Kumtafuta mchepuko wa mumeo

Kumtafuta mchepuko wa mumeo

Mimi21

Member
Joined
Jun 11, 2021
Posts
24
Reaction score
33
Habari za muda huu ndugu zangu, ningependa kusaidiwa jambo.

Nimegundua kwamba mume wangu ana mchepuko, mwanzo alikua na michepuko ambayo sikuitilia maanani ila sasa kuna huyo dada yaani all the time wanapigiana simu imefika wakati akiwa off anatoka anaenda kushinda nae huko anarudi usiku sana.

Kimapenzi na ustaarabu nikaona nisika kimya kwasabu siku zote hua simuulizi kabisa hata kama nikijua katoka huko kuchepuka, huwa sipendi ugomvi namuacha tu ila huyu sasa ananitia wasiwasi. Imagine wanapigiana simu hadi saa kumi na mbili asubuhi.

Kwakweli naumia sana nikashindwa kuvumilia nikamuuliza mwenzangu kwa upole na unyenyekevu kuhusu huyo mwanamke, hakunibu vitu vinavieleweka zaidi akanambia and I quote "Unataka nisiwe narudi nyumbani si ndio?". Kuna sehemu tulikua tunaishi mwanzo tukahama kabla hatujaona (kila mtu alikua ana apartment yake) akanambia nikitaka kujua nikawaulize watu tuliokua tumepanga nao kule wanajua habari za huyo dada.

Natamani sana nimtafute huyo dada nipate closure tu. Kwa maana ndoa hatujafunga bado ni taratibu za mila tu ndo zimekamilika, akaniomba kwa wazazi kwasabu tuna mtoto.

Je, ni sawa nikimtafuta huyo dada?
 
Habari za muda huu ndugu zangu,,
Ningependa kusaidiwa jambo.
Nimegundua kwamba mume wangu ana mchepuko.. mwanzo alikua na michepuko ambayo sikuitilia maanani ila sasa

Natamani sana nimtafute huyo dada nipate closure tu. Kwa maana ndoa hatujafunga bado ni taratibu za mila tu ndo zimekamilika akaniomba kwa wazazi kwasabu tuna mtoto.

Je ni sawa nikimtafuta huyo dada?
Ni sawa 100% mtafute umjue

Ni lazima umjue mshindani wako

Sina shaka yeye anakujua vizuri na habari za wewe kumpa huyo bwana uno la upande upande anazo

Wewe tu ndio huna habari zake

Mtafute umjua usipuuze
 
IMG_3351.jpg
 
Kwa afya ya roho na mwili wako nakushauri usimtafute huyo mchepuko.

Kama unampenda mumeo na anakutreat vema, hakupigi na anakupa haki zako kama mke na mama mtoto wake basi tulia tu ukimuombea aweze epuka vishawishi.

Ila kama unaona huwezi basi jiondoe tu kimya kimya bila ugomvi wala shari
 
Wala usimtafute jitahidi uwe mtu wa furaha usimuulize kitu huyo mumeo vaa pendeza usiwe mtu wa kujali kuchelewa kwake japo ina kera sana uone kama haja badilika
Huu ushauri wako kwa MWANAMKE ambaye alishapenda na kumchukulia mwanaume aliyenae kama ndio soul mate wake ni ngumu kuufuata maana moyo ulishapenda, moyo ulisharidhika, moyo ulishataka na kujiaminisha kuwa ni mimi tu. Sasa sijui kama atakuelewa. Let's see bro
 
Kumbe hata kukuoa bado.

Hata usijishughulishe kuhangaika na huyo mdada mwaya sababu unaeza mpigia akakupa kauli ambazo utajuta kumtafuta mwishowe ukafungasha mabegi bure.
 
Ukimtafuta mchepuko ndo utazidi kuumia na atakuwa anakurusha roho, cha kufanya kuwa busy na issue zako kama huna kazi , tafuta kitu cha kukufanya uwe busy, jitahidi kuvaa, kupendeza na wikiend kutoka out na mwanao ata kwenda kula mihogo tuu au kutembelea ndugu, yani mume akiwa busy na mchepuko nawe kuwa busy na shughuli zako agiza hata chipsi kuku na big pepsi kulaaaaa 💃🏻💃🏻, life is too short, tafuta pesa tafuta pesa .
 
Back
Top Bottom