wakunyonya
JF-Expert Member
- Feb 5, 2024
- 858
- 2,058
Aise! Maisha siyo lelemama! Katika pitapita zangu kwenye mitandao ya kijamii nikakutana na mijadala ya bei za kupaki bodaboda katika vijiwe mbalimbali, kwa Dar na mikoani.
Kilichonishangaza, mfano kwa Dar, vijiwe vingi kuanzia Laki Tano na kuendelea. Ili upake boda yako kijiweni, mfano stendi ya Magufuli nasikia ni Laki Nane (800K), Ubungo Terminal Milioni moja na Laki Tano (1.5m), Kimara Terminal Laki Tano (500K), na hapo unaambiwa nafasi zimejaa, hivyo usubiri mpaka mtu atoke.
Baadhi ya wadau wakauliza: “Hizo hela hupelekwa wapi?” Majibu ni kuwa hupelekwa katika halmashauri husika. Nikajiuliza, hawa madogo wanaoingia boda za mkataba wanatoboa vipi kwa milolongo:
Kilichonishangaza, mfano kwa Dar, vijiwe vingi kuanzia Laki Tano na kuendelea. Ili upake boda yako kijiweni, mfano stendi ya Magufuli nasikia ni Laki Nane (800K), Ubungo Terminal Milioni moja na Laki Tano (1.5m), Kimara Terminal Laki Tano (500K), na hapo unaambiwa nafasi zimejaa, hivyo usubiri mpaka mtu atoke.
Baadhi ya wadau wakauliza: “Hizo hela hupelekwa wapi?” Majibu ni kuwa hupelekwa katika halmashauri husika. Nikajiuliza, hawa madogo wanaoingia boda za mkataba wanatoboa vipi kwa milolongo:
- Pesa ya Boss
- Leseni
- Latra
- Kijiwe