Naomba nieleze kwa ufupi mambo muhimu yafuatayo, ambayo kama taifa inabidi tuwe serious nayo,kipindi hiki si cha mzaha kama baadhi ya watu wanavyodhani; Dr. Slaa ameeleza vizuri sana kuhusu ahadi anazotoa na zote zinatekelezeka. Nakumbuka Katika uchaguzi wa kenya wapinzani walieleza kuhusu elimu ya bure, lakini chama kilichokuwa madarakani wakati ule KANU walipinga sana na kusema haiwezekani. Lakini Upinzani uliposhinda tuliona elimu kenya ikitolewa bure(sina uhakika mpaka level gani). Kumbuka sisi tuna resource nyingi zaidi ya kenya. Lakini nasikia kikwete anapinga ahadi za Dr. Slaa na kueleza watanzania kuwa ahadi hazitekelezeki. NAOMBA NIWAMBIE WATANZANIA WENZANGU
Kumchagua/kumkubali kikwete kuwa Raisi wa jamuhuri ya muungano kwa mara nyingine ni kukubali yafuatayo:
Kumchagua/kumkubali kikwete kuwa Raisi wa jamuhuri ya muungano kwa mara nyingine ni kukubali yafuatayo:
- Ufisadi uendelee kama kawaida,
- Elimu bure mpaka form six hatuitaki
- Katiba mpya si muhimu kwetu haitusaidii chochote.
- Matumizi ya makubwa ya serikali ni sawa tu yaendelee kama kawaida