lutemi
JF-Expert Member
- Dec 24, 2013
- 1,744
- 1,379
Wadau nimesoma kitabu cha Mungu (BIBLIA) nimegundua kwamba utoaji mahari kwa ajili ya kuoa halipo katika maandiko matakatifu.
Bali nimeona kwamba zamani mtu anayetaka kuoa alipeleka zawadi anayoona yeye inafaa.
Mahari ni adhabu na hii ilitokea kwa mtoto wa Yakobo aliyeitwa Dina baada ya kubakwa na kubikiriwa na wafilisti na ilikuwa chukizo sana kwa kaka zake Dina na wakaamua kuwatoza wafilisti walete nyama za magovi yao yaani watahiriwe na walipofanya hivyo wakauawa.
Kwa hiyo mahari ni upagani. Mahari ni unyanyasaji. Mahari kwa wacha Mungu ni kushusha thamani (value) ya binti yako kwamba yeye analingana na kiasi hicho kilichotolewa.
Mahari inafanya vijana wengi wakimbilie makahaba wakawaacha mabinti. Mahari inavunja mmomonyoko wa maadili.
Nimeona hata waislamu hawatozi mahari. Naomba serikali ifute mahari.
Karibu wadau mchangie.
Bali nimeona kwamba zamani mtu anayetaka kuoa alipeleka zawadi anayoona yeye inafaa.
Mahari ni adhabu na hii ilitokea kwa mtoto wa Yakobo aliyeitwa Dina baada ya kubakwa na kubikiriwa na wafilisti na ilikuwa chukizo sana kwa kaka zake Dina na wakaamua kuwatoza wafilisti walete nyama za magovi yao yaani watahiriwe na walipofanya hivyo wakauawa.
Kwa hiyo mahari ni upagani. Mahari ni unyanyasaji. Mahari kwa wacha Mungu ni kushusha thamani (value) ya binti yako kwamba yeye analingana na kiasi hicho kilichotolewa.
Mahari inafanya vijana wengi wakimbilie makahaba wakawaacha mabinti. Mahari inavunja mmomonyoko wa maadili.
Nimeona hata waislamu hawatozi mahari. Naomba serikali ifute mahari.
Karibu wadau mchangie.