EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Wabongo jamani wana bongo, kumbe wengi spana mkononi! Nimeamini kabisa kwamba usianzishe ugomvi ukapigana unaweza kuua.
Karibu Wabongo wote ni wagonjwa, ukitaka uthibitisho mwulize Babu wa Loliondo. Msururu ule wa wazee, vijana, wanawake kwa wanaume, kwenda Samunge ni uthibitisho tosha kabisa, kwamba tulikuwa tunajikausha tu kumbe iko gonjwa.
Vigogo na masikini, sooote maselule tupu. Kikombe cha Babu kimetutanabahishia kuwa kumbe ni ujanja tu, hatuna kitu, nani atabisha kuwa hajakanyaga miwaya, lakini akifika kwa Babu anasingizia kisukari? Wapo wengi wa aina hiyo, tunashukuru Babu hapimi.
Na kama Babu angekuwa na hadubini za kupimia virusi, naamini Wawa Lali asingepiga marufuku haya mapaparazzi kumuhoji na kumpiga picha Babu, kwa sababu hata hivyo nani angejipanga msururu ule kupimwa ngoma?
Thubutu!
Karibu Wabongo wote ni wagonjwa, ukitaka uthibitisho mwulize Babu wa Loliondo. Msururu ule wa wazee, vijana, wanawake kwa wanaume, kwenda Samunge ni uthibitisho tosha kabisa, kwamba tulikuwa tunajikausha tu kumbe iko gonjwa.
Vigogo na masikini, sooote maselule tupu. Kikombe cha Babu kimetutanabahishia kuwa kumbe ni ujanja tu, hatuna kitu, nani atabisha kuwa hajakanyaga miwaya, lakini akifika kwa Babu anasingizia kisukari? Wapo wengi wa aina hiyo, tunashukuru Babu hapimi.
Na kama Babu angekuwa na hadubini za kupimia virusi, naamini Wawa Lali asingepiga marufuku haya mapaparazzi kumuhoji na kumpiga picha Babu, kwa sababu hata hivyo nani angejipanga msururu ule kupimwa ngoma?
Thubutu!