Mateso
JF-Expert Member
- Aug 6, 2008
- 259
- 19
Wakuu nimepitia andiko takatifu na kukuta kumbe kila kiongozi anatoka kwa Mungu kwa hivyo aheshimiwe na kupendwa. Warumi 13: 1. Unasema 'Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu, kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu na ile ilyopo imeamriwa na Mungu.' mstari 6-7 inasema ' Kwa sababu hiyo tena muwalipe kodi kwa kuwa wao ni wahudumu wa Mungu, wakidumu katika kazi hiyo hiyo. Wapeni wote haki zao; mtu wa kodi kodi; mtu wa ushuru, ushuru; astahili hofu, hofu; astahili heshima, heshima.' Sasa msimamo wetu kwa hali ya sasa hivi ni upi kwa uongozi huu.