Kulikoni ATCL Safari za Ndani?

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
18,035
Reaction score
25,031
Haya madaraja ya ATCL safari za ndani yana tofauti gani? TWiga Basic, Twiga Gain, Twiga Comfort, Twiga Business. Inakuwaje ndege moja inakuwa na madaraja mengi kiasi hicho? Nimezowea kuona ndege nyingi zikiwa na Business Class na Economy Class tu, ila hapa kwa ATCL ninashindwa kuelewa.


Nimetafuta ticket za ATCL Dar-Mwanza-Arush-Dar kati ya tarehe za August 9 hadi August 28 inaonekana zipo za madaraja ya juu tu halafu ile ya Mwanza Arusha niliyoweka hapo juu ni inalazmisha mtu aenede Dara Kwanza ndipo anede Aurusha na kutumia karibu siku nzima. Je hizi ndege zipiga trip moja moja moja au abiria ni wengi kiasi kuwa zinaelemewa? Je ile ndege ya Mwanza Dar kupitia Arusha na Zanzibar haipo tena siku hizi?
 
Ikiwa one way inakuwa cheap kiasi

Wakikuzungusha kidogo tu na hela inapanda..
 
Dunia nzima mashirika ya ndege yapo hivyo sio atcl tu,jifunze zaidi utaelewa
 
Hakuna ndege ya moja kwa moja (Direct flight) kati ya Mwanza na Arusha.

Unachukuliwa na ndege inayotoka Mwanza - Dar es Salaam halafu baadaye utachukuliwa na ndege nyingine ya Dar es Salaam - Arusha. Hii ni connected flight.

Kama unaenda Arusha au Moshi njia rahisi ni kukwea ndege ya Mwanza - Kilimanjaro halafu ukifika KIA kuna shuttle bus za kuwapeleka Arusha au Moshi, mnalipa TZS 10,000.00 tu na inatumia around dakika 45 mpaka Arusha.

Mumshukuru sana Magufuli kufufua shirika la ndege walau sasa mnapata cha kuuliza na kuanzishia uzi. 😁
 
Bofya “SELECT” hapo itakupa maelezo zaidi
 
Mmeshindwa Kumshukuru aliyewajengea Barabara ya Lami ,Siku hizi Ata Mvua ikinyesha hampiti Tena Nairobi. Mnakuja kutulazimisha Ujinga.
 
Dunia nzima mashirika ya ndege yapo hivyo sio atcl tu,jifunze zaidi utaelewa
Post yangu ilikuwa na mambo mawili; wewe unaongelea lipi. Kuhusu madaraja ya usafiri wa anga dunia nzima ni mawili tu: Business Class na Economy Class. Yanaweza kuvunjwa kuwapo kwa Premiumu Econdomy na First Class lakini hiyo ni kwenye ndege za long range tu zenye msafa ya kuazia masaa saba na kuendelea. Uwezi kukuta ndege inayoruka msaa mawili tu ikiwa na makundi yaho ya premium Economy na First Class. Wewe unatumia ndege za dunia gani hiyo.




 
Jibu lako ni zuri, ila umelimaliza vibaya kwa kusema "mmushukuru;" lugha za generalization huwa sizipendi.

Zamani kulikuwa na ATCL kutoka Mwanza kwenda Dar kupitia Arusha na Zanzibar, nilidhani ruti hiyo bado ipo. Ngoja nitabuku ya KIA.
 
Bora hata lisingefufuka,
Hili shirika limeleta dhahama,
Nauli wamezidisha maradufu mno,
Bora ilivokuepo fast jet, nauli ya ndege huwazi
 
Bora hata lisingefufuka,
Hili shirika limeleta dhahama,
Nauli wamezidisha maradufu mno,
Bora ilivokuepo fast jet, nauli ya ndege huwazi
Si kweli, kuna kipindi tulikuwa tunahangaika sana. Nauli ya MWZ - DAR ilikuwa hadi laki nane. Siku hizi laki tatu tu imezidi sana laki nne. Fastjet walikuwa na bei nzuri sana, sijui siri ya mafanikio ilikuwa ipi.
 

Ila kama taifa tunasafari ndefu. Mtu mwanza arusha inakulazimu kuwe na layover kuku connect flighy na unakula unatumia masaa hadi 6 kwa iyo safari. Ili halijakaa vizuri kabisa. Utasema una nchi za wageni
 
Madaraja ya kiwiziwizi.
Kama Wana abiria wengi wasingelazimisha mtu kupitia usikotaka, ingeenda moja kwa moja utakako.
 
Ila kama taifa tunasafari ndefu. Mtu mwanza arusha inakulazimu kuwe na layover kuku connect flighy na unakula unatumia masaa hadi 6 kwa iyo safari. Ili halijakaa vizuri kabisa. Utasema una nchi za wageni
Dar-Kigoma ndio utakubali mziki Sasa.Pipa linatoka Dar linatua Dodoma hapo mtakaa mpk utajuta(yaani Ni Kama vile hiace inavyo okoteza wateja njiani).Baadae ndio ngoma inaamsha kutoka Dom to Kigoma.
 
Si kweli, kuna kipindi tulikuwa tunahangaika sana. Nauli ya MWZ - DAR ilikuwa hadi laki nane. Siku hizi laki tatu tu imezidi sana laki nne. Fastjet walikuwa na bei nzuri sana, sijui siri ya mafanikio ilikuwa ipi.
Wacha ujinga wewe, tulikuwa tunaa kwa 80,000/= na fast jet. Hiyo laki nane labda Precision Air.
 
Daaaaaa....fast jet c waje tena Tanzania.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…