Kumbe hii KATIBA ya Tanganyika ipo kimtego

Kumbe hii KATIBA ya Tanganyika ipo kimtego

Lituye

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
1,864
Reaction score
5,697
Siwasikii tena wazanzibari mkilalamikia kuwa serikali ya Tanganyika imejivika koti la Muungano na Yale makero ya Muungano siku hizi kimyaa nini kimewasibu Wazanzibari? Au ndio utamaduni wa kiafrika unao zuia kuongea mkiwa mnakula au kulamba Asali?

Heee naambiwa Sasa hivi Wazanzibari mnateuliwa Tanganyika hadi kuwa ma DC na vyeo vingine kede kede ambayo haviko ktk wizara za Muungano. Huku sio kulamba Asali tena naona wenzetu mmeamua kutumbukia ktk mzinga wenyewe ktk shamba la bibi na kuoga Asali na kujipakaza mwilini.

Sasa hivi watanzania hususani CCM wanaumia kimoyo moyo sio tuu ktk teuzi zinazo onekana kupendelea upande wa Zanzibar pia hawamtaki hata Samia mwenyewe lakini hawawezi kusema wanaumia kimoyo moyo.

Sisi wengine hatuumii kwa kuona nani kateuliwa nani kaachwa ila tunaumia kwa kuona taifa linachezewa na kukosa misingi imara. KATIBA inayo toa mwanya wa mtu mmoja tuu kuamua na kufanya Jambo lolote linalo weza kuleta furaha au madhara kwa wote ni ya hatari na kuogopwa.

KATIBA mpya ni Sasa asie jua umuhimu wa KATIBA mpya aelimishwe.
Maendeleo hayana Vyamaa.
 
Back
Top Bottom