Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza kuitisha Mkutano Mkuu Maalum wa Taifa utakaofanyika kwa njia ya mtandao siku ya Jumamosi, Julai 26, 2025 kuanzia saa 2:00 asubuhi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vyetu vya kuaminika ndani ya CCM, tangazo hilo lililotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) wa Idara ya Oganaizesheni, Issa Haji Ussi Gavu, kwa Makatibu wa Wilaya na wa Mikoa wa CCM linaeleza kuwa mkutano huo utaongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Katika maandalizi ya mkutano huo, Makatibu wa Wilaya na wa Mikoa wa CCM wameelekezwa kuwaelekeza wajumbe wote wa Mkutano Mkuu waliopo katika maeneo yao kuhakikisha wanakusanyika katika ofisi za CCM za Wilaya au Mikoa, kutegemeana na nafasi, ili kushiriki kwa pamoja.
Taarifa hiyo pia imeweka msisitizo juu ya maandalizi ya mazingira ya kufanikisha mkutano huo, ikiwemo kuweka vifaa vya kuoneshea kama televisheni au skrini, viti vya kutosha, na kuhakikisha mazingira ni tulivu pamoja na kuwa na miundombinu imara ya mtandao.
Jambo TV imezungumza na makatibu wa CCM wa wilaya na mikoa mbalimbali ambao wamethibitisha kupokea tangazo hilo huku wakieleza kuanza maandalizi ya mkutano huo.
Hata hivyo ajenda zenyewe za mkutano hazijawekwa wazi huku kukiwa na tetesi juu ya uwepo wa maamuzi kadhaa mazito yatakayopitishwa na mkutano huo wakati ambao chama hicho kiko katika mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali za chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka vyanzo vyetu vya kuaminika ndani ya CCM, tangazo hilo lililotolewa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC) wa Idara ya Oganaizesheni, Issa Haji Ussi Gavu, kwa Makatibu wa Wilaya na wa Mikoa wa CCM linaeleza kuwa mkutano huo utaongozwa na Mwenyekiti wa CCM Taifa, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Katika maandalizi ya mkutano huo, Makatibu wa Wilaya na wa Mikoa wa CCM wameelekezwa kuwaelekeza wajumbe wote wa Mkutano Mkuu waliopo katika maeneo yao kuhakikisha wanakusanyika katika ofisi za CCM za Wilaya au Mikoa, kutegemeana na nafasi, ili kushiriki kwa pamoja.
Taarifa hiyo pia imeweka msisitizo juu ya maandalizi ya mazingira ya kufanikisha mkutano huo, ikiwemo kuweka vifaa vya kuoneshea kama televisheni au skrini, viti vya kutosha, na kuhakikisha mazingira ni tulivu pamoja na kuwa na miundombinu imara ya mtandao.
Jambo TV imezungumza na makatibu wa CCM wa wilaya na mikoa mbalimbali ambao wamethibitisha kupokea tangazo hilo huku wakieleza kuanza maandalizi ya mkutano huo.
Hata hivyo ajenda zenyewe za mkutano hazijawekwa wazi huku kukiwa na tetesi juu ya uwepo wa maamuzi kadhaa mazito yatakayopitishwa na mkutano huo wakati ambao chama hicho kiko katika mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi mbalimbali za chama hicho kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.