Kujiuzulu Lowassa kulinishtua-Sitta

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
[h=3][/h]

*Asema alimbabatiza bila kutarajia hali hiyo
*Akiri kushindwa kuahirisha kikao cha bunge
*Asema mpambano dhidi ya Dowans bado mbichi


Na Edmund Mihale

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Samuel Sitta, amesema kuwa
katika uongozi wake wa Spika wa Bunge la Tisa jambo lilomuumiza zaidi na kumshtua ni siku ambayo Bw. Edward Lowassa alipojiuzulu Uwaziri Mkuu.

Bw. Lowassa ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa nane wa Tanzania alijiuzulu Februari 7, 2008 baada ya kutajwa katika ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison mwakyembe kuchunguza kashfa ya utoaji zabuni bila kufuata taratibu kwa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.

Katika taarifa hiyo, Bw. Lowassa aliyekuwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, alitajwa kuwa alikuwa anashinikiza kampuni hiyo kupewa zabuni na hivyo kutakiwa apime mwenyewe maamuzi yake yameathiri vipi serikali na hadhi ya bunge, hivyo akaamua kujiuzulu kwa maelezo kuwa alikuwa anawajibika.

Akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV juzi usiku, Bw. Sitta alisema kuwa siku hiyo ilikuwa ngumu kwake kutoka na uamuzi uliochukuliwa na Bw. Lowassa, kwa kuwa hakuwa anautarajia.

"Baada ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuchunguza kashfa ya Richmond, nilitegemea kuwa wabunge watajadili, waoneshe upungufu na wapi ripoti hiyo imekosewa na tuijadili na kuifanyia kazi.

"Baada ya Dkt. Mwakyembe kumaliza kusoma hotuba hiyo kulikuwa na wabunge kama watano au sita hivi waliomba kuchangia taarifa hiyo lakini, Bw. Lowassa aliomba aanze kuchangia yeye kabla ya wabunge hao.

"Unajua kwa taratibu zetu, Waziri Mkuu ambaye ndiye kiongozi wa shughuli za serikali bungeni anapoomba nafasi ya kuchangia lazima umpe kipaumbele, nilidhani anataka kurekebisha au kuchangia taarifa hiyo kumbe akatangaza kujiuzulu Uwaziri Mkuu.

"Waziri Mkuu anapojiuzulu maana yake serikali nayo imeanguka, hivyo hakukuwa na serikali, bunge likashindwa kuendelea na sikuweza kufunga bunge siku hiyo, ilinilazimu kumuona rais ili atoe maelekezo naye alifanya hivyo, nikaaihirisha bunge," alisema Bw. Sitta.

Alisema kuwa jambo hilo lilitokea huku akiwa hana matarajio, hivyo kumpa wakati mgumu kufanya uamuzi wa haraka.

Malipo ya Dowans

Bw. Sitta katika mahojiano hayo alisisitiza msimamo wake kutaka Dowans isilipwe mabilioni hayo, akisema kuwa msimamo wake upo pale pale na kwamba atapambana hadi mwisho.

“Unajua kuwa ukifika katika umri wangu unakuwa umepitia na kuona mambo mengi, unatakiwa kuwa mkweli.

"Sikiliza, mbona mnakuwa kama hamna uzalendo, Dowans ni biashara ya kipumbavu…nawashangaa hata hao wanaotulaumu sisi kuwa ndio tumeifikisha nchi katika hatua hiyo ya kutakiwa kulipa deni hilo. Dowans ni wizi ambao kila Mtanzania anapaswa kuulaani ushenzi huu badala ya kushangilia,” alisema Bw. Sitta

Alifafanua kuwa mkataba ulioingia na kampuni hiyo haukuwa sahihi kwakuwa ulikiuka sheria za ununuzi.

Kwa mujibu wa Bw. Sitta, kampuni hiyo ilitakiwa kuingia mkataba na Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO lakini zabuni hiyo ilipitiwa na tume iliyoundwa kutoa serikalini, jambo ambalo lilikuwa ni ukiukaji wa mkataba huo.

Alisema kuwa bodi ya TANESCO ilindaa mkataba kwa kuipa kampuni hiyo vipengele 24 ambayo ilitakiwa kuvitimiza ndipo ipewe zabuni hiyo, lakini tume ilivipunguza hadi kufikia vinne ambavyo navyo ilishindwa kuvitimiza.

Alisema kuwa tume hiyo iliipa kampuni hiyo mkataba wa mwaka mmoja lakini waziri aliyejiuzulu (hakumtaja jina) aliongeza mkataba huo na kuwa wa miezi 24.

Ingawa Bw. Sitta hakutaja jina waziri huyo, mawaziri wawili waliojiuzulu kwa kashfa hiyo zaidi ya Bw. Lowassa, ni wawili, Bw. Nazir Karamagi na Dkt. Ibrahim Msabaha, waliokuwa wameshika wizara ya Nishati na Madini kwa nyakati tofauti.

Bw. Sitta ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki, alisema kampuni hiyo baada ya kufikisha miezi 22 ikiwa imelipwa fedha za capacity charge ( za kuweka mitambo) sh. milioni 152 kila siku bila kuzalisha umeme iliuzwa kwa kampuni ya Dowans

"Fedha hizi zilitosha kabisa kwa kampuni hiyo kujiendesha na baada ya kuuzwa ingekuwa na faida kubwa," alisema Bw. Sitta.

Alisema ni jambo ambalo halimuingii akilini kuona kuna watu wanajiita Mahakama ya Usuluhishi, wanakaa katika Hoteli ya MovenPick jijini Dar es Salaam na kuamua kuwa serikali iilipe Dowans mabilioni ya shilingi huku wakiwa wamelipwa fedha za kukaa katika hoteli hiyo kuamua mambo yasiyofaa.

Bw. Sitta alifananisha mkataba huo sawa na mwizi wa simu ambaye alitaka kuiuza kwa sh. 100,000 akalipwa malipo ya awali ya sh. 60,000 lakini aliyenunua akataa kumalizia malipo yaliyobaki, huku akihoji, "je, mwizi huyo atakuwa na haki ya kudai malipo hayo wakati akijua kuwa simu hiyo ni mali ya wizi?"

Bw. Sitta, maarufu kama Spika wa Kasi na Viwango, katika Bunge lililopita alisimama imara pamoja na baadhi ya wabunge waliojipambanua kama wapambanaji wa ufisadi kupinga Kampuni ya Richmond (na baadaye Dowans) na kuishinikiza serikali ivunje mkataba huo.

Alisema kuwa Watanzania wanapaswa kuwa na uzalendo wa kulipigania taifa lao badala ya kukatishwa tamaa kwa kutishwa kuwa Dowans lazima ilipwe.

“Kwanza nikuhakikishie huu si mwisho wa mapambano, Dowans kulipwa ni sawa na kuhalalisha ushenzi wa majizi hayo, hatuwezi kushangilia, nitapinga hadi mwisho," alisema Bw. Sitta.

ICC iliitia hatiani TANESCO kwa kosa la kuvunja mkataba na Dowans iliyokuwa ikitetewa na wakili wa kimataifa, Bw. Kennedy Fungamtama na ikaiamuru iilipe tuzo hiyo ya sh bilioni 94 na riba ya asilimia 7.5.

Hatua hiyo ya kuchelewesha malipo ya tuzo hiyo itaifanya TANESCO sasa kulipa kiasi kikubwa zaidi, kwani riba imekuwa inaongezeka, na hadi tuzo hiyo inasajili na Mahakama Kuu nchini, Dowans ilikuwa inastahili kulipwa na Tanesco sh bilioni 113 badala ya sh bilioni 94.
 
*Asema alimbabatiza bila kutarajia hali hiyo
*Akiri kushindwa kuahirisha kikao cha bunge
*Asema mpambano dhidi ya Dowans bado mbichi


Na Edmund Mihale

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Samuel Sitta, amesema kuwa
katika uongozi wake wa Spika wa Bunge la Tisa jambo lilomuumiza zaidi na kumshtua ni siku ambayo Bw. Edward Lowassa alipojiuzulu Uwaziri Mkuu.

Bw. Lowassa ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa nane wa Tanzania alijiuzulu Februari 7, 2008 baada ya kutajwa katika ripoti ya Kamati ya Bunge iliyoongozwa na Mbunge wa Kyela, Dkt. Harrison mwakyembe kuchunguza kashfa ya utoaji zabuni bila kufuata taratibu kwa Kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond.

Katika taarifa hiyo, Bw. Lowassa aliyekuwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, alitajwa kuwa alikuwa anashinikiza kampuni hiyo kupewa zabuni na hivyo kutakiwa apime mwenyewe maamuzi yake yameathiri vipi serikali na hadhi ya bunge, hivyo akaamua kujiuzulu kwa maelezo kuwa alikuwa anawajibika.

Akizungumza katika kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na ITV juzi usiku, Bw. Sitta alisema kuwa siku hiyo ilikuwa ngumu kwake kutoka na uamuzi uliochukuliwa na Bw. Lowassa, kwa kuwa hakuwa anautarajia.

"Baada ya ripoti ya Kamati Teule ya Bunge kuchunguza kashfa ya Richmond, nilitegemea kuwa wabunge watajadili, waoneshe upungufu na wapi ripoti hiyo imekosewa na tuijadili na kuifanyia kazi.

"Baada ya Dkt. Mwakyembe kumaliza kusoma hotuba hiyo kulikuwa na wabunge kama watano au sita hivi waliomba kuchangia taarifa hiyo lakini, Bw. Lowassa aliomba aanze kuchangia yeye kabla ya wabunge hao.

"Unajua kwa taratibu zetu, Waziri Mkuu ambaye ndiye kiongozi wa shughuli za serikali bungeni anapoomba nafasi ya kuchangia lazima umpe kipaumbele, nilidhani anataka kurekebisha au kuchangia taarifa hiyo kumbe akatangaza kujiuzulu Uwaziri Mkuu.

"Waziri Mkuu anapojiuzulu maana yake serikali nayo imeanguka, hivyo hakukuwa na serikali, bunge likashindwa kuendelea na sikuweza kufunga bunge siku hiyo, ilinilazimu kumuona rais ili atoe maelekezo naye alifanya hivyo, nikaaihirisha bunge," alisema Bw. Sitta.

Alisema kuwa jambo hilo lilitokea huku akiwa hana matarajio, hivyo kumpa wakati mgumu kufanya uamuzi wa haraka.

Malipo ya Dowans

Bw. Sitta katika mahojiano hayo alisisitiza msimamo wake kutaka Dowans isilipwe mabilioni hayo, akisema kuwa msimamo wake upo pale pale na kwamba atapambana hadi mwisho.

“Unajua kuwa ukifika katika umri wangu unakuwa umepitia na kuona mambo mengi, unatakiwa kuwa mkweli.

"Sikiliza, mbona mnakuwa kama hamna uzalendo, Dowans ni biashara ya kipumbavu…nawashangaa hata hao wanaotulaumu sisi kuwa ndio tumeifikisha nchi katika hatua hiyo ya kutakiwa kulipa deni hilo. Dowans ni wizi ambao kila Mtanzania anapaswa kuulaani ushenzi huu badala ya kushangilia,” alisema Bw. Sitta

Alifafanua kuwa mkataba ulioingia na kampuni hiyo haukuwa sahihi kwakuwa ulikiuka sheria za ununuzi.

Kwa mujibu wa Bw. Sitta, kampuni hiyo ilitakiwa kuingia mkataba na Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO lakini zabuni hiyo ilipitiwa na tume iliyoundwa kutoa serikalini, jambo ambalo lilikuwa ni ukiukaji wa mkataba huo.

Alisema kuwa bodi ya TANESCO ilindaa mkataba kwa kuipa kampuni hiyo vipengele 24 ambayo ilitakiwa kuvitimiza ndipo ipewe zabuni hiyo, lakini tume ilivipunguza hadi kufikia vinne ambavyo navyo ilishindwa kuvitimiza.

Alisema kuwa tume hiyo iliipa kampuni hiyo mkataba wa mwaka mmoja lakini waziri aliyejiuzulu (hakumtaja jina) aliongeza mkataba huo na kuwa wa miezi 24.

Ingawa Bw. Sitta hakutaja jina waziri huyo, mawaziri wawili waliojiuzulu kwa kashfa hiyo zaidi ya Bw. Lowassa, ni wawili, Bw. Nazir Karamagi na Dkt. Ibrahim Msabaha, waliokuwa wameshika wizara ya Nishati na Madini kwa nyakati tofauti.

Bw. Sitta ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Urambo Mashariki, alisema kampuni hiyo baada ya kufikisha miezi 22 ikiwa imelipwa fedha za capacity charge ( za kuweka mitambo) sh. milioni 152 kila siku bila kuzalisha umeme iliuzwa kwa kampuni ya Dowans

"Fedha hizi zilitosha kabisa kwa kampuni hiyo kujiendesha na baada ya kuuzwa ingekuwa na faida kubwa," alisema Bw. Sitta.

Alisema ni jambo ambalo halimuingii akilini kuona kuna watu wanajiita Mahakama ya Usuluhishi, wanakaa katika Hoteli ya MovenPick jijini Dar es Salaam na kuamua kuwa serikali iilipe Dowans mabilioni ya shilingi huku wakiwa wamelipwa fedha za kukaa katika hoteli hiyo kuamua mambo yasiyofaa.

Bw. Sitta alifananisha mkataba huo sawa na mwizi wa simu ambaye alitaka kuiuza kwa sh. 100,000 akalipwa malipo ya awali ya sh. 60,000 lakini aliyenunua akataa kumalizia malipo yaliyobaki, huku akihoji, "je, mwizi huyo atakuwa na haki ya kudai malipo hayo wakati akijua kuwa simu hiyo ni mali ya wizi?"

Bw. Sitta, maarufu kama Spika wa Kasi na Viwango, katika Bunge lililopita alisimama imara pamoja na baadhi ya wabunge waliojipambanua kama wapambanaji wa ufisadi kupinga Kampuni ya Richmond (na baadaye Dowans) na kuishinikiza serikali ivunje mkataba huo.

Alisema kuwa Watanzania wanapaswa kuwa na uzalendo wa kulipigania taifa lao badala ya kukatishwa tamaa kwa kutishwa kuwa Dowans lazima ilipwe.

“Kwanza nikuhakikishie huu si mwisho wa mapambano, Dowans kulipwa ni sawa na kuhalalisha ushenzi wa majizi hayo, hatuwezi kushangilia, nitapinga hadi mwisho," alisema Bw. Sitta.

ICC iliitia hatiani TANESCO kwa kosa la kuvunja mkataba na Dowans iliyokuwa ikitetewa na wakili wa kimataifa, Bw. Kennedy Fungamtama na ikaiamuru iilipe tuzo hiyo ya sh bilioni 94 na riba ya asilimia 7.5.

Hatua hiyo ya kuchelewesha malipo ya tuzo hiyo itaifanya TANESCO sasa kulipa kiasi kikubwa zaidi, kwani riba imekuwa inaongezeka, na hadi tuzo hiyo inasajili na Mahakama Kuu nchini, Dowans ilikuwa inastahili kulipwa na Tanesco sh bilioni 113 badala ya sh bilioni 94.

Sidhani kama huyu mzee anasema ukweli ,lakini sitashangaa kwa maana siku zote Babu Sitta huwa anachokiongea sicho anachokiamini
 
Asante Mhe Sitta, kwa Dowans halipwi mtu labda CCM iamue tu kujilipa leo na kuachia ngazi kwenye siasa kesho yake tu bila kuchelewa.
 
Back
Top Bottom