Kulikoni mnafanya Msiba kama sherehe za kawaida?

Kulikoni mnafanya Msiba kama sherehe za kawaida?

Mandla Jr.

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2013
Posts
3,098
Reaction score
631
Wanabodi habari ya leo,

Binafsi naomba kusema ni vyema kuwajali na kuwahifadhi wapendwa wetu waliotutoka kwa njia nzuri na ambazo ziko kihalali kulingana na mila, desturi, tamaduni na dini tunazoziamini. Lakini pia niseme ni masikitiko sana kuondokewa na mtu katika jamii yetu na kaya zetu, lakini hayo huwa ni mapenzi ya Mwenyenzi Mungu kikubwa ni kuwaombea wapumzike kwa amani waliko tangulia.

Sasa, naomba nishangae mambo yanayoendelea kwa wenzetu Wachaga, kwakweli misiba yao ni sherehe kubwa, majigambo, ufahari mkubwa hakika hii sidhani kama ni jambo zuri hasa kwa wale ambao wanakuwa wamempoteza ndugu yao.

Misiba inakuwa mpaka na Pombe na vinywaji vingine vikali? Ufahari wa magari ya bei kubwa? Yote haya ni kwa faida ya nani? Mfano ukikaa barabara ya Arusha - Moshi utastaajabu utitiri wa magari ya kifahari kwenda kwenye msiba Moshi, hivi hili linawasaidia kweli wafiwa?

Utakuta mtu anatoka msibani analalamika, hoo mimi sikupata bia au hoo mimi sijala nikashiba. Kweli kweli ndugu zangu mmefikia huku....Hakika inaumiza sana.

Nimeyaona ndio maana nimesema, nisichukiwe kwa kusema ukweli!!

SIO JAMBO JEMA AU LENYE AFYA.

Mandla.
 
Nimeyaona ndio maana nimesema, nisichukiwe kwa kusema ukweli!!
 
Pole kwa kukosa akili na uwezo wa kutafuta pesa.kumbuka kwamba mara mtoto anapozaliwa hufanyiwa sherehe kukaribishwa duniani kwenye shida na raha,vivyo hivyo anapokufa huagwa kwenda kwenye shida na raha.wachaga wanatimiza matakwa ya muumba wao alowajalia uwezo,

Kwanza kiakili
Na pili kifedha
 
Mkuu umenifurahisha sana, kwa hito huwa unashinda barabarani siku nzima kuangalia magari ya kifahari unayosema ni ya wachagga yakitoka Arusha kwenda Moshi??


Njoo nikupe kibarua unilimie bustani yangu Maili sita nitakulipa chochote kuliko kazi unayoifanya na umri unaenda mwisho wa siku tunakuona unachomwa moto kwa wizi mtaani kama Sigara.
 
:smile-big::smile-big: ni karibu misiba mingi ya sasa ivo citu vipo tena mpaka vyakula vinakuwa vya thaman kubwa sana
 
Naona kama unawasikitikia wakati waandaaji ndo wafiwa wenyewe, Kwa uwezo wao wafiwa wanaandaa sherehe, misafara ya magari yao wenywe, wanakula na kunywa wenyewe, wewe mpita njia inakuuma nini?
''poor boy in rich family wewe" acha watu wale bata.Mijitu mingine bwana???
 
Magari ya kifahari wananunua cku ya huo msiba au wanakuwa nayo kabla ya mcba au baada ya mcba? kama huna jibu ni wivu
 
Ukabila na udini ni magonjwa yanayokua kwa kasi JF
 
Pole kwa kukosa akili na uwezo wa kutafuta pesa.kumbuka kwamba mara mtoto anapozaliwa hufanyiwa sherehe kukaribishwa duniani kwenye shida na raha,vivyo hivyo anapokufa huagwa kwenda kwenye shida na raha.wachaga wanatimiza matakwa ya muumba wao alowajalia uwezo,

Kwanza kiakili
Na pili kifedha

Natumia elimu yangu kutafuta pesa, hivyo mimi ni mwajiriwa Serikalini. Hivyo hiyo pole yako baki nayo tuu.
 
Mkuu umenifurahisha sana, kwa hito huwa unashinda barabarani siku nzima kuangalia magari ya kifahari unayosema ni ya wachagga yakitoka Arusha kwenda Moshi??


Njoo nikupe kibarua unilimie bustani yangu Maili sita nitakulipa chochote kuliko kazi unayoifanya na umri unaenda mwisho wa siku tunakuona unachomwa moto kwa wizi mtaani kama Sigara.

Mkuu asanteh kwa ofa ya kibarua.
Ila mimi ni mwajiriwa wa Serikali pale Dodoma. Nimekuja Moshi kikazi!
Kama unahitaji chochote naweza kukusaidia niko hapa Leopard Hotel..Karibu
 
ushawahi kuona wanyakyusa wananyoenda kuzika?!"!hao wachaga hawaoni ndani sanasana watawazidi hayo magari unayoyaita ya kifahari,huku mbeya tunazika kwa vigelegele na matarumbeta full shangwe
 
Wanabodi habari ya leo,

Binafsi naomba kusema ni vyema kuwajali na kuwahifadhi wapendwa wetu waliotutoka kwa njia nzuri na ambazo ziko kihalali kulingana na mila, desturi, tamaduni na dini tunazoziamini. Lakini pia niseme ni masikitiko sana kuondokewa na mtu katika jamii yetu na kaya zetu, lakini hayo huwa ni mapenzi ya Mwenyenzi Mungu kikubwa ni kuwaombea wapumzike kwa amani waliko tangulia.

Sasa, naomba nishangae mambo yanayoendelea kwa wenzetu Wachaga, kwakweli misiba yao ni sherehe kubwa, majigambo, ufahari mkubwa hakika hii sidhani kama ni jambo zuri hasa kwa wale ambao wanakuwa wamempoteza ndugu yao.

Misiba inakuwa mpaka na Pombe na vinywaji vingine vikali? Ufahari wa magari ya bei kubwa? Yote haya ni kwa faida ya nani? Mfano ukikaa barabara ya Arusha - Moshi utastaajabu utitiri wa magari ya kifahari kwenda kwenye msiba Moshi, hivi hili linawasaidia kweli wafiwa?

Utakuta mtu anatoka msibani analalamika, hoo mimi sikupata bia au hoo mimi sijala nikashiba. Kweli kweli ndugu zangu mmefikia huku....Hakika inaumiza sana.

Nimeyaona ndio maana nimesema, nisichukiwe kwa kusema ukweli!!

SIO JAMBO JEMA AU LENYE AFYA.

Mandla.

Kiujumla, Makafiri hawana cha kujifunza katika kifo!
Karibu katika Uislaam, wote tupo sawa, tunavalishwa sanda kama Yesu alivyo vyalishwa. Hakuna mbwembwe, wala hutakaa zaidi ya saa 48 kabla ya kuzikwa. Na popote pale palipo ardhi, unazikwa.
 
ushawahi kuona wanyakyusa wananyoenda kuzika?!"!hao wachaga hawaoni ndani sanasana watawazidi hayo magari unayoyaita ya kifahari,huku mbeya tunazika kwa vigelegele na matarumbeta full shangwe

Hamna cha kujifunza!
 
Fanyaaa yako usifatilie mambo ya wengine
Garama waingie wengine kuumia unaumia wewe
 
Kiujumla, Makafiri hawana cha kujifunza katika kifo!
Karibu katika Uislaam, wote tupo sawa, tunavalishwa sanda kama Yesu alivyo vyalishwa. Hakuna mbwembwe, wala hutakaa zaidi ya saa 48 kabla ya kuzikwa. Na popote pale palipo ardhi, unazikwa.

Tutolee udini wako humu....kenge weee
 
Mkuu asanteh kwa ofa ya kibarua.
Ila mimi ni mwajiriwa wa Serikali pale Dodoma. Nimekuja Moshi kikazi!
Kama unahitaji chochote naweza kukusaidia niko hapa Leopard Hotel..Karibu

Mwajiri dodoma!!!!!we umeajiriwa sector gani na umesomea nini na chuo gani au ndo wale wa muslim university.ila kwa nionavyo mhh hata muslim university hujapita.unajua great thinkers wana uwezo wa kumtambua mtu kama kasoma au la we inaonekana mfua nazi rufiji
 
Back
Top Bottom