Waswahili wanasema Waarabu wa Pemba hujuana kwa Vilemba..hii ikiwa na maana zaidi kufikiria kwamba kila mwarabu ni Mpemba..Vilemba vyao ndio kitambulisho na sii rangi au lugha!Wakuu tatizo la Tanzania si nani kasema nini lini na wapi. Cha msingi ni nani kafanya nini lini na wapi. Maneno ya hawa woooote JK na genge lake yamekuwa na utata mara nyingi sana. Kitakachosemwa kinaweza kumaanisha kitu kingine kabisa au ni mtego wa kumyaka ngedere mwingine aliye mbali!!!
Mkuu,
Tutegemee nini kutoka kwako pale unapotaka kulazimisha hoja juu ya JK dhidi ya Lowasa?
Kauli ya JK haipingani kwa namna yeyote na hiyo kauli ya Lowasa.
Lowasa amesema zijengwe hoteli nyingi na JK amesisitiza zisijengwe kiholela ni lazima ziwe na ubora wa hali juu zitazovutia watalii. Kwa maana hiyo basi hata zikijengwa 1000 lakini zikiwa nzuri kama Bilila, RUXAAA!!!!!
rejea kugeuka mbogo kwa jk na excuses za wasimamizi juu ya mahela yale!!!!!!!!!!!!!!!!!! Kichekeshowandugu kwenye siasa au ungwini hakuna aliye sahihi na ambaye si sahihi, kilichopo ni kujenga hoja na kuitetea hoja.
Kikwete amewahi kutofautiana kikauli na lowassa mara nyingi, mojawapo ikiwa ni ile ya "mamilioni ya jakaya". Lowassa alitaka watendaji wa benki wasilete urasimu wa kutoa fedha zile, na kikwete akasema fedha zile ni mikopo, na taratibu zote za kibenki za kugawa mikopo nafuu zifuatwe, na hakuna kugawa fedha kiholela holela. Ni hoja tu, na jinsi mtu anapoweza kuzijenga na kukubalika.
Na wakati mwingine mwenye kisu kikali ndiye mla nyama, na jk ana kisu cha urais, na mara nyingi yeye husema mwishoni.
Mzee Mwanakijiji mwanzo nilikuona kama mtu mwenye busara lakini sasa naanza kupata mashaka kidogo kwamba ndiye mwanakijiji huyu huyu aliyekuwa anatuletea hadithi za kuvutia au mwingine.
Date::7/11/2009
Kikwete apinga hoteli kujengwa mbugani
Na Peter Edson
RAIS Jakaya Kikwete amepinga hoja ya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowasa aliyoitoa bngeni enzi za uongozi wake ya kutaka zijengwe hotel nyingi maeneo ya hifadhi za taifa.
Badala yake Rais Kikwete ameiagiza Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kuwa inadhibiti ujenzi holela wa hoteli katika maeneo ya mbuga za wanyama.
Akizungumza wakaki wa uzinduzi wa hoteli ya kitalii ya Bilila Kempinsk yenye hadhi ya nyota tano katika mbuga ya wanyama ya Serengeti, Rais Kikwete alisema kama kutakuwepo na ujenzi holela wa hotel katika mbuga baadaye kunaweza kuleta athari kwa wanyama.
Tunahitaji hoteli nzuri za kitalii zenye sifa na siyo kila mtu aje mbugani kujenga hoteli. Haitaleta maana yeyote, hivyo nawagiza ninyi Tanapa (Shirika la Hifadhi la Taifa) na wizara husika kusimamia vyema jambo hili, alisema Kikwete.
Mwaka 2007, Lowasa aliwahi kulieleza bunge kuwa serikali inakusudia kuanza kujenga hotel kwa wingi katika maeneo ya mbuhgani kwa lengo la kuvutia watalii kutokana na ukosefu wa hoteli zenye hadhi nchini.
Alisema sekta ya utalii ni eneo muhimu katika ukuaji wa uchumi hapa nchini kwani katika kipindi cha mwaka 2007/2008 sekta hiyo iliweza kuchangia pato la taifa kwa asilimia 17.2 na kuingiza fedha za kigeni kwa asilimia 25, jambo ambalo halikuwahi kutokea huko nyuma.
Alisema kukamilika kwa hotel hiyo ni sehemu ya kutangaza utalii katika mbuga ya Serengeti nje ya nchi, hivyo ni vema wamiliki na wafanyakazi katika hotel hiyo wakafanya kazi kwa uaminifu ili kuvutia zaidi wawekezaji.
Tutapokea watalii wengi katika hoteli hii, lakini hata sisi tumepata ajira kutokana na kukamilika kwa hoteli hii, msiiharibu, ipendeni ili nayo iendelee kuwalea, alisema Rais Kikwete.
Alisema hivi sasa Serikali ipo katika mchakato wa kupunguza kiwango cha malipo kwa hati ya kusafiria kwa watalii kutoka asilimia 100 hadi kufikia 50 kwa mtalii mmoja, lengo likiwa ni kuondoa vikwanzo vinavyosababisha kupungua kwa watalii nchini hasa katika kipuindi hiki cha kuyumba kwa uchumi duniani.
Mwananchi Tanzania Newspaper(MCL)