Kukomoana katika ada baada ya COVID-19

Kukomoana katika ada baada ya COVID-19

Mr Sir1

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2018
Posts
1,787
Reaction score
8,118
Japokuwa serikali kupitia Wizara ya Elimu iliasa juu ya shule kutokukomoa wazazi baada ya likizo hii ya lazima, nyingi ya shule imeenda kinyume kwa kuleta ujanja wa kuongeza lisaa limoja au mawili na baada ya hapo kupandisha ada kwa karibia 50%.
Mfano hai ni shule ya Genius Kings iliyopo Tabata.

Wamekaa wakatunga ujanja ujanja wa masaa kupelekea ada ya sehemu ya muhula iliyokuwa 440,000 kwenda mpaka kuwa 660,000 na hii sio kwa kipindi kimoja tu bali vipindi vyote kati ya June-Aug na Sept-Dec. Wanajaribu kufidia miezi mitatu ya kufungwa shule kwa kuibia wazazi kwa kiini macho cha jedwali la masaa.

Serikali ina haja ya kuingilia kati katika hili laa sivyo wazazi wengi watashindwa kupeleka watoto shule maana wengi wetu ni wahanga wa COVID baada ya shughuli nyingi za uchumi kudorora.

Screenshot_20200623_141603.jpg
Screenshot_20200623_141549.jpg
Screenshot_20200623_141536.jpg
 
Hayo ndiyo mawazo ya waTanganyila walio wengi. Hawataki hata kudai haki yao. Kila linalopangwa na yoyote wanakubali tu.
Kabisa......

Mimi mwenyewe am puzzled, muhula uliopita wa covid nililipa nikabakiza 200,000#......tu...... Sasa hapa ndio ujumbe umeingia tumalize ada yote ya muhula uliopita na tulipe na hii........

Unalipiaje huduma ambayo hujatumia??????

Kama nchi tunakwenda wapi??????

Viongozi wetu wakwapi watoe ufafanuzi??????

Au Serikali in fungu lake toka private schools tujue........

It's a shame
 
Hayo ndiyo mawazo ya waTanganyila walio wengi. Hawataki hata kudai haki yao. Kila linalopangwa na yoyote wanakubali tu.
Na kwa fikra hizi za kuwa hakuna namna ndio maana wachache wanajikuta wana haki zaidi ya wengine. Kwa swala kama la ada wazazi wote wakigoma shule lazima isalimu amri lakini wanatokea wale wa 'pambana tu hamna namna' kupelekea wengine wote waathirike.
 
Na kwa fikra hizi za kuwa hakuna namna ndio maana wachache wanajikuta wana haki zaidi ya wengine. Kwa swala kama la ada wazazi wote wakigoma shule lazima isalimu amri lakini wanatokea wale wa 'pambana tu hamna namna' kupelekea wengine wote waathirike.

Hi nchi Bana, sijui Nyerere aliifanyaje.......majitu yanaonewa, yanasema hamna namna.
 
Hi nchi Bana, sijui Nyerere aliifanyaje.......majitu yanaonewa, yanasema hamna namna.
ukiuliza unaambiwa ni nchi inayopenda amani. Kutokujua kuna tofauti kubwa kati ya kuwa na amani na kuwa limbukeni. Sisi ni malimbukeni wa kuamini kama halikuathiri liache lipite, hatma yake ndio tumefika hapa tulipofika sasa.
 
Na kwa fikra hizi za kuwa hakuna namna ndio maana wachache wanajikuta wana haki zaidi ya wengine. Kwa swala kama la ada wazazi wote wakigoma shule lazima isalimu amri lakini wanatokea wale wa 'pambana tu hamna namna' kupelekea wengine wote waathirike.
kweli kabisa
 
Kabisa......

Mimi mwenyewe am puzzled, muhula uliopita wa covid nililipa nikabakiza 200,000#......tu...... Sasa hapa ndio ujumbe umeingia tumalize ada yote ya muhula uliopita na tulipe na hii........

Unalipiaje huduma ambayo hujatumia??????

Kama nchi tunakwenda wapi??????

Viongozi wetu wakwapi watoe ufafanuzi??????

Au Serikali in fungu lake toka private schools tujue........

It's a shame
kuna unyanyasaji mwingi sana katika hizi shule za private ambao wazazi tunakutana nao. Na wamiliki wanakuwa na kiburi kikubwa wakiamini hakuna tunachoweza wafanya.
 
Shida yote hii ni kutokana na elimu kubinafsishwa, mbona kipindi cha nyuma serikali ilikuwa inatoa elimu bora sana tena kwa ada ndogo..
 
Enzi zetu ilikuwa ukikosa shule ya serikali yaan unajiona kichwani hazimi kbs, ilikuwa sifa kubwa kusoma shule ya serikali.
Ila kwa sasa hali imekuwa tofauti
Shida yote hii ni kutokana na elimu kubinafsishwa, mbona kipindi cha nyuma serikali ilikuwa inatoa elimu bora sana tena kwa ada ndogo..
 
Sasa mkuu tatizo ni nini? Hauna hela au ? Kwanza hio shule ni ya kawaida sana ukilinganisha na huduma inayotolewa hapo na hizo ada haifananii kabisa..we lipa ada tu
 
Kuna shule nyingi wazazi wameambiwa walipe ada kwa vile waliendelea na masomo kwa internet. Hilo sawa, lakini ilitakiwa meal na accommodation viondolewe.
Na kwa fikra hizi za kuwa hakuna namna ndio maana wachache wanajikuta wana haki zaidi ya wengine. Kwa swala kama la ada wazazi wote wakigoma shule lazima isalimu amri lakini wanatokea wale wa 'pambana tu hamna namna' kupelekea wengine wote waathirike.
 
Sasa mkuu tatizo ni nini? Hauna hela au ? Kwanza hio shule ni ya kawaida sana ukilinganisha na huduma inayotolewa hapo na hizo ada haifananii kabisa..we lipa ada tu
Kuna mawili kama wewe si mwalimu wa shule mfano wa hiyo niliotolea mfano basi ni wazi huna mtoto unaesomesha. Si kila jambo unalitolea comment ili tu ionekane umecomment ndugu unless una maslahi binafsi katika hii topic.
 
Kuna shule nyingi wazazi wameambiwa walipe ada kwa vile waliendelea na masomo kwa internet. Hilo sawa, lakini ilitakiwa meal na accommodation viondolewe.
hata kama sio wazazi wote walishiriki katika hayo masomo ya online kutokana changamoto nyingi sana ikiwemo wa ujuzi wa kushiriki hayo masomo ya online.
 
Sasa mkuu tatizo ni nini? Hauna hela au ? Kwanza hio shule ni ya kawaida sana ukilinganisha na huduma inayotolewa hapo na hizo ada haifananii kabisa..we lipa ada tu

Mzazi kala ada
 
Back
Top Bottom