Maneno ya busara sana haya. Unamtuma aendelee kujifunza jinsi ya kukabiliana na changamoto za ufugaji, na elimu hii haipatikani darasani, ni mtaan tu. Na mtaan kwenyewe ni kupitia waliofanikiwa na waliofeli.Umeleta malalamiko au ushauri?
Watu hizo ndo kazi zetu tuna zaidi ya miaka8 sasa ndani ya kazi wewe miezi6 tu lakini pole mkuu jipange kwa sababu umezijua changamoto zake basi upo karibu na mafanikio
Kuna dalali anaepata hasara, kuna dalali wa ufugaji kwa zaidi ya miaka8?Wewe unafuga au dalali?
Umeleta malalamiko au ushauri?
Watu hizo ndo kazi zetu tuna zaidi ya miaka8 sasa ndani ya kazi wewe miezi6 tu lakini pole mkuu jipange kwa sababu umezijua changamoto zake basi upo karibu na mafanikio
Sawa nimekupata mkuu, ila mimi nimeshindwa kujua kama yeye amekata tamaa, ndio mana nimemuuliza malalamiko au ushauri au wewe mkuu kwa uelewa wako mwenzetu anahitaji nini hapo na km ushauri kivipi?Mkuu mimi nafikiri ungemsaidia kwa kumpa mawazo mbadala. Kwa ulichoandika hujamsaidia.
Sawa nimekupata mkuu, ila mimi nimeshindwa kujua kama yeye amekata tamaa, ndio mana nimemuuliza malalamiko au ushauri au wewe mkuu kwa uelewa wako mwenzetu anahitaji nini hapo na km ushauri kivipi?
Vizuri mkuu, ili kuepuka na gharama kubwa za vyakula yampasa kwanza afanye window shop ili kujua bei mbalimbali za vyakula km vile ambavyo amepost kuwa bei tajwa hapo juu, pia yapasa afahamu kuwa km kuku atawaanzishia kwa chakula cha gharama nafuu basi ni bora kuendelea na chakula hicho na kwa kampuni hiyo inayozalisha bidhaa hiyo ili impatie tofauti ya chakula cha kuku wadogo, wa wiki mbili na wakubwa, kuliko kuchanganya aina tofauti ya vyakula na kampuni, pia ni bora kuanza na chakula cha gharama ndogo kisha kupanda nao kwa chakula bora zaidi kwa gharama kubwa hii itapelekea improvement kwa kuku na siyo kuanza lishe ya elfu 71 kisha unamalizia kwa lishe ya elfu45 kwa kuku wakubwa lazima utawaona km wana utapiamlo.Ni kweli mkuu, japo hakuwa straight moja kwa moja, lakini nafikiri anachangamoto kupata chakula cha kuku kwa bei nzuri, na kama kuna mbadala wake.
Wakati mwingine mtu kama huyu aliyekata tamaa, jawabu lake ni kumpa moyo kwa utashi wa yeye kuendelea mbele.
Kama chakula kilichochanganywa tiali unaona kina gharama kubwa jaribu kununua ingredients zinazohitajika uchanganye mwenyeweSijaleta malalamiko, ila nimeleta uzoefu nilioupata kwa miezi 6. Sijakata tamaa, naendelea
Salami wana JF.
Naleta mada hii ya uzoefu wangu katika kufuga kuku wa nyama (broilers).
Nimekuwa mfugaji kwa miezi sita sasa. Awali nilipewa matumaini sana kuwa wana biashara nzuri kama ambavyo wengi wanavyoaminishwa humu.
Lakini ufugaji huu una changamoto nyingi kiasi ambacho faida yake hutaiona.
Tatizo kubwa ni gharama ya Chakula. Ni kweli hawa kuku wanachukua hadi week 5 hadi uwauze, lakini chakula chake ni bei ghali, inabidi ujipanhe sana maana kukibwenyewe wakisha fikisha week ya tatu wanakula kama wamechanganyikiwa.
Kuna brand nyingi za vyakula na bei inatofautiana na ubora. Inaanzia kati ya Sh52,000 hadi Sh71,000 kwa kilo 50.
Inategemea unafuga kuku wangapi ndio ujue watatumia kiasi gani.
Hao kuku wanakula usiku na mchana, hawana mapumziko, sasa ole wako uwafanyie ubahili. Utashangaa zimefika week 5 hawauziki. Hasara.
Au wakati mwingine ukiwabadilishia chakula walichozoea wanadumaa.
Inabidi uwe na mtaji wa kutosha kuwalisha kikamilifu kwa mwezi mzima. Kama una hela ya mawazo usifanye hii biashara.
Ahsanteni
Hahah mkuu jipe moyo usichoke mapema kaza buti endelea na biashara yako ya kujiajiri.
Umemalizia,kama una hela ya mawazo uachane na hii biashara! Naomba ufafanuzi maana ya "hela ya mawazo"Sijaleta malalamiko, ila nimeleta uzoefu nilioupata kwa miezi 6. Sijakata tamaa, naendelea
Ok,nimekuelewa. Naomba mchanganuo wako wa mpango fedha uliokuangusha na huu mahsusi utakaoanza nao kwa broiler 100 ili nijifunze. Asante.Namaanisha uwe na hela mahsusi kwa biashara hiyo.
Sijui kama nimekuelewa vizuri, lakini nilianza kwa kifuga Kuku 300 Sh1,200@ nikatumia mifuko 13 ya Chakula @ Sh65,000. Nikauza Sh5,300 @ kuku baada ya mwezi.Ok,nimekuelewa. Naomba mchanganuo wako wa mpango fedha uliokuangusha na huu mahsusi utakaoanza nao kwa broiler 100 ili nijifunze. Asante.
Ulikaribia kunielewa,nilitaka kujua mapato na matumizi ili nijue faida au hasara ilitokana na nini. Na uliposema utaendelea,umerekebisha wapi.Sijui kama nimekuelewa vizuri, lakini nilianza kwa kifuga Kuku 300 Sh1,200@ nikatumia mifuko 13 ya Chakula @ Sh65,000. Nikauza Sh5,300 @ kuku baada ya mwezi.
Niliongeza 400 kwa miezi kadhaa, 500, 600 na sasa namalizia kuku 700.
Ninakupongeza kwa kulifikisha kundi lote hadi mauzo bila kufa hata mmoja. Kwani mkuu kwa makisio,faida inaweza kuwa asilimia ngapi ya pesa yote uliyotumia (ukiondoa gharama ya Mabanda na vilishio)Kuku wa nyama wanafaida kama ukifuga wengi. Mimi ninafuga hawa kuku. Nilianza na kuku 200 kwa mara ya kwanza. Ninawalisha chakula toka kampuni ya Hill. Hawa jamaa chakula chao ni pellets , wana starter,growers na finisher nilitumia mifuko nane. Walipofika wiki ya nne niliuza kuku 100 kwa being ya sh. 5000 na walipofika wiki ya tank niliuza kuku 100 Kwa bei ya sh 5,500 .Nilipata jumla ya sh 1,050,000. Faida ilipatikana kiasi ila kuna mambo kadhaa nilijifunza kama vile kuhakikisha kuku unaowaingiza sokoni wamefikia uzito unaoridhisha, kupunguza ghàrama za uendeshaji kadiri inacyowezekana, kufuga kuanzia kuku 300 nakuendelea, uwe na chakula cha kutosha, at least uwe na batch mbili na kuendelea kwa mwezi mmoja au hizo wiki tano. Mimi huwa nauza kwa hao jamaa wa hapo Mbagala rangi tatu sokoni. Nilicho experience solo ni kubwa has a kuku wakiwa na uzito unaoridhisha.