Kumbe hata Ulaya marefa nao ni magumashi

Kumbe hata Ulaya marefa nao ni magumashi

Niwemugizi

JF-Expert Member
Joined
Oct 15, 2012
Posts
902
Reaction score
462
Baada ya kupata ushauri mbalimbali kutoka kwa wana JF hatimaye tumeambatana na mama kwenda kwenye mpira leo.Tumeanza na gemu la Liverpool na Everton kwa kuwa sehemu nayoangalizia ni full makelele kipindi cha kwanza kilipoisha tu akaamua kuondoka zake akasema mpira ukiisha nirudi nyumbani.Lakini wapi sikurudi wala nini imebidi niunganishe na wa Chelsea na Man United. Kusema ukweli huyu refari wa gemu la Man na Chelsea kaharibu mpira sana haiwezekani kuwapa wachezaji wawili kadi nyekundu.Kiuwazi Man wamebebwa na kila siku wao ni kubebwa tuuuuuuuu na kwa mwendo huu Man U hawafiki mbali kwenye Champions league maana kule hakuna mambo ya FA na marefari wa England.Mi nilidhani tu Man huwa wanabebwa na Howard Web kumbe ni makakati wa FA nzima
 
Wajiulize mashabiki wa Man U, iweje wawe mabingwa mara kadhaa zaidi ya Barcelona walivyo mabingwa wa Spain lakini wasiwe mabingwa Europe zaidi ya ubingwa wa Europe?
 
Sikatai ni kweli mpira unaendana pia na bahati na ufindi, lakini kwa Manchester mpira wao unaendana na rafari atakaechezesha mechi yao.Correct me if I am wrong but that ie my story and I will stick on it.Manchester manabebwa sana lakini muda ni mwalimu mzuri ipo siku timu zingine zitalivalia njuga suala hili maana mmezidi sana
 
Sikatai ni kweli mpira unaendana pia na bahati na ufindi, lakini kwa Manchester mpira wao unaendana na rafari atakaechezesha mechi yao.Correct me if I am wrong but that ie my story and I will stick on it.Manchester manabebwa sana lakini muda ni mwalimu mzuri ipo siku timu zingine zitalivalia njuga suala hili maana mmezidi sana

mkuu mwisho wa Man U ni kustaafu kwa huyu babu. Hawana lolo washenzi hawa.
 
Mark Clattenburg kanikera sana leo! pamoja na kwamba sikushabikia timu yoyote leo ila kaharibu game pambafu yule! Chelsea ilibidi waondoke na point 3 leo! unlucky sons!!
 
Mark Clattenburg kanikera sana leo! pamoja na kwamba sikushabikia timu yoyote leo ila kaharibu game pambafu yule! Chelsea ilibidi waondoke na point 3 leo! unlucky sons!!
Nami ingawa timu yangu ya Liver inapumlia gesi kusema ukweli Man U wamebebwa na refa kaharibu kabisa radha ya gemu.Ilitakiwa Man wapigwe kipigo cha mwizi
 
Uyu refa ingekuwa ndo game inapigwa pale uwanja wa Tandika mabatini asingetoka hai na wala game lisingeisha salama
 
Hivi Man u ni kitu gani hiki! Wanabebwa lika siku! Mechi ya leo was a disgrace haiwezekani waamzi wote na kamisa wao washindwe kuona makosa ya wazi kiasi hicho
Hapa ndipo huwa nawashangaa mashabiki. Wenzenu (hao marefa na wachezaji) mpira ni profession yao, wamesomea na wakafuzu. Leo hii, wewe unayejifanya unajua mpira, mara refarii kakosea, mara makosa ya wazi yaliachwa, hukuwahi kucheza hata mpira wa soksi kwenye uwanja wa vumbi! Bado soka letu kama Taifa linapumulia mashine lakini wanazi wa mpira ukiwasikiliza utadhani walishawahi kuchezea Spain! Tofautisheni ushabiki na utaalamu, maneno matupu na vitendo. Wewe unayelalamika tukikupa timu ya Simba mwakani uifundishe itashika hata nafasi ya 3 kweli? Acheni kuota ndoto za Abunuasi!
 
Mashabik wao wanaona aibu..! Wameshnda lakin siwaon huku mtaan..! Kaz Kwao F.A kuokoa soka la England hasa mech za Man U.
 
Man U, wamebebwa na mbeleko ya chuma...

Rafu wacheze wao, kadi apewe Torres... Ingekuwa Bongo yule refa wangemroga, sitanii. Cheza na akina Akilimali na Bamchawi (RIP) nini?
 
BARCELONA ANABEBWA LAKINI ANA SWAGGA ZA KUKUTIA PRESHA MPINZANI HADI MOYONI UNAKUBALI MPIRA WANAUJUA

LAKINI MAN UTD WANABEBWA HATA KAMA HAWANA SWAGGA ZA KUSHAMBULIA KAMA BARCA as MAN UTD BILA MAREFA HAKUNA KITU..

Inshort MAN UTD na BARCA WANABEBWA SANA
 
Tatizo la wabongo ni vilaza....,mpira una sheria na kanuni za kufuata,unataka uvunje kanuni uachwe, pili marefa ni watu kama watu wengine tu kuna makosa mengine ya kibinadamu ....viva Man U viva refaree kwa kufuata za soka..
 
Back
Top Bottom