Kumbe inawezekana kuendesha nchi bila baraza la mawaziri!

kinjumbi one

JF-Expert Member
May 27, 2015
1,694
2,132
Kumbe inawezekana kuendesha nchi bila Baraza la mawaziri. Ni kitambo sasa tangia professor Muhongo kutumbuliwa kama waziri wa nishati na madini, lakini mambo yanaenda sawia kabisa na hata usumbufu wa kukatika kwa umeme mara kwa mara, kumepungua mno.

Lakini pia wakuu wa mikoa ya Dar es salam na Arusha, wameonyesha wakuu wa mikoa wanaweza ku cover kazi za mawaziri.

Kwa mfano daresalam chochote utakacho fanya hata kama wewe ni waziri, kama hujaenda sawa na RC, haitafaanikiwa, mfano mmoja wapo ni Lukuvi na suala la hekali 1500 za huko Kigamboni. Kumbe tunaweza kuwa na serekali bila mawaziri. Makatibu wakuu na wakuu wa mikoa wanatosha.
 
Naona chapisho lako linahang, embu malizia mkuu.

Labda unataka mawaziri wajihudhuru wote au kama wanaipenda sana kaz basi wafanye kwa kujitolea maana mchango wao hauna tija sana kwa taifa, au wawe washauri tu wa kitengo husika kama ni wabobezi katika nyanja hizo.

Neno wizara lisiwepo badara yake ziwe idara tu, maana zikibaki kuwa wizara basi waziri hakwepeki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna duplication kubwa sana kwenye vyeo vya nchi hii mfano kila Halmashauri ya Wilaya ina (1) Mkuu wa Wilaya (2) Mwenyekiti / Meya wa halmashauri na (3) Mkurungenzi wa halmashauri.....hawa wote wanalishwa na kodi zetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…