Kumbe Georgina ni Kisa cha kweli!

Kumbe Georgina ni Kisa cha kweli!

Wildlifer

JF-Expert Member
Joined
May 12, 2021
Posts
1,883
Reaction score
5,270
Ninasikiliza Kipindi cha 'zilipendwa', basi nimesikia Mkasa ulio nyuma ya wimbo wa Georgina wake Marijan Rajab.
marijani-rajabu-1.jpg




Wimbo huu ni mkasa wa kweli. Mapenzi shuleni.

Marijan yaelezwa alikuwa akisoma Tambaza na rafikiye mmoja. Huyo Rafiye alikuwa na uhusiano na binti aitwaye Georgina Mahiga; Mtoto wa kaka yake Marehemu Balozi Augustine Mahiga. Binti huyo alikuwa ni mwanafunzi wa kidato cha Pili pale Azania Secondary school. Bahati mbaya akapata ujauzito. Kuepusha dhahma, wazazi wa Georgina walimtoa Azania na kumpeleka Iringa.

Rafikiye Marijan hakuwa anajua kuwa Mwanamke wake ameondoshwa Dar. Alikuwa akimtafuta pasi na kujua amekwenda wapi. Aliteseka na kuondoka kwake.

Katika hangaiko lile, ndipo Marijani akapata fursa ya Kutunga wimbo huo miaka ya 1970.

Kilichofuata ni wimbo ambao umeishi hadi leo. Masherehe mengi wimbo huu huwa haukosi.

FM Academia waliufanyia live performance wimbo huu.


Source: [emoji343] Kahama FM
 
Kwa kweli unaweza changanyikiwa. Na hii inaweza kutesa maisha yako yote. Hata ukipata mwanamke mwingine, a bado akili zako zitakuwa kwake.
upo sahihi,huwa na imagine wanaofiwa inakuje kama akiondok tu inauma vile je akifa, kuna jamaa juzi amenisimulia alipata mpenzi mzuri na mwenye pesa lakini walidumu kama mwezi tu yule binti akafa kwa kuuwawa,
jamaa alianza kuishi nae kabisa na wakapanga ndoa
 
upo sahihi,huwa na imagine wanaofiwa inakuje kama akiondok tu inauma vile je akifa, kuna jamaa juzi amenisimulia alipata mpenzi mzuri na mwenye pesa lakini walidumu kama mwezi tu yule binti akafa kwa kuuwawa,
jamaa alianza kuishi nae kabisa na wakapanga ndoa
Ndio maana wapo wanaume ambao hawachukui muda mrefu nao hufariki pindi wafiwapo na wake zao hasa ambao umri umekwisha kwenda.
 
Ila manamke hata ukifa linadunda hata miaka 100 aisee
Si kwa sababu wana roho ngumu, sababu ni utofauti wa Umri. Wanaume huoa wanawake ambao tumewazidi umri, na mfumo wa maisha it's more likely kwa sisi wanaume kufa mapema kuliko wanawake. Na pili sisi wanaume tunakuwa tunahudumiwa na wanawake kwenye mambo ya nyumbani, kumbuka over 65, hata watoto washaondoka home, so mke akifa mwanaume ule upweke humfanya afe mapema.
 
Si kwa sababu wana roho ngumu, sababu ni utofauti wa Umri. Wanaume huoa wanawake ambao tumewazidi umri, na mfumo wa maisha it's more likely kwa sisi wanaume kufa mapema kuliko wanawake. Na pili sisi wanaume tunakuwa tunahudumiwa na wanawake kwenye mambo ya nyumbani, kumbuka over 65, hata watoto washaondoka home, so mke akifa mwanaume ule upweke humfanya afe mapema.
Hawa waga wana move on faster mkuu age doesn't matter hapo swala ni upendo
 
Nitarudi nami kuelezea ya kwangu

Ila yote na yote usiombe ufungwe umuache mkeo ulaiani

Ni mara 1000 kabla ya hukumu umuombe kuudhi na akuache upate sababu ya kumlaumu ukiwa gerezani
 
upo sahihi,huwa na imagine wanaofiwa inakuje kama akiondok tu inauma vile je akifa, kuna jamaa juzi amenisimulia alipata mpenzi mzuri na mwenye pesa lakini walidumu kama mwezi tu yule binti akafa kwa kuuwawa,
jamaa alianza kuishi nae kabisa na wakapanga ndoa
Kufiwa kuna nafuu maana utapata hata Faraja kua ni kazi ya Mungu haina Makosa. Lakini kumkosa ni maumivu makubwa kwani utatengeneze imagination nyingi zingine negative na kuongeza maumivu zaidi.
 
Tatizo lenu mnarogwa sana!!! halafu mnalialia hovyo! km majinga!! ukitaka kujua hili Lamba chooni kama utamkumbuka mtu hapa!
 
Huyo Jojina kwa sasa najua atakuwa mbibi sasa!! .......mtoto wa mkaka wake Maiga??........Duuu!! ebu weka kapicha tumuone?? au tukamtembelee kabisa unajua hiyo ni habari na ina hela!!.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom