Kukimbiza Mwenge Kumepitwa na Wakati!

Kukimbiza Mwenge Kumepitwa na Wakati!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
26,021
Reaction score
25,425
Kukimbiza mwenge nchi nzima kwa kisingizio cha kufungua miradi ya maendeleo ni suala lililopitwa na wakati. Watetezi wa mbio za mwenge wanadai kuwa mwenge ni kwa ajili ya kuzindulia miradi ya maendeleo! Je, bila mwenge hiyo 'miradi' haiwezi kuzinduka? Hii ni sababu ya kizamani sana na ambayo haina mantiki yoyote katika karne hii. Kabla ya kung’ang’ania kukimbiza mwenge ni bora tukatafakari madhara yatokanayo na mbio za mwenge:

Mosi, shughuli ya kukimbiza mwenge husababisha kuenea kwa ukimwi kupitia kwenye mikesha ya mwenge. Angalau kila wilaya unakopita mwenge, wananchi hukesha kwenye mikesha ya mwenge huku wakishindwa kujikita kwenye shughuli za maendeleo. Katika mikesha hii ndipo wananchi hulewa na kufanya ngono zembe ambazo hupelekea kupata maambukizi ya zinaa, pamoja na ugonjwa hatari wa ukimwi.

Pili, wafanyakazi wa umma hupoteza muda wa kufanya kazi za maendeleo kwani mwenge ukipokelewa kwenye wilaya fulani shughuli zote za kimaendeleo husimama na badala yake watumishi wote hujikita ktk maandalizi ya mapokezi na kukimbiza mwenge. Hili ndilo kundi ambalo huathirika zaidi na mbio za mwenge. Mwenge unatarajiwa kupokelewa hapa majuma matatu yajayo. Lakini cha ajabu watu wameacha kufanya kazi kila siku wapo kwenye vikao vya maandalizi ya mwenge. Hivi ni tija kiasi gani itakayopotea kwa kutokufanya kazi kwa majuma matatu kwa kisingizio cha vikao vya maandalizi ya mapokezi ya mwenge huu wa kipuuzi?

Tatu, pamoja na upotevu wa muda wa kazi, watumishi wa umma, hasa walimu, hukatwa sio chini ya Tsh. 20,0000 kutoka kwenye mishahara yao kwa lazima kwa ajili ya kuchangia mafuta ya mwenge na viburudisho kwa wakimbiza mwenge. Hii huwatia hasara walimu na kuzidi kuwakandamiza kiuchumi, pamoja na kwamba mishahara yao ni duni sana.

Na nne, mwenge husababisha utoro kwa wanafunzi hivyo kuwarudisha nyuma kielimu na kusababisha matokeo mabaya kwenye mitihani yao. Mwenge ukifika kwenye wilaya, wanafunzi hutolewa madarasani na kuamrishwa kusimama barabarani kuushangilia mwenge; na ikiwa kuna mwalimu mkuu atakayeshindwa kuwatoa wanafunzi darasani, hufutwa kazi au kushushwa cheo. Aidha, wanafunzi husimamishwa masomo kwa muda wa takribani wiki nzima wakitunga na kujifunza nyimbo za kuusifia mwenge siku ya mapokezi na mkesha. Kibaya zaidi, wanafunzi, wengi wao wakiwa wa kike, hukesheshwa kwenye mikesha ya mwenge wakiimba nyimbo za kuusifu mwenge usiku kucha. Hapa ndipo wanafunzi wengi hupewa mimba zisizotarajiwa na hata kuambukizwa ukimwi.

Kuna haja ya serikali kuangalia upya falsafa ya mwenge hasa kwa kuzingatia madhara yatokanayo na mbio za mwenge ukilinganisha na makusudio yake. Katika karne hii ya dijitali, ni aibu kupoteza muda wa wananchi kwa kuwalazimisha kukimbiza moto kwa sababu ambazo hazina kichwa wala miguu.

mwenge.jpg

:yield:
 
Katika hili nakuunga mkono sioni sababu ya kuendelea kupoteza mamilioni na muda kwa ajili ya kitu kisicholeta faida...


Mwenge uhifadhiwe makumbusho tu
 
hawawezi kuacha kuukimbiza cjui una maagano huo mwenge aliyeuanzisha mwenyewe hayupo
 
Ni upuuzi,,haya ni miongoni mwa ya kijinga aliyoacha Mwalimu.
 
Leo kuna njemba imepiga mweleka na mwenge chini hapa Kigoma..ahamadi!!! Mafuta yoote yakamwagika chini!! Kilichotokea sasa baada ya hapo!!
 
Katika hili nakuunga mkono sioni sababu ya kuendelea kupoteza mamilioni na muda kwa ajili ya kitu kisicholeta faida...


Mwenge uhifadhiwe makumbusho tu

Ni wewe au a/c yako iko hacked? Kwa mara ya kwanza leo umeanza kujitambua. Keep it up!
 
Leo kuna njemba imepiga mweleka na mwenge chini hapa Kigoma..ahamadi!!! Mafuta yoote yakamwagika chini!! Kilichotokea sasa baada ya hapo!!

Hayo mafuta yangemuunguza mwili mzima ili liwe fundisho kwa wapumbavu wengine wenye kiherehere kama chake.
 
Hamjui kama nyerere alikua masonic mkubwa? mwenge ni 1 ktk rogo zao!!
 
Sijawahi kuuona mwenge kwa macho. Kila mara ukipita huwa nipo kwenye harakati zangu. Tarehe 24 utapita huku Mpui - Sumbawanga, natarajia kwenda zangu mashambani kuangalia mahindi.
 
upuuzi wa nyerere

Uchawi wa kututawala bila kujijua kuwa anatukandamiza ndio maana alikuwa akiona sehemu fulani wanaanza kumshtukia basi mwaka unaofuata mwenge unalala hapo hapo
 
ni zaidi ya mwenge, una mambo mengi,ni kama zindiko la nchi, na serikali haiwezi kuufuta, hata ninyi mnaobwata humu mkishakuwA Viongozi mtalazimika kufanya hayo na kama mtakataa mtawekwa out of system..........
 
Leo kuna njemba imepiga mweleka na mwenge chini hapa Kigoma..ahamadi!!! Mafuta yoote yakamwagika chini!! Kilichotokea sasa baada ya hapo!!

Mkuu hii habari yako imekaa vizuri sana tatizo umeeleza kwa kifupi sana ilikuwaje na baada ya hiyo tochi kuanguka wakafanya nini ?

Itapendeza sana ikiwa km utaanzisha thread yake halafu utuelezee kilichojili hapo,unajua habari kama hii huwezi ipata gazetini wala redioni ni hapa tu jf.
 
Back
Top Bottom