Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,082
Ni jambo la busara kujitunza wewe na mwanao. Kutunza mtoto wako linaweza kuwa jambo la kukufurahisha, lakini ni kazi ngumu. Utampatia mtoto chakula/utamlisha mtoto mara ngapi na baada ua wakati mgani? Wewe hufanya nini mwanao anapolia au anapougua? Unozuia maradhia aje?
Unaweza kuwa mwepesi kushtuka/utakuwa na wasiwasi au lakini utayagundua hayo haraka. Utashtuliwa na ambayo unajua tayari. Katika sehemu hii, utapata kujua unayofaa kufanya utakapomleta mwanao nyumbani
Kumpeleka mwanao nyumbani
Mtoto aliyezaliwa anajiratibisha na ulimwengu ulio tofauti na joto na usalama wa tumbo la mamake. Watoto hawa wanastahili kupendwa,kulishwa, kuwekwa safi na wakiwa na joto inayofaa. Kuna mambo mengi mapya wazazi wanapaswa kujua.
Afya ya mwanao
Unafaa kumwita/kumpigia daktari wako kama utaona uafuatayo kwa mwanao:
Kukosa kula/kukataa chakula
Kuwa na rangi isiyostahili
Nguvu kidogo
Joto la juu ya 380c chini ya kwapa
Ghasia/fujo zisio za kawaida
Kulala zaidi ya kawaida
Kutapika au kuhara
Shida za kupumua
Kumbadilisha nepi
Usimwache mwanao juu ya meza ya kumbadilishia nguo sababu anaweza kuanguka na kuumia. Weka kila kitu unachohitaji juu ya meza hii au karibu nawe. Wakati unasafiri, beba kila kitu kwa kifuko cha diaper.
Jinsi ya kumbadilisha napi
Mlaze mwanao mahali dhabiti na tambarare kama kwa meza kasha ufungue diaper iliyochafuliwa.
Inua miguu ya mwanao kwa kuishikia kwenye kufundo na utoe diaper hio.
Osha mwanao vizuri kwa kutumia katani na maji moto (kwa watoto wachanga sana).
Hakikisha umempamgusa mwanao mbile na nyuma ili kinyesi kisitapakae kea sehemu zingine za mwili.
Tumia uvumbi wa wanga wa nafaka (comstarch powder) au Fulters Earth na usiguze uso. Usitumie uvumbi huu kwa watoto wachanga mno.
Pitisha diaper chini ya mtoto. Vuta sehemu ia mbele kati ya miguu na ufunge.
Vipele visabishwao na napi
Mtoto hutumia diaper kama kumi kwa siku. Kama hutomgeuzia mtoto wako diaper atapata vipele. Hili hutokea kama mwanao atakuwa na maji maji (ulowevu) akiwa amevishwa diaper. Huu upele hukaa mwekundu na hukaa kwa siku chache. Diaper rash inaweza sababishwa pia na sabuni ya vumbi ya kuosha ilizo na nguvu sana au vitu vya kufanya ngozi iwe nyororo, kwa hivyo kama kumweka mwanao safi na mkavu hakusaidii geuza bidhaa unazo muosha nazo.
Jinsi ya kushughulikia vipele vya napi
Unapongeuzia mwanao diaper mwache kwa dakika 10 ili apunge hewa
Lowesha nyuma ya mwanao kwa maji moto kisha ipanguze kwa tahadhari
Geuzia mwanao Diaper ma utumie napi kwa muda au kama unatumia napi geuza na uanze kutumia diaper kwa muda
Usitumie suruali za ndani zitakazo hifadhi ulowecu kwa diaper
Tumia cream kama Fissmn Paste kwa rash. Usitumie uvumbi au lotion
Kama vipele havittoweka baada ya siku tatu au mtoto anaanza kupata malengelenge, muone daktari wa watoto.
Kumnyonyesha mwanao
Kwa watoto wengi, maziwa ya mama ndicho chakula bora zaidi. Ni rahisi kwa watoto wako kulisaga kulicho ya kununua (infont fomula). Maziwa ya mama humlinda mtoto kutokana na maradhi Fulani na waru wengine hudhani pia husaidia kumfanya mwanao mwerevu. Maziwa ya mama pia huwa na viwango vistahilivyo vya mafuta, sukari, maji na protein. Kumnyonyesha mwanao pia huhifadhi wakati na pesa.
Mnyonyesha mwanao anapokuwa na njaa au baada ya masaa 2-3. Kama mtoto wako anapata kuzichafua (kukonjolea na kukumia) nappy 6-8 ni ishara ya kwamba anashiba. Unafaa kungoja hadi mwanao atakapokuea na miezi 4-6 ili kuanza kumlisha chakula kikavu. Ni jambo la busara kuuliza daktari wako aina ya chakula unachofaa kumlisha mwanao au wakati unataka kumpatia chakula kipya ambacho hujawahi kumpatia tena.