Ndugu yangu ameingia kwenye siku zake(hedhi) maarufu kama Period kabla ya muda.
Kwa mwezi huu mzunguko ulitokea tarehe 6 hadi 10. Lakini leo kaona siku zake tena.
Tangu aanze kupata siku zake hajawahi kutokewa na hali ya kuwahi au kuchelewa kupata hedhi kwenye mzunguko wa siku zake.
Nimejaribu kumuuliza kama anatatizo ambalo linaweza kusababisha hii hali kutokea nimebaini kuwa ana msongo wa mawazo kwa siku kadhaa toka ijumaa ya wiki iliyopita maana yeye ni mwanafunzi wa Chuo.
Pia nimemuuliza kama anahisi maumivu yoyote kwa kutokewa na hii hali, kasema hahisi maumivu yoyote isipokuwa ana bleed kwa mfululizo( kwa kutoka matone matone ya damu ) toka asubuhi saa 3 hadi sasa hivi ninavyoandika huu uzi jioni hii.
Akina mama, Madaktari, Manesi au Wajuvi wote wa haya mambo mliopo humu, hii hali inatokana na tatizo gani hasa? Mbali na sababu niliyoibaini mimi kwa uelewa wangu.
Jee tiba yake ni nini?.
Msaada tumusaidie ndugu yetu kutokana na hii hali.
Ahsanteni!
Kwa mwezi huu mzunguko ulitokea tarehe 6 hadi 10. Lakini leo kaona siku zake tena.
Tangu aanze kupata siku zake hajawahi kutokewa na hali ya kuwahi au kuchelewa kupata hedhi kwenye mzunguko wa siku zake.
Nimejaribu kumuuliza kama anatatizo ambalo linaweza kusababisha hii hali kutokea nimebaini kuwa ana msongo wa mawazo kwa siku kadhaa toka ijumaa ya wiki iliyopita maana yeye ni mwanafunzi wa Chuo.
Pia nimemuuliza kama anahisi maumivu yoyote kwa kutokewa na hii hali, kasema hahisi maumivu yoyote isipokuwa ana bleed kwa mfululizo( kwa kutoka matone matone ya damu ) toka asubuhi saa 3 hadi sasa hivi ninavyoandika huu uzi jioni hii.
Akina mama, Madaktari, Manesi au Wajuvi wote wa haya mambo mliopo humu, hii hali inatokana na tatizo gani hasa? Mbali na sababu niliyoibaini mimi kwa uelewa wangu.
Jee tiba yake ni nini?.
Msaada tumusaidie ndugu yetu kutokana na hii hali.
Ahsanteni!