Kuishi na ndugu wa mume

Bi dentamol

JF-Expert Member
Feb 1, 2014
987
1,912
kuna mdogo wangu anamchumba wake ambae process zote za kuoana tayar japo jamaa kaomba hajajipanga kufunga ndoa sasa hv uchumi haujakaa sawa anaomba amchukue kwanza ndoa baadae

bint amepanga kwake mkoa tofauti na jamaa sasa jamaa kamuomba akae na mtoto wa dada binti kamaliza form 4 mwaka huu. hataki kurudi kijijin hivyo akae kwa bint siku ya kuolewa ikifika wataenda pamoja kw a jamaa maana jamaa hawez kukaa na ndugu yake kwa sasa anataka kuchukua likizo hivyo akae kwa bidada mpaka akitaka kuolewa ndio atamchukua binti anasema kukaa nae sio shida Ila tabia zake ndio shida

Alishawahi kukaa nae anavitabia flan vinakera hana heshima wala uoga anaweza maliza kuoga akachukua nguo yako akavaa bila kuomba yaan anavitabia tu vya ajabu ajabu ukimgombeza kidogo anaanza kulia, alishakaa nae mwez 1 alihisi kuumwa sasa hv anataka aje akae mda wote mpaka atakapo pata maisha yake,

anashindwa amjibuje mchumba wake anaogopa kukataa ataonekana hapend ndugu bado mapema na akikubal anahisi changamoto kubwa bora angekua anakuja kusalimia tu kuliko kuishi nae siku zote
anaomba ushaur afanyeje au amjibu mini jamaa?
 
Bora nusu shari kuliko shari kamili, mshauri akatae tu kuish nae huyo binti!
 
kuna mdogo anamchumba wake ambae process zote tayar ila jamaa kaomba hajajipanga kufunga ndoa sasa hv uchumi haujakaa sawa anaomba amchukue kwanza
ndugu + wazazi wapande zote 2 wamekubal watafunga mwaka kesho waishi tu wote


kilichonileta kwenu bint anachumba chake lkn mwez unao anatakiwa ahamie mkoa mwingine kwa jamaa
leo jamaa kama na mada anaomba akae na mtoto wa Dada ake jamaa, kamaliza form 4 hataki kurudi kijijin hivyo akae kwa bint siku ya kuolewa ikifika wataenda pamoja kw a jamaa maana jamaa hawez kukaa na ndugu yake kwa sasa anataka kuchukua likizo hivyo akae kwa bidada mpaka akitaka kuolewa ndio atamchukua


Bint anasema kukaa nae sio shida Ila niwale mabint dizain ya wale watu wasio na heshima wala uoga hana heshima anaweza maliza kuongea akachukua nguo yako akavaa bila kuomba yaan anavitabia tu vya ajabu ajabu ukimgombeza kidogo anaanza kulia,,, alishakaa nae mwez 1 alihisi kuumwa sasa hv anataka aje akae mda wote mpaka atakapo pata maisha yake,,,,,

anashindwa amjibuje mchumba wake anaogopa kukataa ataonekana hapend ndugu bado mapema na akikubal anahisi changamoto kubwa bora angekua anakuja kusalimia tu kuliko kuishi nae siku zote
maisha ni kusaidiana
 
Kama alisha wahi kaa naye anamjua tabia mmm atafute sababu mambo mengine kupeana stress
 
Back
Top Bottom