Kumtafuta mchepuko wa mumeo

Ni kweli, lakini watu wanaoongoza kuja hapa MMU kuomba ushauri kwa maswala ya mapenzi, sasa sijui unataka tuwaignore?🤔😄
Hii inakuwa changamsha jukwaa mkuu🤣🤣we unadhani wanafata ushauri wetu.
 
Kwa hiyo yeye awe busy anaombea hako kaupendo ili hali mwanaume yuko busy ana enjoy 🤣 huo si utumwa jamani. Kwani nani kasema single maza hawaolewi na pia sio lazima kuolewa kama hujampata mtu sahihi wa kuthamini upendo wako kwake.
Hakuna mwanaume ambaye hachepuki. Hata huko atakapoenda michepuko atakutana nayo tu
 
Pole bibie watu wameshaur mengi binafsi nafikir ww ni mtu mzima unajua nn cha kufanya eni wei nikutakie ndoa njema
 
Ushauri uweke akilini.

Katafute mume akuoe huyo ni umiza kichwa na usimfuatilie wewe stopisha unyumba utapata gonjwa hatari unalijua.

Usipende kuumiza kichwa . Sio rahisi ila mtoto akufanyie uwe mtumwa .

Nyota inang'aa mama katengenezae upate mwingine .

Usimwoneshe ila olewa kwingine yeye abaki na huyo mwanamke wake ampendaye .

Mmeshakuwa na mahusiano ya serious why anakudharau nakuona waziada , anaenda hadi usiku Kisa mwanamke .


Ushauri part 11 mweke kwenye maombi ya siku 7 haitoshi siku 14.
Ushauri 111 nenda kaangalie Kwa mtaalam wa mahusiano Iangalie huyo dada kamuweka dawa ili amuone ndio wewe na ndio anaumuhimu so inabidi atolewe akujue maana hakujui anakuona ndio yule dada so Hana mpango na wewe
 
Umtafute umpige biti au ??.
 
Wanawake kama wewe ndio wa kuoa huyo bwege achana nae huyo
 
Kweli kabisa lazima aanze kujithamini mwenyewe ndo atathaminiwa, akimrusha roho kidogo tuu lazima mwanaume atapata wivu.
Ehee anatakiwa kuonewa wivu ukishaona mme anakuchukulia poa jua humrushi roho Yaan kumuupdate
 
Ushauri mzuri sana huu
 
Ukimtafuta tu huyo dada ww unafukuzwa na huyo dada ataolewa..
 
Aisee,pole sana dada,nakushauri kama una uwezo wa kumuacha huyo mwanaume muache mapema,atakusumbua sana mkishafunga ndoa,kama amekuonyesha dharau hivyo huyo hakupendi,ukiona mwanaume hajaoi hisia zako huyo Hana upendo na ww sema ni kwa sababu tu mna mtoto,jitahidi sana uanze kumtoa moyoni kidogo kidogo ili hata siku ukisikia kazaa na huyo dada usiumie zaidi,am speaking from experience,hata mimi yalinikuta nakapuuzia in the name of love and believing,yani nilikuwa nadanganywa naitikia tu kwa sababu nilimuamini kupita kiasi,kilichonikuta Mungu ndo anajua.
 
Umtafute huyo dada umwambie nini?. Deal na mumeo mtarajiwa, yeye ndio mzizi mkuu wa tatizo kuliko kupambana na matawi.
 
Kumtafuta mchepuko ni kujishushia heshma
Asiyejua thamani yako ni huyo aliyeamua kutafuta mchepuko
Upendo ukishahama, ni neema ya Mungu tu ndio inaweza urejesha. Mpaka mtu anafanya kila kitu hadharani bila hofu hapo jahazi lishaingia maji zamani sana. Akicheza huyo mchepuko atampindua asubuhi na mapema.
 
Hii inakuwa changamsha jukwaa mkuu🤣🤣we unadhani wanafata ushauri wetu.
Sasa Kuna haja gani ya kuomba ushauri alafu usifuate wowote ule.? Ila katika hao wapo ambao wanakuwa katika situations ambazo by themselves wanaona hawawezi na kuhitaji ushauri my dear.
 
Kwanza pole mamii, pili kwa jibu alilokupa angalia wewe ndiyo usijekuwa ni mchepuko...
Wanaume wana mengi sana, huenda mwenzako alikataa kuishi naye mpaka ndoa.
Wewe ikawa rahisi, anaweza enda funga ndoa akitokea hapo home kwenu.

Jitafakari mauhusiano yenu, jipe muda ongea na Mungu atakupa jibu, kama huyo ndiyo mtu sahihi aliyekuandalia ama lah.
Kila la kheri...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…