Kusema ukweli wananchi wa Tarime wana msimamo. Nipo huku kwetu Tarime kwa kweli kila kona ni UKAWA. Vijana wa Tarime wamehamasika kuunga mkono UKAWA kwa asilimia mia moja. Mgombea wa CCM wa Jimbo la Tarime Mjini kila akipita hakuna wa kumsikiliza. Leo badala ya kuzindua Kampeni katika viwanja vya Serengeti hapa mjini amekimbilia Buhemba kuogopa aibu. Kesho ni uzinduzi wa UKAWA hapa Tarime, kwa kweli kutakuwa ni mafuriko. Wananchi wamemueleza mgombea wa CCM asiharibu fedha yake aelekeze hizo fedha kwa familia yake kwa sababu hatapata ushindi. Kwenye ngazi ya Udiwani katika Kata ya Nyamisangura ndiyo usiseme. Mgombea wa UKAWA ameambiwa asifanye kampeni, UDIWANI ni wake. Uzuri wa Wakurya wakikukataa wanakueleza bila kukuficha. Mfano hai ni pale walipomueleza Nyambari Nyangwine kuwa asisumbuke hapati tena Ubunge na ndivyo ilivyotokea. TUWAIGE WENZETU WAKURYA WA TARIME WANA MSIMAMO KABISA.