Ndugu wanabodi,
Ningeomba sana tujifunze kusoma between the lines kisha kama mbayuwayu tuchanganye na za kwetu..
Maelezo haya hapa yanajieleza vizuri sana toka barua aliyoandika Jairo na kipande hiki ndicho hasa tunatakiwa kukitazama. Kinasema hivi:-
"Gharama hizi kubwa zimesababishwa na kupanda kwa gharama za posho kutoka Sh60,000 mpaka Sh200,000, Sh50,000 hadi Sh150,000 na Sh30,000 hadi Sh100,000 kwa wenyeviti na makatibu, wajumbe na sekretarieti sawia," inaeleza sehemu ya waraka huo uliondikwa na Jairo na kuongeza:
"Kwa kuwa bajeti ya wizara ya 2009/2010 ilikadiriwa kwa viwango vya zamani, ni dhahiri wizara haiwezi kubeba gharama hizi peke yake. Hivyo inashauriwa Wizara igharamie 96,626,000 na wadau muhimu wa wizara wagharamie 90,000,000".
Barua hiyo haifafanui kuhusu wenyeviti, makatibu, wajumbe na sekretarieti ambao wanapaswa kulipwa posho hizo.
Kwa malezo haya pekee kuna maswali yanajitokeza na muhimu zaidi kuyafuatilia.
1. Posho zimepanda mara tatu zaidi ya posho za awali (AWALI)! - Hivyo posho hizi zilikuwepo na kiwango kimeelezwa Je, ni nani aliyepanga posho hizi na kwa kutumia kifungu gani cha sheria?..Bunge na wajumbe wake walitegemea hizi posho zitatoka kifungu gani cha matumizi haya toka wizara hizi..
2. Wanaolipwa ni Wenyeviti, makatibu, wajumbe na sekretariet... Hawa ni kina nani? kwani yaonyesha wazi utamaduni huu haukuanza jana wapo wenyeviti, makatibu , wajumbe na sekretariet waliokuwa wakipokea POSHO hizi kwa kiwango cha zamani cha Tsh 60,000, 50,000 na 30,000.