Kulima nilime mimi, shida nipate mimi, halafu mteja unichagulie?

Kulima nilime mimi, shida nipate mimi, halafu mteja unichagulie?

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
Joined
May 14, 2010
Posts
2,182
Reaction score
309
Wakulima wa Tanzania ni miongoni mwa watu wenye dhiki na shida zisizomithilika.

Kodi wanalipa lakini serikali yao haiwapatii huduma za jamii-shule wanazosoma watoto wao ni vichekesho vitupu, miondombinu (barabara, mawasiliano, etc) ni kejeri kubwa, mbwa wa watawala wanapatiwa huduma za afya zilizo bora kuliko wanazopata zaidi ya asilimia 80 ya wapiga kura (wakulima).

Lakini kejeri kubwa kuliko zote ni kuwazuia wakulima kuuza mazao yao nje ya maeneo fulani wanayotaka watwawala, kuwalazimisha wauze mavuno yao kwa wateja inaowataka serikali!

Kwanza huku ni kukiuka haki ya msingi kabisa ya uhuru wa kuchagua lakini pia ni kuhakikisha kuwa wakulima wanaendelea kuwa masikini kwani.

Ninapoandika kuna zuio la kuuza mchele wa Tanzania nje ya nchi, mwaka jana ulikuwa mwaka wa mavuno mazuri na wakulima wengi walitarajia kuwa wangenufaika na jasho lao lakini watawala wetu wamepiga marufuku mchele wetu kuvuka mipaka ambako ungewezesha wakulima wa TZ kupata bei nzuri (tunasikia waligombana na marais wa nchi jirani hivyo kuwakomoa ni kuzuia mchele, ambao wanautegemea utoke TZ).

Kwa nini wenye viwanda wanahamasishwa kuuza bidhaa zao nje ya nchi? Au wakulima wetu ni second class citizens (daraja la chini, aka watawaliwa)?
 
Mods kwa nini mmehamisha hoja hii? Au mpaka kuwe na neno siasa ndo iwe mada ya siasa?
Pathetic!
 
Najua tunaongozwa na biashara huria, je mazao nayo yaamo kwenye hilo?
 
Huku siasa ni chadema na ccm,mbowe,slaa na zito kabwe
 
Hii ndiyo Tanzania, mkulima hana chake!. Lakini huenda serikali inafanya hivyo ili kudhibiti mfumuko wa bei za vyakula nchini.
 
kwenye hili suala ndiyo huwa nachoka kabisaaa. Mbaya zaidi mtu unakuta katumia nguvu zake kulima na kodi analipa. Huu ni uhuni tu!!
 
Kweli ni majanga! shamba ulime wewe,mbolea ununue wewe,kuvuna upigike wewe, bei upangiwe na kuuza wakupangie wao!
 
Hii ndiyo Tanzania, mkulima hana chake!. Lakini huenda serikali inafanya hivyo ili kudhibiti mfumuko wa bei za vyakula nchini.

Mkuu, ina maana wakulima ndio wana wajibu wa kuhakikisha bei hazipandi? Huu ni uhuni kwani hilo siyo jukumu lao, ni jukumu la serikali na ndiyo maana serikali inakusanya kodi kuhakikisha kuwa nchi inaendeshwa lakini wanayofanya kwa kuzuia uuzwaji wa mazao nje ya nchi ni uhuni na kwa sababu wakulima hawana umoja kwani wakipinga hakuna mkuu wa mkoa, wilaya au waziri anayeweza kusimama mahakamani kupambana nao.
 
Mkuu, ina maana wakulima ndio wana wajibu wa kuhakikisha bei hazipandi? Huu ni uhuni kwani hilo siyo jukumu lao, ni jukumu la serikali na ndiyo maana serikali inakusanya kodi kuhakikisha kuwa nchi inaendeshwa lakini wanayofanya kwa kuzuia uuzwaji wa mazao nje ya nchi ni uhuni na kwa sababu wakulima hawana umoja kwani wakipinga hakuna mkuu wa mkoa, wilaya au waziri anayeweza kusimama mahakamani kupambana nao.

Dawa ni sisi wanajamii tuwatafutie masoko nje hawa wenzetu wakulima na wauze mazao yao pasipo kuishirikisha serikali maana kwa sasa tupo kwenye mfumo wa soko huria.
 
Dawa ni sisi wanajamii tuwatafutie masoko nje hawa wenzetu wakulima na wauze mazao yao pasipo kuishirikisha serikali maana kwa sasa tupo kwenye mfumo wa soko huria.

Mkuu,

Tatizo ni kuwa serikali imepiga marufuku uuzwaji wa mchele nje ya nchi, kwa maana nyingine ni kosa la jinai (wakuu wa mikoa nadhani ndio hutoa amri hizi) kwa mtanzania yeyote kuuza mchele nje ya nchi. Hii ina maana kuwa kama Rusumo kilo moja inauzwa TZS2,000 na Kahama mjini kilo hiyo hiyo inauzwa 1,000 mkulima wa Kahama/Tanzania haruhusiwi kunufaika na soko la Rusumo, hata kama anaweza kupeleka mchele wake kwa faida serikali yake imekifanya kitendo cha kufaidika na nguvu zake kuwa haramu!
 
Najua tunaongozwa na biashara huria, je mazao nayo yaamo kwenye hilo?

Mkuu,

Kwa mtizamo wangu hayamo, halafu wanasiasa wetu wakipanda majukwaani wanasema "KILIMO KWANZA"

Itakuwaje kilimo kwanza kama kilimo hakilipi?
 
Back
Top Bottom