Kumbe Hata Wakristo Wana Mahakama Zao?

Kumbe Hata Wakristo Wana Mahakama Zao?

Buchanan

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2009
Posts
13,192
Reaction score
1,976
Wakuu,
Kumbe hata Wakristo wana Mahakama zao, Serikali ifike mahali itungie Sheria Mahakama za Kanisa ili zitambuliwe kisheria na kama ikiwezekana Kikatiba! Naomba kutoa hoja!

10653647_884656378222843_2855008467810999438_n.jpg
 
Ndiyo makanisa yana mahakama zao lakini hazijadiliwi na bunge. Ndiyo maana tunasema hizo za kadhi zisijadiliwe bungeni. Kama mtu haridhiki na maamuzi ya mahakama anaweza kukata rufaa serikalini lakini kama kanisa limeamua kumfukuza kanisani serikali haiwezi kumrejesha.
 
Wanayo lakini siyo ya kupeleka bungeni ipitishwe na bunge km mahakama ya kadhi.
 
Ni mhimu hizi mahakama ziendeshwe na waumini wenyewe kama ni waislmu waendeshe wenyewe kama ni wakristo hali kadhalika nao waendeshe mahakama zao serikali nayo iendelee na mahakama zake
 
After all hakuna aya yoyote ndani ya Qur'an inayosema kuwa Mahakama za Kadhi LAZIMA zianzishwe na kuendeshwa na Serikali!!

Kama ilivyo kuua viatu unapoingia msikitini. Hakuna aya inayosema lazima uvue viatu.

Vitu vingine vinalazimishwa ila havina backup kwenye qurani.
 
Mfumo wa mahakama uliopo sasa hivi ni wa kikiristo, kwa zaidi ya asilimia 90. Na huu uliachwa na wakolon waingereza ambao walikuwa wakiristo. Kwa maana hiyo basi sheria za nchi ni za kikiristo
 
Wakuu,
Kumbe hata Wakristo wana Mahakama zao, Serikali ifike mahali itungie Sheria Mahakama za Kanisa ili zitambuliwe kisheria na kama ikiwezekana Kikatiba! Naomba kutoa hoja!


10653647_884656378222843_2855008467810999438_n.jpg

Ni kweli, hasa waroma. Hukumu zipo na katiba mpya ya jamhuri ya muungano wa Tz inatambua
 
Yesu alisema ya Mungu mpe Mungu na Kaizari mpe Kaizari, hivyo kama wakristo wana mahakama basi wameiga mambo ya dunia
 
Lengo la baadhi ya viongozi maslahi wa dini ya kiislam wanataka kuiendesha mahakama ya kadhi kibiashara zaidi ya ibada.
 
suala ni kwamba watu wanataka ajira ili walipwe na serikali kwa mambo yao ya kidini.

hiyo mahakama ya dhulma sijui nani ataitaka maama ukipiga sensa ya wanawake wa hiyo dini wanaoitaka hiyo mahakama sidhani kama wapo.
kwenye sheria zao wao hawahesabiki hivyo hakuna watakachokuwa wanaambulia
 
Serikali yetu haina dini ...vipi leo kodi za wasiohusika zitumike kuendesha mahakama ambayo haipo kwa ajili ya kuwasaidia?
 
Mahakama zipo na hatukuwahi kuandamana au kuweka kambi bungeni kushinikiza miswada.

Its just a "gentleman's agreement"
 
Migogoro ya ndoa za kikristo huwa inashughulikiwa kikanisa ngazi kwa ngazi...

Hadi inapofika ngazi ya mahakama za kiserikali ni kwamba kanisa limwshindwa kutatua katika taratibu zake...
 
Mfumo wa mahakama uliopo sasa hivi ni wa kikiristo, kwa zaidi ya asilimia 90. Na huu uliachwa na wakolon waingereza ambao walikuwa wakiristo. Kwa maana hiyo basi sheria za nchi ni za kikiristo

Kuna sehem mshtakiwa anatakiwa akatubu kwa padre/kasisi au mchungaji ili afutiwe mashtaka yake ??... kuna ukanisa gani hapo kwenye mahakama ?.. au mnafata mkumbo tu bila kutafakari. Toa ushahid wa uyasemayo ?
 
Makanisa yana utaratibu wake wa kushughulikia mambo mbalimbali yahusuyo maisha ya waumini wao. Kuna mabaraza ya usuluishi na mahakama za kanisa ngazi kwa ngazi.

Kuna mafundisho ya watoto ngazi mbalimbali n.k. Yote haya yanaendeshwa kwa utaratibu waliojipangia wenyewe na kwa fedha za kanisa lenyewe. Sio fedha za serikali.
 
Back
Top Bottom