niliondoka kwake nipo kwetu na nahudumiwa na wazazi wangu.
 
Ni maamuzi yako kumwambia kama umejifungua au la, ila kwa maoni yangu ukimwambia naye akiamua kutokujali na kutokuja kuwaona wewe na mtoto itakuumiza sana. Tafakari kwa kina maongezi yenu ya mwisho alipokuambia kwamba hakupendi ili kuamua kama umwambie au la, si vibaya pia kuomba mawazo ya wazazi wako. Kila la heri katika ujauzito wako.

 
Mmmmmmmh! Mwambie too! Kama makosa ni yake! Ubaya wa mtu mwingine usikufanye na wewe uwe mbaya! We mwambie tu, possibly hatojibu chochote!

I know you are mad, maybe boiling, i understand how you are feeling ( honestly i dont, i imagine the worst) lakini makosa ya baba usimlipishe mtoto! Mpe chansi mtoto ya kumjua baba yake. Wewe itakuumiza mnoo ila mtoto itamsaidia kujua maisha yalivo na jinsi wewe usivo na makosa! Anaweza kuwa mkubwa anajiaminisha baba yake mtu wa maana kumbe ni MTU MZIMA OVYO flani tu.

DONT LET THE WORLD TURN YOU TO SOMETHING YOU ARE NOT!
 
Ningekua mimi ndo wewe kwanza ningeshamwambia nimetoa mimba halafu baada ya hapo maisha yangu yanasonga mbele.
Mtu kama huyo atasubiri mwanao akishakuwa ataanza kujisifu"mie kidume bwana hili ni jembe langu"
 
Tatizo muomba ushaur hataki kueleza side A ilikuwaje hadi jamaa anaamua kufanya haya,maana inaonekana kuna jambo kubwa alilofanya huyu mwanamke ndo maana yametokea haya..na kwa uzoefu ni kuwa wanawake huwa ni watu wanaoanza kuumiza wanaume kwa kutokuwa waaminifu,mwanaume akifanya yake huwa mwanamke husika hupiga kelele sana kuwa anaonewa na hawako tayar kusema ukweli kwa walichofanya...nina amini hiyo mimba itakuwa ilishaleta mgogoro haswa wa jamaa kutokuwa na imani kuwa ni yake..
 
Sioni sababu ya kunyali mtu hapa km huwezi kumshauri,mnapenda kucomment tu hata akili inatema mapepe
 
Tatizo muomba ushaur hataki kueleza side A ilikuwaje hadi jamaa anaamua kufanya haya,maana inaonekana kuna jambo kubwa alilofanya huyu mwanamke ndo maana yametokea haya..na kwa uzoefu ni kuwa wanawake huwa ni watu wanaoanza kuumiza wanaume kwa kutokuwa waaminifu,mwanaume akifanya yake huwa mwanamke husika hupiga kelele sana kuwa anaonewa na hawako tayar kusema ukweli kwa walichofanya...nina amini hiyo mimba itakuwa ilishaleta mgogoro haswa wa jamaa kutokuwa na imani kuwa ni yake..

Don't complecate your self mkuu. Mdada ameuliza kwamba baada ya kujifungua, jekunahaja ya kumpa taarifa x wake?
 
we omba Mungu ujifungue vizuri ulee mtoto wako. Huyo hata ukimwambia sidhani kama atakuja kuhudumia mtoto. Yeye alikuacha na mimba kubwa so anajua una kiumbe chake akapiga kimya anaendelea na maisha yake. Zaa tu ulee mwanao akipenda atakutafuta
 
Stori kama hizi zinasikitisha sana..hivi siku hizi kuna watu bado wanakimbia watoto kweli ..?!
 
kukaa kmya hakusaidii sana kwani kuna siku atajua na mtoto akikua atahitaji tu kwenda kwa ndugu zake ...labda uamue kumuua mtoto nor kukaa kmya haisaidii,alafu kwani ukimwambia inakupunguzia nini wewe?acha visasi mwombe Mungu ndo anajua
 
Don't complecate your self mkuu. Mdada ameuliza kwamba baada ya kujifungua, jekunahaja ya kumpa taarifa x wake?

Haya mambo huwez kuamua kwa kuangalia tamati bila kuangalia chanzo...sasa unamuambia usimuambie umuambie halafu????
 
Nawe hukulazimishwa uandike chochote. Mtu anapokuja na post ya kuomba ushauri solazima umseme mbaya. Kwani angekua dada yako ungemtolea maneno yenye maumivu kiasihicho?

naww acha kujipaka mafuta ww vp?
Mpe ushaur ww sasa. Hvi wakat wanavuana vyupi walikuja kutuomba ushaur?
Acha kulealea watu bhana
 
pole bidada me naona haina haja ya kumficha/ kutompa taarifa ni vema umjulishe naimani atajirudi tu mwombe mungu plz tena plz ukijifungua mjulishe hapo roho ya ubinadam itamjia na mambo yataenda sawa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom