Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Kama 'mwanamke akikuambia hana hisia na wewe tena basi anza kufungasha na ujiandee kuondoka'. Hayo yalikuwa ni maneno ya ushauri wa mama wa makamo kwa vijana wanaopitia misukosuko ya mapenzi. Ushauri huo ulitokana na uzoefu wake kuhusu hali ambayo mwanamke katika jamii fulani alipohojiwa kwa nini hawezi kurudiana na mwanaume wake aliitanabahisha hivi kwa kifupi: 'mtima mtitu'. Hali hii, inayomaanisha 'moyo mweusi', inasemekana humtokea mwanamke pale ambazo hisia zake zote kwa mwanaume fulani aliyekuwa anampenda hugubikwa na wingu zito jeusi.
Lakini kuna wataalamu wa masuala ya mapenzi wanaodai hisia ni sehemu tu ya mapenzi na sio msingi mkuu. Kwa mtazamo wao mapenzi ni maamuzi. Yaani, kupenda ni kuamua. Si hisia. Hivyo maadam ukishaamua kumpenda mtu fulani basi inabidi uendelee (kuamua) kumpenda kila siku hata kama hujisikii. Wataalamu hao wamejikita katika mtazamo wa kiimani kuwa ukishapendana na mtu kikamilifu ni mauti tu yanayoweza kuwatenga - si hisia wala nini.
Swali la msingi ni, je, ukijisikia 'mtima mtitu' unapaswa kufanya nini? Kuvumilia kisabuni tu? Au kubwaga manyanga?
Lakini kuna wataalamu wa masuala ya mapenzi wanaodai hisia ni sehemu tu ya mapenzi na sio msingi mkuu. Kwa mtazamo wao mapenzi ni maamuzi. Yaani, kupenda ni kuamua. Si hisia. Hivyo maadam ukishaamua kumpenda mtu fulani basi inabidi uendelee (kuamua) kumpenda kila siku hata kama hujisikii. Wataalamu hao wamejikita katika mtazamo wa kiimani kuwa ukishapendana na mtu kikamilifu ni mauti tu yanayoweza kuwatenga - si hisia wala nini.
Swali la msingi ni, je, ukijisikia 'mtima mtitu' unapaswa kufanya nini? Kuvumilia kisabuni tu? Au kubwaga manyanga?