Kumsamehe aliyekusaliti

Ni vizuri uwe mwepesi kusamehe kwa sababu najua makosa hayakosekani, so ukiwa unaweka vitu moyoni huo moyo utakuza mzito kama sim tak mwisho wa siku kukosa furaha moyoni.

Ukisamehe unakua comfortable sana na unabarikiwa na Mungu, embu jiulize Mungu angekua hasamehi dhambi zako tungebaki wangapi hapa duniani? Kuna makosa mazito sana kusamehe ni ngumu ila ww ukiwa tayari vitu vinapita tu na love inakua mingi sana... ila kwenye mapenzi pagumu mno mkuu...
 
Ni kwel mkuu vp kwa mfano mwnamke akakussliti mara ya kwanza akakili na akaomba msamaha yakaisha alafu baada ya muda Tena karudia Yale Yale Tena vp unaweza msamehe

NB : bado anakujali na heshima iko pale pale yaan hajabadilika kitu
Anakuheshimu vipi wakati anakusaliti. Sijakuelewa
 
Mbona hakumsamehe lucipher alipoasi kule mbingini?
 
Kama simpendi namsamehe ......ila kama nampenda siwez aiseee naumia saana !!!!
Kuna ex alikuwa anawaambia wenzie huyu gf wangu ananivumilia,Kumbe mwenzie sijawah kumpenda[emoji23][emoji23] moyo ni kiza kinene
 
Ngoja namm nisamehe tuuu basi hakuna namna Tena sjui nmpende zaidi ili aondoe Ile hulka yake ya kuzoea kusaliti
Kusamehe ni kukipigia magoti kifo kiingie katika nyumba yenu.
Shikamoo!
 
Maisha marefu?
 
Mwanamke ni mvumilivu sana ikifikia sehem akakusaliti basi hatoweza kuacha hiyo tabia maana wanayo point of no return .....inashauriwa usimsamehe piga chiniiiii
 
Kama uchawi upo umerogwa siyo bure kama uchawi haupo lazima unashida katika akili.
 
Mungu mwenyewe alisalitiwa na shetani akamfukuza kwenye ufalme wake sembuse wewe mwanadamu.
Kumsamehe msaliti ni kujichimbia kaburi lako mwenyewe hata Mungu alishindwa, acheni kujitia wakomavu wa uvumilivu, mtaharibu maisha yenu.
 
Kusalitiwa inauma ila sisi kusaliti ni mtelezo tu hsina shida
 
Mimi mpenzi wangu akinisaliti anakutana na ngumi za kutosha halafu maisha yanaendelea akitaka kula kona kimpango wake sasa
 
yalinikuta nikaombwa msamaha nikasamehe kosa kubwa la hawa viumbe kama ana marafiki wanaokujua na kesi pia wanaijua jiandae maumivu

Baada ya msamaha tulienda vizuri tu adabu kama zamani kadri siku zinapozidi kwenda dharau zikaanza ukiongea nae basi lazima mashoga zake wajue na mambo ya mitandao haya

siku moja kama Mungu tu akaniongoza hebu mtafute muulize mustakabali wenu ndani ya huu mwaka mpya nikaambiwa baaadae tutaongea nikanyuti baadae kupiga simu naqmbiwa nacheki tamthilia nikapga usingizi
kesho yake night nikamjia hewani nikakuta yuko kwenye jam asubuhi kuuliza imekuwa kesi kwamba complaining nyingi na vitu ambavyo havieleweki
Nikapiga goti chini Mungu akasikiliza kilio changu nikamuacha alikuwa ni mtu amabae sio rahisi kumuacha

suala la kurudiana na mtu aliekusaliti ni kama kujiua mwenyewe samehe na move on
Mungu husikia kilio cha kila mja wake
mkuu Hapo umefunuliwa tu huyo mwenzako ni mtu wa aina gani usipoteze muda kumrekebisha utakwama kila wakati fanya maendeleo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…