Basi bwana majuzi kayi tukiwa msibani akaja mwanafamilia mmoja kijana tu tuliskiaga ameokoka Akaanza kusalimia wazee hukooo alipomaliza akaja kunikuta nimekaa na dadangu yule mwenye WOWOWO kubwa alieambiwa "pima iyo" pale moshi mjini.
Sasa sister Wangu mwenye WOWOWO ni mtata kuliko Penny, alipomwona anakuja akaniambia Penny acha niongee mimi leo Mtumishi wa bwana akaja akatusalimia na kutoa pole nyingi kama kawaida yake
Sister Wowowo: Asante sana Mtumishi, eh za masiku jamani sijakuona muda, uko wapi, kazi wap, familia salama watoto je
Mtumishi: Mimi Mzima Dada kwa uweza wa Mungu naendelea vizuri sana
Money Penny: Umeoa?!
Mtumishi: kwa Sasa sijawowa ila namwamini Bwana atanipa Mke
Sister Wowowo: Bwana gan akupe Mke? !
Mtumishi: Bwana Yesu
Sister Wowowo: Yesu anakupaje Mke labda
Mtumishi: ananiwezesha kujua kwenye maombi, maono
Money Penny: kwenye maono inakuwaje
Mtumishi: ananiletea picha ya Mke wangu na nikimwona live namjua
Sister Wowowo: kwahiyo tangu umpate bwana Yesu mpaka Sasa umeshampata mkeo kwenye maono au bado
Mtumishi: bado sijampata bado hajanionyesha
Money penny: una umri gan Mtumishi: miaka 34
Sister Wowowo: we bado bikra?!
Mtumishi: ndio
Sister wowowo: hujawahi kula tunda la Eden tangu uzaliwe?!
Mtumishi: nimeokoka nikiwa na miaka 12 mpaka leo sijampata Mke wa kuwowa namwamini Mungu very soon atanipa
Sister Wowowo: kwahiyo wewe hausikiagi nyege?!
Mtumishi: hapana
Money Penny: miaka 34 husikii nyege?!
Mtumishi: hapana kwasababu nguvu za Mungu zimenifunika ananiwezesha siskii nyege wala hamu ya mwanamke.
Doh, namshukuru Mungu nimekaa Moshi aisee, Moshi kuna miujiza mingi hataree... juzi wamesema pima hio, leo Mtumishi hand nyege. ..
Ngoja niendelee kukaa Moshi huenda nikaandika kitabu kabisa sio kwa vituko hivi.
Eti ni kweli wanaume waliookoka hawasikii hamu ya mwanamke?!
Kumbe kuna wanaume mabikra wenye miaka 34 huku Tz?!
Kiru, Aikambe wanaume wakichaga!