kumekucha Kalenga kipindi cha lala salama

kumekucha Kalenga kipindi cha lala salama

ebaeban

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,205
Reaction score
2,707
Kwa hakika niko jimboni Kalenga kipindi cha lala salama kampeni za uchaguzi mdogo, CCM, Kijana anaangushwa na uwezo mdogo wa kujieleza na kuyajua kwa undani matatizo ya wana kalenga kwa kweli kama akipita basi atakuwa amebebwa na chama lakini uwezo hana, CHADEMA Dadad anajitahidi kumbe wanawake nao wanaweza,anayajua matatizo ya wanakalenga yanayowakabili mfano tatizo noti mbovu za shs 500 amelieleza vizuri kweli Tatizo la uduni wa elimu shule za kata amelielezea vizuri kweli Tatizo la uhaba wa soko la ulanzi amejitahidi kulieleza vizuri kweli Tatizo la watoto wa wakubwa kubebwa japokuwa uwezo hawana kama huyu mpinzani wake mtoto wa Mgimwa ambae hajui kabisan kuamka bila chai mwezi mzima amelieleza vizuri kweli Kwa hakika wana kalenga wanatarajia kupata mwakilishi mzuri ambae anayajua matazizo yao kiundani huyu dada wa CHADEMA, ki ukweli wanakalenga hawatajuta kumchagua mgombea wa CHADEMA #
 
Huyu dada yetu Grace yuko vizuri na anafaa kuwakilisha wana Kalenga!!! watajutia maamuzi yao baada ya muda mfupi tu iwapo hawatamchagua huyu mama!
 
wapi dada grace kamata mwiz meeeen mi utanikuta dodoma siku ya kuapishwa chadema udom wanakusubir watakupokea gairo 2taenda na wewe mpaka dodoma kwa maandamano
mungu ibariki tanzania
mungu ibariki chadema
mungu mbariki tendega
 
Naamini grace atakuwa mwarobaini wa matatizo ya wana kalenga cyo huyu mtoto wa pampac
 
SIKU ZOTE KURA NI siri na hilo litadhwihiri siku ya kupiga kura.

usishangilie wingi wa watu kukusikiliza kwani wengi si wapiga kura bali ni wanazi tu.

tuvute subra kujua ukweli.
 
SIKU ZOTE KURA NI siri na hilo litadhwihiri siku ya kupiga kura.

usishangilie wingi wa watu kukusikiliza kwani wengi si wapiga kura bali ni wanazi tu.

tuvute subra kujua ukweli.

Mkuu, kura ni siri? Mbona kwenye katiba mnadai iwe wazi?
 
Kila la heri kamanda lakini bado hamjasema mna wenye shahada za kura wangapi na kama mna wakala waaminifu na je ushindi mnaotegemea ni kwa asilimia ngapi. Ni lazima muwe na uwezo wa kutabiri mambo na hiyo itawapa hamasa wapiga kura.
 
Nakusifu kwa habari nzuri na inayojitosheleza.Kila la kheri Grace na chadema katika uchaguzi huu.
Hata hivyo kama CCM wenyewe walisema W.Mgimwa ni mzigo,huyu bila shaka naye atakuwa mzigo maana KAMA MTOTO WA NYOKA NI NYOKA,VIVYO HIVYO MTOTO WA MZIGO NAYE NI MZIGO.
 
SIKU ZOTE KURA NI siri na hilo litadhwihiri siku ya kupiga kura.

usishangilie wingi wa watu kukusikiliza kwani wengi si wapiga kura bali ni wanazi tu.

tuvute subra kujua ukweli.

hao unaosema si wapiga kura ipo siku watajitambau na kuwa na sifa za kupiga kura!
 
Kweli.CCM hubebana wao kwa wao.na hawana aibu.aibu walioipata Meru ya kumpitisha mtoto wa mbunge aliofariki.wanairudia tena Kalenga.lakini sioni ajabu kama mnawie alinyanyuliwa kwa nini na yeye asinyanyue wenzake?wanakalenga kamwe msikubali urith huo.mue ngangari kwa kutopoteza kura zenu kumchagua kamanda mama Grace.
 
Mkuu, kura ni siri? Mbona kwenye katiba mnadai iwe wazi?

Kama ni hivyo tupige kura za mlolongo kama mzee moi alivyofanya. Mnajipanga mstari kwenye picha ya mgombea unayemtaka hii hata kuchakachua huwezi.
 
Back
Top Bottom