Kumekucha CHADEMA Ilemela kesho

Kumekucha CHADEMA Ilemela kesho

Kesho Ijumaa CHADEMA wilaya ya Ilemela itarusha helkopa maeneo yote ya wilaya ya Ilemela.Makamanda Wanzagi,Damas na viongozi mbali mbali watanadi sera muhimu za CHADEMA.Pia watakagua maendeleo na kazi za maendeleo zilivyotekelezwa na Wananchi wakishirikiana na Wenyeviti wa serikali za mitaa.Igombe,Nyamilolelwa,Ilemela,Nyamhongolo,Buswelu,Nyamanoro,Pasiansi,Kilimahewa,Kirumba,Kitangiri,Igoma kaeni mkao wa kuwapokea Makamanda.PEOPLES POOOOOOOOOOWER
Buswelu asije na helicopter aje kwa barabara aone mahandaki kwenye barabara ya National to Ofisi ya wilaya
 
Kesho Ijumaa CHADEMA wilaya ya Ilemela itarusha helkopa maeneo yote ya wilaya ya Ilemela.Makamanda Wanzagi,Damas na viongozi mbali mbali watanadi sera muhimu za CHADEMA.Pia watakagua maendeleo na kazi za maendeleo zilivyotekelezwa na Wananchi wakishirikiana na Wenyeviti wa serikali za mitaa.Igombe,Nyamilolelwa,Ilemela,Nyamhongolo,Buswelu,Nyamanoro,Pasiansi,Kilimahewa,Kirumba,Kitangiri,Igoma kaeni mkao wa kuwapokea Makamanda.PEOPLES POOOOOOOOOOWER
Kamanda watanzania tatizo lao siyo Helkopta, waelezeni mtawafanyia nini ambacho CCM wameshindwa nyie Chadema mtakifanya siyo watu waje kuona Helkopta inatimua vumbi.
 
CCM ni wachawi, wantumia FISI.

ACT wao Zitto hupigwa na mikia ya Fisi kabla ya kufanya lolote.

Chadema ni wacha Mungu, huamini katika ubunifu, sayansi na teknolojia, hivyo hutumia Hutumia Helicopta.

Kuna kingine labda??
 
Kamanda watanzania tatizo lao siyo Helkopta, waelezeni mtawafanyia nini ambacho CCM wameshindwa nyie Chadema mtakifanya siyo watu waje kuona Helkopta inatimua vumbi.

Ni Fisi??
 
Wanakuja na helikopta ya nini? Waje na magari ili waone barabara zilivyo mbaya hasa jimbo la Ilemela kata za Buswelu,Ilemela,Bugogwa,Shibula na Sangabuye. Jimbo ambalo linaongozwa na mbunge Kiwia wa Chadema. Waangalie barabara ya Kiseke,ya kutokea airport kuelekea Igombe na nyinginezo zilivyo mbovu. Ni dharau kwa wapiga kura kwa viongozi hawa wa Chadema kutumia helikopta wakati wapiga kura wao wanapita kwenye mahandaki.
 
mtatuua na helkopita hii sasa sifa hadi ilemela helkopita cdm mnatumia vibaya ruzuku
 
Kesho Ijumaa CHADEMA wilaya ya Ilemela itarusha helkopa maeneo yote ya wilaya ya Ilemela.Makamanda Wanzagi,Damas na viongozi mbali mbali watanadi sera muhimu za CHADEMA.Pia watakagua maendeleo na kazi za maendeleo zilivyotekelezwa na Wananchi wakishirikiana na Wenyeviti wa serikali za mitaa.Igombe,Nyamilolelwa,Ilem ela,Nyamhongolo,Buswelu,Nyamanoro,Pasiansi,Kilimahewa,Kirumba,Kitangiri,Igoma kaeni mkao wa kuwapokea Makamanda.PEOPLES POOOOOOOOOOWER
 
PLZ DONT INTERUPT
CHADEMA TUPO KAZINI

Ilemela standup

CHADEMA wilaya ya Ilemela kesho kulitikisa jiji la Mwanza kwa kufanya mikutano 25 jimbo zima la Ilemela kwa Chopa,akiongea na mwandishi wa habari hii katibu wa CHADEMA wilaya hiyo na mtaalamu wa sheria na Siasa kamanda Damas Kimenyi,amewataka wakazi wa Ilemela kuwapokea kwa mikono miwili katika operation hiyo itakayozinduliwa kesho majira ya saa 5 asubuhi katika viwanja vya ofisi ya chama wilaya hicho,amesema operation hiyo itafahamika kwa jina la"MISHAGAWELA".

Kamanda Kimenyi amesema lengo la operation hiyo ni kuwaamsha wale waliolala kwenye usingizi wa pono ndani ya jimbo hilo na jiji zima kwa ujumla huku nchi ikitafunwa na wachache,umaskini ukitamalaki ,migomo nchi nzima na watendaji wa CCM kutopea kwenye ufisadi mkubwa wa fedha na rasilimali za nchi,katibu huyo wa Ilemela jimbo linaloongozwa na Mbunge Hyness Kiwia kupitia CHADEMA,anasema hata jina la operation hiyo"MISHAGAWELA" limebuniwa na wazee na viongozi wa wasukuma likiwa na maana ya "Amka kumekucha"lengo kubwa likiwa ni kuihamasisha jamii ya wasukuma na wananchi wote kwa ujumla kuamka na kujiandikisha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura,kupiga kura na kuzilinda mwezi wa kumi,pamoja na kuhamasisha uimarishaji wa walinzi wa chama 200 kila kata.

Katibu huyo amewataja washiriki wengine wa tukio hilo la kihistoria na ambao watakuwa pia ni miongoni mwa wahutubiaji na waratibu wa mikutano hiyo kuwa ni pamoja na kamanda wa Vikosi vya majini CHADEMA Alphonce Mawazo ambaye pia ni mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Geita,Viongozi wa Kanda ya Ziwa Vicktoria,Edwin Sarungi ambaye ni mhazini wa CHADEMA wilaya hiyo,mwenyekiti wa Vijana,katibu wa balaza wazee,Balaza la wanawake,katibu mwenezi na Balaza la Vijana .
Katibu huyo ametoa wito kwa wakazi wa wilaya ya Ilemela kujitokeza kwa wingi.
 
Back
Top Bottom