Kumbe CCM waliibiana kura uchaguzi EAC!!!!!

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500
Kweli mjasiri haachi asili. Nimeipata hii habari kwenye gazeti la Mtanzania. CCM hata wenyewe kwa wenyewe wameibiana kura duh!!!!!

CCM waibiana kura


Imeandikwa na Maregesi Paul, Dar es Salaam: Thursday, April 05, 2012 09:44

UCHAGUZI wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeingia doa. Chanzo chetu cha habari kilichokuwa katika uchaguzi huo, kilisema jana kuwa, uchaguzi huo uliofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam, ulijaa kasoro kwa baadhi ya wagombea kuibiwa kura.

Chanzo hicho kilisema kuwa, mmoja wa wanaodaiwa kuhujumu kura hizo ni aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi huo, ambaye pia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. Nape alikuwa akisaidiana na kada wa chama hicho, Abdulrahman Kinana.

Chanzo hicho kilisema kuwa, dalili za kuwapo hujuma katika uchaguzi huo, zilianza baada ya wabunge kukataa kura kuhesabiwa chini ya usimamizi wa meza kuu iliyokuwa ikiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

“Mimi nilikuwapo ukumbini na niliingia kama mmoja wa mawakala waliokuwa katika chumba cha kuhesabia kura, kwani nilikwenda kumsimamia jamaa yangu ambaye alikuwa anagombea.

“Kwanza kabisa kabla ya kuingia katika chumba cha kuhesabia kura, kura zilipigwa kama kawaida, zoezi hilo lilipokamilika, ukafika wakati wa kwenda kuhesabu kura.

“Kabla ya hapo, Kinana alisimama na kutueleza kwamba, kura za wagombea zitasimamiwa na meza kuu, aliposema hivyo, wabunge wakalipuka kwa kusema hatutaki na wengine walidiriki hata kuzomea.
 
Unashangaa CCM kuibiana kura? Ni sawa na kushangaa kumuona simba serengeti.
 
Kweli mjasiri haachi asili. Nimeipata hii habari kwenye gazeti la Mtanzania. CCM hata wenyewe kwa wenyewe wameibiana kura duh!!!!!

CCM waibiana kura


Imeandikwa na Maregesi Paul, Dar es Salaam: Thursday, April 05, 2012 09:44

UCHAGUZI wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki kwa upande wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), umeingia doa. Chanzo chetu cha habari kilichokuwa katika uchaguzi huo, kilisema jana kuwa, uchaguzi huo uliofanyika juzi kwenye Ukumbi wa Karimjee, Dar es Salaam, ulijaa kasoro kwa baadhi ya wagombea kuibiwa kura.

Chanzo hicho kilisema kuwa, mmoja wa wanaodaiwa kuhujumu kura hizo ni aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi huo, ambaye pia ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. Nape alikuwa akisaidiana na kada wa chama hicho, Abdulrahman Kinana.

Chanzo hicho kilisema kuwa, dalili za kuwapo hujuma katika uchaguzi huo, zilianza baada ya wabunge kukataa kura kuhesabiwa chini ya usimamizi wa meza kuu iliyokuwa ikiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

“Mimi nilikuwapo ukumbini na niliingia kama mmoja wa mawakala waliokuwa katika chumba cha kuhesabia kura, kwani nilikwenda kumsimamia jamaa yangu ambaye alikuwa anagombea.

“Kwanza kabisa kabla ya kuingia katika chumba cha kuhesabia kura, kura zilipigwa kama kawaida, zoezi hilo lilipokamilika, ukafika wakati wa kwenda kuhesabu kura.

“Kabla ya hapo, Kinana alisimama na kutueleza kwamba, kura za wagombea zitasimamiwa na meza kuu, aliposema hivyo, wabunge wakalipuka kwa kusema hatutaki na wengine walidiriki hata kuzomea.

HUJATWAMBIA WALIIBIANAJE! Mkuu hebu kuwa specific, nani kwamwibia nani na nani kaibiwa na nani? hit the point please!
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom