wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 24,688
- 26,796
Yaani unakuta mtalii tena mgeni yuko mbugani na mikamera yake alafu akikuta mnyama anaekula mnyama mwenzake kama fisi simba au chui anataka kula mnyama badala ya kumsaidia huyo mnyama anaeliwa asiliwe eti ndio kwanza anaseti kamera vizuri kushoti video mnyama anavyoliwa.
Kinachouma zaidi unakuta mnyama kama twiga au pundamilia na nyati ambae serikali ndio inawathamini zaidi ndio wanauwawa, badala ya kuzuia wanawaacha. Inauma sana/nimeumia sana, hawa watalii hata kama wanatuingizia hela nimewachukia sana.
Mbona kwao wanyama wao wanawapa nyama, tena mara nyingi naona ya ng'ombe hawaachi wakaua ovyo ovyo kama huku kwetu? Au wanafurahia wanyama wetu wanavyouliwa?
Kinachouma zaidi unakuta mnyama kama twiga au pundamilia na nyati ambae serikali ndio inawathamini zaidi ndio wanauwawa, badala ya kuzuia wanawaacha. Inauma sana/nimeumia sana, hawa watalii hata kama wanatuingizia hela nimewachukia sana.
Mbona kwao wanyama wao wanawapa nyama, tena mara nyingi naona ya ng'ombe hawaachi wakaua ovyo ovyo kama huku kwetu? Au wanafurahia wanyama wetu wanavyouliwa?