JAPUONY
JF-Expert Member
- Jul 16, 2010
- 383
- 186
Ndugu Wanabodi,
Suala la kujitoa kwa ndugu Mwapachu CCM na kudai Kuwa ati CCM siyo mamake, siyo suala geni. Wafukunyungu kama sisi tulilifahamu hili sikunyingi na tulisubiria litokee. Wengine bado wapo an watafuata siku si nyingi!
Kama alivyoeleza yeye binafsi, Mwapachu alikuwa ni TeamLowassa , Lowaasa akiwa bado yuko CCM. Mwapachu ni miongoni mwa makada wa CCM waliokuwa wakigawa fedha za Lowassa pale DODOMA. Mwapachu alikuwa ni miongoni mwa walioratibu msafara wa vijana waendesha bodaboda walioendesha pikipiki hadi Dodoma kumuomba EL agombee Urais. Ni Mwapachu huyu huyu aliandaa (kwa kushirikiana na Team Lowassa) CV za watakaowekwa katika nafasi mbalimbali mara EL atakapotinga Ikulu kupitia CCM.
kubwa zaidi na kilichofanya ajitoe CCM, Balozi Mwapachu ameahidiwa na aliahidiwa nafasi ya UWAZIRI WA MAMBO ya NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA. Tunalifahamu hili na list nzima ya Walioahidiwa Ukuu wa Mikoa, Wilaya, Wizara, Ubalozi, na Ukatibu Mkuu ipo.
Ninachotaka kuwaambia ni kuwa hao wanaotoka CCM siyo kwa sababu wanataka MABADILIKO YA KWELI in kwa sababu wanafuata maslahi. Wanaotaka mabadiliko ha kweli walikuwa CDM tangu hata kabla ya uchaguzi mkuu kuanza. Kuweni makini mnaposhabikia wanaojiondoa CCM muda huu wa kampeni Zambia lala salama!
nawasilisha.
Suala la kujitoa kwa ndugu Mwapachu CCM na kudai Kuwa ati CCM siyo mamake, siyo suala geni. Wafukunyungu kama sisi tulilifahamu hili sikunyingi na tulisubiria litokee. Wengine bado wapo an watafuata siku si nyingi!
Kama alivyoeleza yeye binafsi, Mwapachu alikuwa ni TeamLowassa , Lowaasa akiwa bado yuko CCM. Mwapachu ni miongoni mwa makada wa CCM waliokuwa wakigawa fedha za Lowassa pale DODOMA. Mwapachu alikuwa ni miongoni mwa walioratibu msafara wa vijana waendesha bodaboda walioendesha pikipiki hadi Dodoma kumuomba EL agombee Urais. Ni Mwapachu huyu huyu aliandaa (kwa kushirikiana na Team Lowassa) CV za watakaowekwa katika nafasi mbalimbali mara EL atakapotinga Ikulu kupitia CCM.
kubwa zaidi na kilichofanya ajitoe CCM, Balozi Mwapachu ameahidiwa na aliahidiwa nafasi ya UWAZIRI WA MAMBO ya NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA. Tunalifahamu hili na list nzima ya Walioahidiwa Ukuu wa Mikoa, Wilaya, Wizara, Ubalozi, na Ukatibu Mkuu ipo.
Ninachotaka kuwaambia ni kuwa hao wanaotoka CCM siyo kwa sababu wanataka MABADILIKO YA KWELI in kwa sababu wanafuata maslahi. Wanaotaka mabadiliko ha kweli walikuwa CDM tangu hata kabla ya uchaguzi mkuu kuanza. Kuweni makini mnaposhabikia wanaojiondoa CCM muda huu wa kampeni Zambia lala salama!
nawasilisha.