Kariakoo, Dar: Wafanyabiashara wadogo wanatozwa kati ya elfu 50 hadi laki 3 kama adhabu

Kindeena

JF-Expert Member
Sep 27, 2017
9,031
15,736
Baadhi ya viongozi wa Wafanyabiashara wadogo katika Soko la Kariakoo, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na askari wa Jiji wanadaiwa kuwatesa na kuwanyanyasa Wafanyabiashara wadogo, na kuwatoza Wafanyabiashara hao faini kubwa kati ya Tshs 50,000/= hadi 300,000/= kama adhabu ya "makosa" mbalimbali na hawatoi risiti.

Mfano leo Jumamosi, 26/03/2022, baadhi ya Wafanyabiashara wadogo walikamatwa na mizigo yao kuchukuliwa kisha kupelekwa ofisini kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kufungua biashara wakati Mkuu wa Wilaya ya Ilala anafanya usafi. Kwa hiyo wao pia walipaswa kwenda kufanya usafi na siyo kufungua biashara.

Katika kujitetea, Wafanyabiashara wadogo hao wameamriwa kulipa laki 3 ili warudishiwe mizigo yao, na wakikaidi watapelekwa Mahakama ya Jiji.

Mmoja ya Wafanyabiashara hao kanieleza kwamba waliwaomba wapunguziwe ndipo wakaafikiana kwamba walipe elfu 50 (cash mkononi) kila mmoja na wasipolipa watakiona.

Inaelezwa kwamba, ofisini hapo kuna namba ya akaunti kwa ajili ya kwenda kulipia adhabu, lakini viongozi wanapokelea pesa mikononi na hawatoi risiti wala maandishi yeyote.

Mmoja ya viongozi hao, alisikika akimwambia mfanyabiashara mmoja kwamba hiyo pesa ya adhabu asiitoe hadharani kwa sababu ukutani kuna namba maalumu ya kulipia kwa hiyo asije akawaingiza matatizoni kwa kupokea fedha kinyume na utaratibu uliowekwa na Serikali.

Nimedokezwa kwamba hata mfanyabiashara akikomaa kwamba apelekwe mahakamani, hapelekwi na badala yake wanashikilia tu mizigo yake na au kuzunguka naye kwenye gari ili aingie hofu na alipe fedha ambazo wanakula hao viongozi.

Taarifa zinasema kwamba kuna sehemu Wafanyabiashara wataotuhumiwa hupelekwa na hiyo sehemu panaitwa "depo"; yaani ni kama mahabusu fulani hivi ya kuwatesea wakosaji.

Hata kama ni kushughulikiwa, sheria ifyatwe. Iweje mtu afanye kosa halafu bidhaa zinashikiliwa, anatozwa hela kubwa na hapewi risiti???

Kwanza hakuna uwiano kati ya kutenda kosa na kisha mgambo kuchukua bidhaa za wamachinga. Huo ni uhuni na ni unyang'anyi.

Machinga walipagwa na Serikali kwa agizo la rais, sasa iweje wanafanyiwa ukatili?

Tafadhali sana, wadau wa serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala na maafisa wengine wa chama na Serikali fuatilieni hili ili kuweka mambo sawa na hao viongozi warudishe pesa za hao Wafanyabiashara wadogo.
 
Baadhi ya viongozi wa Wafanyabiashara wadogo katika Soko la Kariakoo, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na askari wa Jiji wanadaiwa kuwatesa na kuwanyanyasa Wafanyabiashara wadogo, na kuwatoza Wafanyabiashara hao faini kubwa kati ya Tshs 50,000/= hadi 300,000/= kama adhabu ya "makosa" mbalimbali na hawatoi risiti.

Mfano leo Jumamosi, 26/03/2022, baadhi ya Wafanyabiashara wadogo walikamatwa na mizigo yao kuchukuliwa kisha kupelekwa ofisini kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kufungua biashara wakati Mkuu wa Wilaya ya Ilala anafanya usafi. Kwa hiyo wao pia walipaswa kwenda kufanya usafi na siyo kufungua biashara.

Katika kujitetea, Wafanyabiashara wadogo hao wameamriwa kulipa laki 3 ili warudishiwe mizigo yao, na wakikaidi watapelekwa Mahakama ya Jiji.

Mmoja ya Wafanyabiashara hao kanieleza kwamba waliwaomba wapunguziwe ndipo wakaafikiana kwamba walipe elfu 50 (cash mkononi) kila mmoja na wasipolipa watakiona.

Inaelezwa kwamba, ofisini hapo kuna namba ya akaunti kwa ajili ya kwenda kulipia adhabu, lakini viongozi wanapokelea pesa mikononi na hawatoi risiti wala maandishi yeyote.

Mmoja ya viongozi hao, alisikika akimwambia mfanyabiashara mmoja kwamba hiyo pesa ya adhabu asiitoe hadharani kwa sababu ukutani kuna namba maalumu ya kulipia kwa hiyo asije akawaingiza matatizoni kwa kupokea fedha kinyume na utaratibu uliowekwa na Serikali.

Nimedokezwa kwamba hata mfanyabiashara akikomaa kwamba apelekwe mahakamani, hapelekwi na badala yake wanashikilia tu mizigo yake na au kuzunguka naye kwenye gari ili aingie hofu na alipe fedha ambazo wanakula hao viongozi.

Taarifa zinasema kwamba kuna sehemu Wafanyabiashara wataotuhumiwa hupelekwa na hiyo sehemu panaitwa "depo"; yaani ni kama mahabusu fulani hivi ya kuwatesea wakosaji.

Tafadhali sana, wadau wa serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala na maafisa wengine wa chama na Serikali fuatilieni hili ili kuweka mambo sawa na hao viongozi warudishe pesa za hao Wafanyabiashara wadogo.
Washughulikiwe kwa sababu leo ilikuwa siku ya usafi hadi saa 4 kama walizingua ulitaka wachekewe?
 
Washughulikiwe kwa sababu leo ilikuwa siku ya usafi hadi saa 4 kama walizingua ulitaka wachekewe?
Hata kama ni kushughulikiwa, sheria ifyatwe. Iweje mtu afanye kosa halafu bidhaa zinashikiliwa, anatozwa hela kubwa na hapewi risiti???

Kwanza hakuna uwiano kati ya kutenda kosa na kisha mgambo kuchukua bidhaa za wamachinga. Huo ni uhuni na ni unyang'anyi.

Machinga walipagwa na Serikali kwa agizo la rais, sasa iweje wanafanyiwa ukatili?
 
Kama issue kutotoa Risit, basi toeni hizo risiti.

Alikwambia utoe Fine, mwambie na yeye akupe risiti.

Tatizo hapa wote wafabiashara na wakusanyaji wote Janja Janja.
 
Uko sahii,watanzania tunatabia za kinafkii na kulia Lia,hiyo ilipitishwa Tanzania nzimaa jmosi ya mwisho wa mwezi Ni siku ya usafiri mpaka saa 4,kwaiyo ukikiuka mamlaka haina Budi kuchukua mkondo,pia wafanya biashara ndogo ndogo sanyingine wanadharau,mfanonl mnaambiwa msipange bidhaa barabarani we unajiona mjanjaa unapanga unategemea nini

Sent from my TECNO B1p using JamiiForums mobile app
 
Baadhi ya viongozi wa Wafanyabiashara wadogo katika Soko la Kariakoo, Dar es Salaam, kwa kushirikiana na askari wa Jiji wanadaiwa kuwatesa na kuwanyanyasa Wafanyabiashara wadogo, na kuwatoza Wafanyabiashara hao faini kubwa kati ya Tshs 50,000/= hadi 300,000/= kama adhabu ya "makosa" mbalimbali na hawatoi risiti.

Mfano leo Jumamosi, 26/03/2022, baadhi ya Wafanyabiashara wadogo walikamatwa na mizigo yao kuchukuliwa kisha kupelekwa ofisini kwa kile kilichoelezwa kwamba ni kufungua biashara wakati Mkuu wa Wilaya ya Ilala anafanya usafi. Kwa hiyo wao pia walipaswa kwenda kufanya usafi na siyo kufungua biashara.

Katika kujitetea, Wafanyabiashara wadogo hao wameamriwa kulipa laki 3 ili warudishiwe mizigo yao, na wakikaidi watapelekwa Mahakama ya Jiji.

Mmoja ya Wafanyabiashara hao kanieleza kwamba waliwaomba wapunguziwe ndipo wakaafikiana kwamba walipe elfu 50 (cash mkononi) kila mmoja na wasipolipa watakiona.

Inaelezwa kwamba, ofisini hapo kuna namba ya akaunti kwa ajili ya kwenda kulipia adhabu, lakini viongozi wanapokelea pesa mikononi na hawatoi risiti wala maandishi yeyote.

Mmoja ya viongozi hao, alisikika akimwambia mfanyabiashara mmoja kwamba hiyo pesa ya adhabu asiitoe hadharani kwa sababu ukutani kuna namba maalumu ya kulipia kwa hiyo asije akawaingiza matatizoni kwa kupokea fedha kinyume na utaratibu uliowekwa na Serikali.

Nimedokezwa kwamba hata mfanyabiashara akikomaa kwamba apelekwe mahakamani, hapelekwi na badala yake wanashikilia tu mizigo yake na au kuzunguka naye kwenye gari ili aingie hofu na alipe fedha ambazo wanakula hao viongozi.

Taarifa zinasema kwamba kuna sehemu Wafanyabiashara wataotuhumiwa hupelekwa na hiyo sehemu panaitwa "depo"; yaani ni kama mahabusu fulani hivi ya kuwatesea wakosaji.

Hata kama ni kushughulikiwa, sheria ifyatwe. Iweje mtu afanye kosa halafu bidhaa zinashikiliwa, anatozwa hela kubwa na hapewi risiti???

Kwanza hakuna uwiano kati ya kutenda kosa na kisha mgambo kuchukua bidhaa za wamachinga. Huo ni uhuni na ni unyang'anyi.

Machinga walipagwa na Serikali kwa agizo la rais, sasa iweje wanafanyiwa ukatili?

Tafadhali sana, wadau wa serikali hususani Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mkuu wa Wilaya ya Ilala na maafisa wengine wa chama na Serikali fuatilieni hili ili kuweka mambo sawa na hao viongozi warudishe pesa za hao Wafanyabiashara wadogo.
Acha wapigwe tu. Nchi ikishakuwa ya watu mabwege ndiyo inavyokuwa. Mtu mmoja anaweza kuwaamrisha watu zaidi ya milioni 3 eti siku fulani ni siku ya usafi na hakuna kufanya shughuli wakati usafi wenyewe ni maigizo tu na watu wanatii kama wako jela!
 
Acha wapigwe tu. Nchi ikishakuwa ya watu mabwege ndiyo inavyokuwa. Mtu mmoja anaweza kuwaamrisha watu zaidi ya milioni 3 eti siku fulani ni siku ya usafi na hakuna kufanya shughuli wakati usafi wenyewe ni maigizo tu na watu wanatii kama wako jela!
Aisee
 
Wabongo wengi akili zetu ni kama punda tu, bila mijeledi hatuwezi kwenda.
 
Back
Top Bottom