Kumbe michango bado ipo shule za serikali!

Kumbe michango bado ipo shule za serikali!

Mkwere Sumbawanga

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2015
Posts
745
Reaction score
660
Habari Wana JF
Katika Joining Instructions za form five naona michango kama vile ya madawati bado ipo, hivi hadi awamu hii ya 5 bado ipo mm nlijua imeisha.

Kwa mfano Jangwani Sekondari, Michango mingine ya shule inayotakiwa kulipiwa ni
1.Tsh. 10,000/- kwa ajili ya taaluma
2.Tsh 15,000/- kwa ajili ya dawati
3.Tsh. 10,000/- kwa ajili ya tahadhari
4.Tsh. 15,000/- kwa ajili ya ulinzi
5.Tsh. 15,000/- kwa ajili ya usafi

Unaweza pitia attachment ya mifano ya joining instructions za baadhi ya shule hapa chini
 

Attachments

Michango imeondolewa Elimu msingi tu kwa sekondari inaendelea. Elimu msingi inaishia kidato cha NNE. Kuanzia kidato cha tano hadi cha sita ni sekondari. Shule ulizotaji zinatoa Elimu ya sekondari, tuna imani hapo mbeleni serikali itafuta na kwa ngazi ya sekondari
 
Mkuu michango imeondolewa kwa wanafunzi wa kuanzia chekechea hadi kidato cha nne tu. Waliobaki wataendelea kulipa michango kama ilivyokuwa miaka iliyopita.Chakuangalia ni kuwa wakuu wa shule wasio waaminifu wanaweza kuongeza michango kwa wanafunzi wa vidato vya V na VI ili kufidia michango iliyofutwa na serikali.
 
Michango imeondolewa Elimu msingi tu kwa sekondari inaendelea. Elimu msingi inaishia kidato cha NNE. Kuanzia kidato cha tano hadi cha sita ni sekondari. Shule ulizotaji zinatoa Elimu ya sekondari, tuna imani hapo mbeleni serikali itafuta na kwa ngazi ya sekondari

asante mkuu nimekupata vizuri
 
Mkuu michango imeondolewa kwa wanafunzi wa kuanzia chekechea hadi kidato cha nne tu. Waliobaki wataendelea kulipa michango kama ilivyokuwa miaka iliyopita.Chakuangalia ni kuwa wakuu wa shule wasio waaminifu wanaweza kuongeza michango kwa wanafunzi wa vidato vya V na VI ili kufidia michango iliyofutwa na serikali.

hapo sawa
 
Hii elimu bure kuna wanafunzi walienda Shule bila madaftari wala uniform eti elimu bure.
 
Kwani umesahau kuwa elimu bure mwish kidato cha nne?
 
Back
Top Bottom