Kukataliwa kunauma

Kukataliwa kunauma

bidam90

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2013
Posts
273
Reaction score
203
Ni binti tuliojuana naye kwa muda wa kama miezi minne sasa, tulianza kufahamiana kupitia WhatsApp, tukachat muda mrefu mpaka kufikia kuwa wapenzi, japo tulikuwa mikoa ya mbali.

Tulitumiana picha na videos na kujuliana hali muda wote, basi tu ili tuzidi kuwa karibu japo hatukuwahi kuonana uso kwa uso! Leo ni siku ambayo sitoisahau maishani, mwangu! Nimefunga safari ya kuja kuonana nae, tulikutana na binti muda wa kama masaa mawili hivi, tukatembea na kuzungumza pamoja huku kila mmoja wetu akiwa mchangamfu kwa mwenzake.

Nilimuandalia na zawadi ndogo tu nikampa. Mida ya jioni ilipofika tuliachana na kila mmoja kuelekea nyumbani anakoishi. Nimefika nyumbani, nakuta message ya yule binti kwenye simu yangu ikisema "Samahani, moyo wangu umeshindwa kukupenda, naomba unisamehe".

Ilibidi nimpigie simu muda ule ule kumuuliza kwanini, lakini hakunipa jibu, aliniambiya tu hata yeye hajui moyo tu umekataa. Roho imeniuma sana. Najiuliza mpaka sasa ni nini alichotaka kuona kutoka kwangu, kama ni hali ya maisha nilimuelzea ukweli kitambo, muonekano wangu, ongea yangu vyote anavijua!

Roho inaniuma sana. Nimeshindwa kwakweli kukaa nalo moyoni nikaona nililete huku kwenu kwa ushauri.

Wadau, tatizo itakuwa nini? Au mnanishauri nini juu ya hili? Maana nipo njia panda.
 
Sijui amepatwa na nini,ila pole. Kubali tu matokeo japo sio rahisi,ila huwezi kulazimisha maji kupanda mlima. Jiweke pembeni subiri wa kwako
 
Labda hajavutiwa na wewe baada ya kukuona. Au maybe jinsi mazungumzo yenu yalivyokuwa, na jinsi alivyoobserve baadhi ya Vitu vyako, akajikuta moyo wake umekukataa.

Blind dates zina challenges pia haswa inapotokea mnakutana afu wewe ndo ukakolea while mwenzako akakukinai. Sio issue lakini, shukuru tu Mungu dada wa watu kawa honest na wewe, hajataka kukupa matumaini wala kukupotezea muda. Shukuru kwa yote, jikaze maisha yaendelee.
 
Msema kweli mpenzi wa Mungu. Au ulikuwa umevaaje.? Maana usikute mkanda haukumatch na viatu... au hukupiga mswaki vizuri. Au hukubrush viatu, au ulipaka unyunyu mkali sana, au suruali haikuendana na shati... au ulinyoa kibwenzi... au hukupaka deodorant?

Au ulidundika sana mrembo akamind? au ulilipa bill hukutoa wallet ukafinyia hela mfukoni? Au story zako zilikuwa za my anko... my braza... my anti? Au hukwenda straight to the point?

Naomba usinichukie, nimejaribu kuangalia sehemu zinazotuput off wakinadada...
 
Broo, uyo mtt hakukukubali tangu zaman sema alikua hana uhakika wa hisia zake so alitegemea atleast akikuona ataona kitu flan special kutoka kwako tofauti na alivokufaam wasap ili angalau kimvutie, niwaz hakukupenda tangu zamani bado alikua anatafta sababu yakukupenda na ndoivo hajaiona,we ni mtt wa kiume kukataliwa kawaida,so tupa kule angalia kulia na kushoto kama hakuna gari linalokuja vuka upande wa pili kuna wengi wanakusubiria
 
Aliyekwambia mchumba anatafutwa kwa whatsapp nani?...jipe moyo na uwe mvumilivu Mungu atakuletea mwingine.
 
Badilika kuanzia leo, dont trust a girl (anybody). Kitu nilichokiobserve kwa wanawake, akili zao zinafanya kazi kama computer, especially kwenye mahusiano. Wakati wewe unawaza kitu kimoja, mwenzio ashafanya calculation sita kichwani na majibu anayo.

THINK!! Anzisha mahusiano kwa trust ya 50% coz hawa wenzetu ndivyo walivyo.
 
Umekosea sana.. Wenzio hzo blind date tunazifanyia maghetoni.. Demu unakua umemshapanga kwamba anakuja gheto.. Akija gheto ukishindwa kula papuchi hiyo ni ujinga wako. Ukila papuchi hata kama aseme hakutaki haiumi..
Kaka tupo ndani ya mwezi wa ramadhan hivo haikuwezekana kufanya hivyo wote tulikuwa tumefunga!hata kukumbatiana haikuwezekana
 
Msema kweli mpenzi wa Mungu. Au ulikuwa umevaaje.? Maana usikute mkanda haukumatch na viatu... au hukupiga mswaki vizuri. Au hukubrush viatu, au ulipaka unyunyu mkali sana, au suruali haikuendana na shati... au ulinyoa kibwenzi... au hukupaka deodorant?

Au ulidundika sana mrembo akamind? au ulilipa bill hukutoa wallet ukafinyia hela mfukoni? Au story zako zilikuwa za my anko... my braza... my anti? Au hukwenda straight to the point?

Naomba usinichukie, nimejaribu kuangalia sehemu zinazotuput off wakinadada...

Labda ni story ndo hazikumvutia kwasababu alikuwa na haraka ya kurudi home kwan mda ulikuwa umeenda! Mavazi yalikuwa ya kawaida (t-shirt nyeupe,jeans nyeuc na raba nyeupe)! nilimuuliza ka ni muonekano wangu aniambie ukweli akasema muonekane haukuwa na shida!!

Nimeomba niutane nae tena jumamosi ndo atakuwa free!!Ngoja nikamsikilize kama kabadili msimamo wake au ananijaribu
 
Labda hajavutiwa na wewe baada ya kukuona. Au maybe jinsi mazungumzo yenu yalivyokuwa, na jinsi alivyoobserve baadhi ya Vitu vyako, akajikuta moyo wake umekukataa.

Blind dates zina challenges pia haswa inapotokea mnakutana afu wewe ndo ukakolea while mwenzako akakukinai. Sio issue lakini, shukuru tu Mungu dada wa watu kawa honest na wewe, hajataka kukupa matumaini wala kukupotezea muda. Shukuru kwa yote, jikaze maisha yaendelee.
Si kwamba labda ananijaribu pengine!!Tumepanga kukutana nae jumamosi ngoja nikamsikilize!!ka vp napiga chini siwezi kulazimisha kupenda pasipopendeka
 
Msema kweli mpenzi wa Mungu..........au ulikuwa umevaaje......?......maana usikute mkanda haukumatch na viatu.......au hukupiga mswaki vizuri..........au hukubrash viatu.........au ulipaka unyunyu mkali sana........au suruali haikuendana na shati........au ulinyoa kibwenzi..........au hukupaka deodorant.......?.......au ulidundika sana mrembo akamind........?.....au ulilipa bill hukutoa wallet ukafinyia hela mfukoni............?.......au story zako zilikuwa za my anko.....my braza.......my anti...........?.......au hukwenda straight to the point.......?.....

Naomba usinichukie........nimejaribu kuangalia sehemu zinazotuput off wakinadada..........

Huyu dada nashindwa kumtathimin sijui ni mnene au mwembamba, mfupi au mrefu,sijui ni wamakamo au binti
 
Duuh .. pole dear.. huyo hakuwa wako pray and God will give you .. Pole sana..kwa yaliyokukuta... its very pain .. just remember God hasn't forget about you.. wako yuko njiani.. Thanks..
 
Duuh .. pole dear.. huyo hakuwa wako pray and God will give yours ... Pole sana..kwa yaliyokukuta... its very pain .. just remember God hasn't forget about you.. wako yuko njiani.. Thanks..
 
Labda ni story ndo hazikumvutia kwasababu alikuwa na haraka ya kurudi home kwan mda ulikuwa umeenda!Mavazi yalikuwa ya kawaida(t-shirt nyeupe,jeans nyeuc na raba nyeupe)! nilimuuliza ka ni muonekano wangu aniambie ukweli akasema muonekane haukuwa na shida!!

Nimeomba niutane nae tena jumamosi ndo atakuwa free!! Ngoja nikamsikilize kama kabadili msimamo wake au ananijaribu

Mbona kama ulipendeza tu.......labda hizo raba zilikuwaje.....?.....isije kuwa zile ulimi nje.......au mkate boflo........unajua swala la viatu wadada tunaangalia sana.........
Lakini kwa maelezo yako.......nadhani ulipendeza........dada tu anataka kukuletea tashtiti......we kutana nae hiyo jumamosi.......halafu uje utuambie kasemaje.........
Usisahau kunitag........sawa eeeh.......
 
Back
Top Bottom