Kumbe Kick Boxing marufuku Zanzibar

Mwana Mtoka Pabaya

JF-Expert Member
Apr 22, 2012
15,118
16,470
Dakika chache zilizopita nikisikiliza kipindi cha michezo Radio One, nimesikia kituko cha mwaka. Ndani ya ardhi ya Zanzibar, mchezo wa Kick Boxing ni marufuku.

Waziri wa michezo wa Zanzibar amemjibu mjumbe wa Baraza la Wawakilishi aliyetaka kujua ni lini sheria ya kupiga marufuku mchezo wa Kick Boxing itaondolewa na Zanzibar iruhusiwe kushiriki mchezo huo hatimaye kuipa Zanzibar jina katika ramani ya mchezo huo duniani.

Waziri amejibu kuwa sheria hiyo haitaondolewa kamwe, ili kumuenzi Hayati Karume aliyepiga marufuku michezo ya ngumi zenye muelekeo huo. Pamoja na hilo, waziri pia amesisitiza kuwa mashindano ya Tusker Challenge Cup hayatafanyika Zanzibar kwa kuwa yana udhamini wa POMBE.

Maswali yangu:
1. Tunaacha kufanya michezo itakayotoa ajira kwa ajili ya kumuenzi mtu?
2. Kuna nchi ambayo TENDE na HALUA ziliwahi kudhamini mashindano mpk Zanzibar ikatae pombe?
3. Zanzibar haipokei misaada toka nje? Kama inapokea, hawajui kuwa kuna kodi za mivinyo katika hizo fedha wanazopokea?
 
Dakika chache zilizopita nikisikiliza kipindi cha michezo Radio One, nimesikia kituko cha mwaka. Ndani ya ardhi ya Zanzibar, mchezo wa Kick Boxing ni marufuku.Waziri wa michezo wa Zanzibar amemjibu mjumbe wa Baraza la Wawakilishi aliyetaka kujua ni lini sheria ya kupiga marufuku mchezo wa Kick Boxing itaondolewa na Zanzibar iruhusiwe kushiriki mchezo huo hatimaye kuipa Zanzibar jina katika ramani ya mchezo huo duniani.Waziri amejibu kuwa sheria hiyo haitaondolewa kamwe, ili kumuenzi Hayati Karume aliyepiga marufuku michezo ya ngumi zenye muelekeo huo. Pamoja na hilo, waziri pia amesisitiza kuwa mashindano ya Tusker Challenge Cup hayatafanyika Zanzibar kwa kuwa yana udhamini wa POMBE.Maswali yangu:1. Tunaacha kufanya michezo itakayotoa ajira kwa ajili ya kumuenzi mtu?2. Kuna nchi ambayo TENDE na HALUA ziliwahi kudhamini mashindano mpk Zanzibar ikatae pombe?3. Zanzibar haipokei misaada toka nje? Kama inapokea, hawajui kuwa kuna kodi za mivinyo katika hizo fedha wanazopokea?
mkuu mbavu zangu hoi hapo kwenye udhamini wa tende na halua
 
Kuna debate kubwa kuhusu michezo ya impact na jinsi inavyosababisha "brain concussions" nchi zilizoendelea. Kiasi mpaka wana re evaluate safety measures. This is most evident in American Football, but also seen in professional boxing.

One has only to look at how Muhammad Ali has become vegetative to say, business interests aside, maybe Karume, amidst all his buffoonery, had a case after all.

Especially given the time, for such a young nation with meager resources.
 
kwa kipindi hicho ilipowekwa sheria hiyo zanzibar ilikua ni taifa lililo katika umoja wa kiislam OIC lakini baada ya muungao kufanyika si muda mrefu watanganyika wakafanya kila wanacho fanya na kuindoa zanzibar katika umoja huo kwa maana hiyo karume aliikataa michezo hiyo kufanyika zanzibar kwa sababu ilikua haiendani na tamaduni zetu za kizanzibar na hata wakati huo ilikua hakuna mabaa wala makanisa ila makanisa ilikua ni mawili tu amabayo yalijengwa toka enzi sa ukoloni amabalo ni kanisa la mkunazini na kanisa la minara miwili liliopo shangani kwa maana hiyo karume alijua wazanzibar wana utamaduni wao na utamaduni wao unatokana na tamaduni za kiislam mchezo wa ngumi katika uislam ni haram kwa iyo haukufaa kuletwa zanzibar na tunaomba iendelee hivyo daima kama watanganyika watatukubalia manaake zanzibar hatuna nguvu hiyo ila watanganyika wakiamua hata leo inawezekana ukafanyika na kuhusu pombe mimi nawashangaa sana viongozi wetu wa zanzibar matangaazo yasifanyike ila kuingizwa na kuuzwa hakuna tabu na mabaa kila kona masikini zanzibar
 
kwa mamlaka niliyojipa mimi mwenyewe natoa ruksa kwa wazanzibar kucheza kick boxing...ila sharti moja watekeleze...wacheze huku wakiwa wamevaa kanzu.lol
 
mkuu mbavu zangu hoi hapo kwenye udhamini wa tende na halua

Hawa kina yahe wana mbwembwe kukataa udhamini wa Pombe na Sigara, basi wadhaminiwe na madawa ya kulevya ambayo kule kwao ni kama sigara huku bara
 
Dakika chache zilizopita nikisikiliza kipindi cha michezo Radio One, nimesikia kituko cha mwaka. Ndani ya ardhi ya Zanzibar, mchezo wa Kick Boxing ni marufuku.

Waziri wa michezo wa Zanzibar amemjibu mjumbe wa Baraza la Wawakilishi aliyetaka kujua ni lini sheria ya kupiga marufuku mchezo wa Kick Boxing itaondolewa na Zanzibar iruhusiwe kushiriki mchezo huo hatimaye kuipa Zanzibar jina katika ramani ya mchezo huo duniani.

Waziri amejibu kuwa sheria hiyo haitaondolewa kamwe, ili kumuenzi Hayati Karume aliyepiga marufuku michezo ya ngumi zenye muelekeo huo. Pamoja na hilo, waziri pia amesisitiza kuwa mashindano ya Tusker Challenge Cup hayatafanyika Zanzibar kwa kuwa yana udhamini wa POMBE.




Maswali yangu:
1. Tunaacha kufanya michezo itakayotoa ajira kwa ajili ya kumuenzi mtu?
2. Kuna nchi ambayo TENDE na HALUA ziliwahi kudhamini mashindano mpk Zanzibar ikatae pombe?
3. Zanzibar haipokei misaada toka nje? Kama inapokea, hawajui kuwa kuna kodi za mivinyo katika hizo fedha wanazopokea?

mbona timu yao inashiriki mashindano hayo...au inakuwa harami yakifanyika Zanzibar,ila ikiwa nje ya Zanzibar inakuwa poa......mbombo ngafu naloli!
 
mbona timu yao inashiriki mashindano hayo...au inakuwa harami yakifanyika Zanzibar,ila ikiwa nje ya Zanzibar inakuwa poa......mbombo ngafu naloli!

Inashiriki wapi mkuu? Usije ukawa unachanganya na Boxing, hapa nazungumzia KICK BOXING, ile mix ya mateke ngumi na vichwa, hata meno yanaruhusiwa
 
ok,kuna sehemu nafikiri umeongelea kwamba pombe ni haram huo upande mwingine na katu mashindano ya Tusker haywezi katu kufanyika huko,nami nimaongezea tu hapo kwamba mbona kama pombe ni haramu Zanzibar heroes wamekuwa wnashiriki mashindano ya Tusker?...ni hilo tu nafikiri nimeeleweka

Inashiriki wapi mkuu? Usije ukawa unachanganya na Boxing, hapa nazungumzia KICK BOXING, ile mix ya mateke ngumi na vichwa, hata meno yanaruhusiwa
 
ok,kuna sehemu nafikiri umeongelea kwamba pombe ni haram huo upande mwingine na katu mashindano ya Tusker haywezi katu kufanyika huko,nami nimaongezea tu hapo kwamba mbona kama pombe ni haramu Zanzibar heroes wamekuwa wnashiriki mashindano ya Tusker?...ni hilo tu nafikiri nimeeleweka

Ah, akili nzuri ukiwa nayo bana. Hata kuilaani Marekani na kuwaita makafir ni sawa. at the same time nimemuona Kakke ubalozini anaomba viza, sijui anataka nini kwa makafir, na akinyimwa atalalama huyo as if huko anaenda kuhiji
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom