Kumbe wanachopewa wazee NSSF ni msaada tu

Kumbe wanachopewa wazee NSSF ni msaada tu

Starton

Member
Joined
Jun 4, 2018
Posts
18
Reaction score
14
Siku ya tarehe 1/6/2018 baadhi ya wazee walienda makao makuu ya NSSF kufuatilia pension ya mwezi wa tano ambao baadhi yao hawajapewa hadi sasa kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.

Wazee wale wakionekana kuchoka na kukata tamaa, mmoja wa wale akina dada aliyekuwa anawahudumia pale makao makuu ghorofa ya 10 nadhani aliona kwake ni usumbufu akatoa kauli ya kuwaambia wale wazee kuwa 'hata hivyo hizi pension tunazowapa ni msaada tu NSSF inatoa kwenu hamjastahili kuzipata'.

Wazee wale walipigwa na butwaa kwa hiyo kauli na mmoja kati ya wale wazee alishindwa kujizuia na akamwambia yule dada kuwa hata yeye Mungu akimjalia atafikia umri kama wao na vilevile Mwenyezi Mungu akipenda anaweza asifike.

Wazee wale waliambiwa kuacha namba za simu warudi nyumbani watafahamishwa.Sasa kwa jambo hili la wazee kukosa pension na majibu tata ya kiwango hiki tunadhani NSSF kuna shida.

Ni vyema NSSF wakalitolea kauli hili swala kwa ujumla wake kwani watu wameanza kuwa na tafsiri mbaya.Sasa mifuko ikishaunganishwa na wanachama wakawa wengi zaidi hali itakuwaje?
 
bado najiuliza maswali mengi sana. Hivi malalamiko yanayotoka katika mifuko ya jamii huwa hayawafikii wahusika? Mbona kila mara ni kero?
 
Hivi si nasikia nidhamu imeimarika miongoni mwa watumishi wa umma, hayo majibu mabayamabaya na huduma mbovu nssf imekuwaje tena?
 
Siku ya tarehe 3/6/2018 baadhi ya wazee walienda makao makuu ya NSSF kufuatilia pension ya mwezi wa tano ambao baadhi yao hawajapewa hadi sasa kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.

Wazee wale wakionekana kuchoka na kukata tamaa, mmoja wa wale akina dada aliyekuwa anawahudumia pale makao makuu ghorofa ya 10 nadhani aliona kwake ni usumbufu akatoa kauli ya kuwaambia wale wazee kuwa 'hata hivyo hizi pension tunazowapa ni msaada tu NSSF inatoa kwenu hamjastahili kuzipata'.

Wazee wale walipigwa na butwaa kwa hiyo kauli na mmoja kati ya wale wazee alishindwa kujizuia na akamwambia yule dada kuwa hata yeye Mungu akimjalia atafikia umri kama wao na vilevile Mwenyezi Mungu akipenda anaweza asifike.

Wazee wale waliambiwa kuacha namba za simu warudi nyumbani watafahamishwa.Sasa kwa jambo hili la wazee kukosa pension na majibu tata ya kiwango hiki tunadhani NSSF kuna shida.

Ni vyema NSSF wakalitolea kauli hili swala kwa ujumla wake kwani watu wameanza kuwa na tafsiri mbaya.Sasa mifuko ikishaunganishwa na wanachama wakawa wengi zaidi hali itakuwaje?
Ni kweli kauli za dada huyo ni tata, mimi aliwahi kuniambia kuwa NSSF haihusiki na ucheleweshwaji wa malipo hivyo kama kina malalamiko yapelekwe shirika la Posta wao hawahusiki! Chakujiuliza wastaafu wanamkataba gani na Posta? Ukweli ni kwamba kuna unyanyasaji mkubwa kwenye malipo ya mwezi kwa wastaafu.
 
Ni kweli kauri za dada huyo ni tata, mimi aliwahi kuniambia kuwa NSSF haihusiki na ucheleweshwaji wa malipo hivyo kama kina malalamiko yapelekwe shirika la Posta wao hawahusiki! Chakujiuliza wastaafu wanamkataba gani na Posta? Ukweli ni kwamba kuna unyanyasaji mkubwa kwenye malipo ya mwezi kwa wastaafu.
Huyo dada yupo ofisi gani nani namba ngapi , au tutajie alivyo ili ashughulikiwe kama wengine wanaotumia madaraka vibaya na sheria ifuate mkondo.
 
Wale wafanyakazi wa makao makuu nssf, especially wadada wana majibu ya shombo sijapata ona.
 
Huyo dada yupo ofisi gani nani namba ngapi , au tutajie alivyo ili ashughulikiwe kama wengine wanaotumia madaraka vibaya na sheria ifuate mkondo.
Anyway najua huwezi kumshughulikia ila yupo ghorofa ya kumi chumba cha kwanza kushoto zilipo mashine za photocopy. Tatizo mfuko hauna msimamizi na hauhangaikii matatizo ya wastaafu wahusika wamejikita kwenye kugawana pesa zisizo na mwenyewe.
 
Wale wafanyakazi wa makao makuu nssf, especially wadada wana majibu ya shombo sijapata ona.
Huwezi kuamini hasa pale anapomjibu majibu yaliyopinda mtu ambaye ni makamo ya babu yake kule kijijini.Anajisikia na anajiona yupo 'on top of everything'.Hakika nssf ni kaa la moto kwa wastaafu.Wazee wale ni 'helpless' hata wanapojibiwa majibu ya ovyo hubaki kimya na kubaki kumshuru Mungu tu.
 
Haya ni mateso makubwa kwa hawa Wazee. Nashauri Serikali iingilie kati.
 
Ni kweli kauli za dada huyo ni tata, mimi aliwahi kuniambia kuwa NSSF haihusiki na ucheleweshwaji wa malipo hivyo kama kina malalamiko yapelekwe shirika la Posta wao hawahusiki! Chakujiuliza wastaafu wanamkataba gani na Posta? Ukweli ni kwamba kuna unyanyasaji mkubwa kwenye malipo ya mwezi kwa wastaafu.
Mmh!
 
Back
Top Bottom