Kuigawa Mbeya: Ushauri wa JF Kuhusu Mlowo

Kuigawa Mbeya: Ushauri wa JF Kuhusu Mlowo

Basi kwa mantiki hii Ukerewe nayo iwe mkoa ili kuwasogezea raia huduma za muhimu...!
 
Umejenga hoja vizuri sana Ileje. Ila naona umesahau kipengele muhimu sana hapo. Chunya hawakuomba kujitenga. Walioomba kujitenga ni Rungwe! Hilo unalisemeaje?
Kama kweli Chunya hawakuomba na hawaoni haja ya wao kujitenga na Mbeya basi ni bora wakajenga hoja ya wao kubaki mkoa wa Mbeya! Lakini nionavyo mimi wanafurahia wazo hilo na hata mimi ningefurahia kupewa hadhi hiyo!

Kuhusu wenzetu wa Rungwe ni kweli kama ulivyoeleza katika hoja yako kuwa ni wabaguzi, wakabila na wasiopenda kushirikiana au kuwasaidia wenzao kujikwamua katika lindi la umaskini! Tabia hii si ya leo au jana bali toka enzi za wakoloni! Wanyakyusa hawa wa milimani waliwabagua wenzao wa mabondeni na wakawabagua zaidi watu wa Ileje kiasi kwamba kuna baadhi ya wandali ambao kutokana na ubaguzi huo na kujiona wanyonge wakajibatiza kuwa wanyakyusa au wakabadili lugha yao ili kwa kiasi kikubwa ifanane na kinyakyusa!! Ajabu sana hii!!!

Kwa hiyo kama wenzetu hawa wa Rungwe bado wanang'ang'ania kutaka mkoa basi nashauri wapewe hadhi ya kuwa angalau mkoa mdogo au nusu ili wapate amani ya moyo!! Hii ni kwa sababu naelewa hoja yao ya kutaka kujitenga haijafutwa kabisa kwa kuwa hata katika mkoa huo wa Mbeya walikobakizwa bado wataendeleza hoja hiyo kupitia mlango wa nyuma!!
 
Ilishasemwa Ubaguzi Mbaya!
Nyie mkafikiri ni Ubaguzi wa Kikabila tu na Kidini.
Hata huu wa Kimikooa eti huduma hazifiki? My foot! Zilifikaje zamani?
Nasisi Rufiji tunataka MKOA na Mkulu lazima Asimamie hili kabla hajatoka, Na Makao makuu ni Kibiti.Hatutaki kuwa Mkoa wa Pwani kwani ni Mkubwa sana, Na kufuata Huduma Kibaha ni Mbali sana, We Fikiria Mtu utoke MKURANGA, RUFIJI uje mkoani Kibaha, Inawezekana Kweli? Kwanza Tuna mafuta na Gas lazima tujitenge na Msoga.
 
Kama kweli Chunya hawakuomba na hawaoni haja ya wao kujitenga na Mbeya basi ni bora wakajenga hoja ya wao kubaki mkoa wa Mbeya! Lakini nionavyo mimi wanafurahia wazo hilo na hata mimi ningefurahia kupewa hadhi hiyo!

Kuhusu wenzetu wa Rungwe ni kweli kama ulivyoeleza katika hoja yako kuwa ni wabaguzi, wakabila na wasiopenda kushirikiana au kuwasaidia wenzao kujikwamua katika lindi la umaskini! Tabia hii si ya leo au jana bali toka enzi za wakoloni! Wanyakyusa hawa wa milimani waliwabagua wenzao wa mabondeni na wakawabagua zaidi watu wa Ileje kiasi kwamba kuna baadhi ya wandali ambao kutokana na ubaguzi huo na kujiona wanyonge wakajibatiza kuwa wanyakyusa au wakabadili lugha yao ili kwa kiasi kikubwa ifanane na kinyakyusa!! Ajabu sana hii!!!

Kwa hiyo kama wenzetu hawa wa Rungwe bado wanang'ang'ania kutaka mkoa basi nashauri wapewe hadhi ya kuwa angalau mkoa mdogo au nusu ili wapate amani ya moyo!! Hii ni kwa sababu naelewa hoja yao ya kutaka kujitenga haijafutwa kabisa kwa kuwa hata katika mkoa huo wa Mbeya walikobakizwa bado wataendeleza hoja hiyo kupitia mlango wa nyuma!!

Umenena vema Ileje. Ni kweli kwamba lengo la uzi huu ambalo pengine halikutegemewa linaweza likawa haja ya kutumbua hiki kijipu cha kuusambaratisha mkoa wetu. Nani hasa mwanzilishi wa wazo hili? Lakini pia kuna faida gani tunapata katika kusambaratika huku. Je serikali imechukua hatua sahihi katika kushughulikia suala la kuusambaratisha mkoa?

Nikubaliane na wewe kwamba Chunya wamekosa miundo mbinu mingi kwa miaka mingi na kuleta shida kwa ndugu zetu Wabungu kuna wakati huwa napata wasiwasi kama wanajisikia ni wakazi wa Mkoa wetu. Nina mdogo wangu anaishi Chunya mjini kajenga kule. Sijawahi kuenda kule kumjulia hali kwa sababu tu ya shida ya usafiri. Lakini hilo la kusahaulika ni kweli kuhusu Ileje Pia. Nina biashara ambayo inanipa nafasi ya kujua kwamba wafanyabiashara wenzangu wanaokaa Chunya na Ileje wanalipia gharama kubwa sana kufadhili safari za mafundi kutoka Mbeya Mjini kwenda ama Chunya, ama Ileje. Fundi wa mashine akisikia neno Chunya, au Ileje, anajua hiyo ni kazi ya siku mbili hadi tatu, wakati ambapo anaweza kwenda Tunduma, Kyela Vwawa--au hata Makambako akafanyakazi na kurudi kulala nyumbani Mbeya.

Nirudi kwenye hoja: Rungwe wanataka kujitenga. Hilo limezaa Wazo la kuitenga Chunya, lakini pia limezaa wazo la Mbozi na Ileje kutaka kujitenga. Kwa mtizamo huo Rungwe wameleta utengano katika mkoa.

Serikali imefanya sawa katika lile ambalo imefanya? Kwa mara ya kwanza naomba niseme ndiyo. Serikali imekwepesha Rungwe ikiwa inajua hilo linaweza kuleta shida kati ya Kyela na Rungwe yenyewe huko mbele. Yanaweza kuzuka masuala ya Ruzuku za Serikali na mtawanyo wa maendeleo watu wakakatana mapanga na kuchomeana nyumba pale. Kwa hiyo dawa ni kuwabakiza hawa katika pool moja inaitwa Mkoa wa Mbeya. Serikali wamefanya sawa kuwanyima Rungwe Mkoa kwa sababu Mkoa huo ungelazimisha Kyela, na pengine Ileje kuwa ndani, na Rungwe wangewasumbua sana Kyela na Ileje kwa misimamo ya wazi na ya siri kuwa wao ndo haswa wakubwa, ambao waliomba mkoa na wakaupewa! Nadhani wewe pia umeafiki mtizamo wa serikali. Hapo tupo pamoja.

Kuhusu Chunya kutengwa ama kujitenga--kama wanataka--hili niseme lingejadiliwa na WanaChunya wenyewe waangalie kama kuna faida kwenye lipi: Pesa za kuugawa mkoa ziboreshe miundombinu Chunya na Ileje hasa, ama pesa hizo zipewa makandarasi wa kujenga majengo ya makao makuu ya Mkoa wa Chunya ili watu wa Ileje wabaki na miundo mbinu mibovu kama ilivyo sasa na kulazimika kusafiri umbali mrefu kufuata makao makuu Chunya.

Binafsi nadhani kitu sahihi ni kuboresha miundombinu kwenye haya maeneo mawili: Hivi Tukiwa na Lami safi kati ya Mbeya Mjini na Chunya Mjini, halafu tukaweka Lami safi kati ya Mbeya mjini na Ileje--hasa kupitia njia mkato inayoanzia Njia panda ya Iyula, kuelekea Idiwili , kupitia Hezya hadi Itumba. Huoni kama Mbeya mjini patafikika kirahisi sana kati kwa kila mtu? Ujue kwa kuweka lami safi kwenye maeneo ambayo nimeyataja, Mtu aliyepo Chunya na Aliyepo Itumba watafika pengine wakati huohuo Mbeya Mjini na mtu ambaye anatakoka Kyela.

Wakati huo huo uboreshaji wa miundombinu--hasa hasa barabara utakuwa na faidi nyingi za ziada ukiachana na hili la kufikika kwa urahisi makao makuu ya mkoa. Wagonjwa watafika Rufaa haraka, wahalifu wa jinai kubwa watafika haraka mahakama kuu Mbeya mjini. Huduma chake zinazolazimika kufanyika mkoani kwa kuwa haziwezekani wilayani zitafuatwa na kufikika kwa urahisi Mbeya mjini.

Mimi kwa kweli nadhani kitu sahihi ni kuboresha miundo mbinu badala yakuongeza gharama za kuendesha serikali kule Mbeya. Kama kuna mtu ana pesa zinamuwasha kujenga majengo na kuajiri rundo la watu Mkwajuni nashauri ajenge lami kwenda Chunya na Ileje na hizo hela.
 
Ilishasemwa Ubaguzi Mbaya!
Nyie mkafikiri ni Ubaguzi wa Kikabila tu na Kidini.
Hata huu wa Kimikooa eti huduma hazifiki? My foot! Zilifikaje zamani?
Nasisi Rufiji tunataka MKOA na Mkulu lazima Asimamie hili kabla hajatoka, Na Makao makuu ni Kibiti.Hatutaki kuwa Mkoa wa Pwani kwani ni Mkubwa sana, Na kufuata Huduma Kibaha ni Mbali sana, We Fikiria Mtu utoke MKURANGA, RUFIJI uje mkoani Kibaha, Inawezekana Kweli? Kwanza Tuna mafuta na Gas lazima tujitenge na Msoga.

Mkuu, okoa foot yako hapo! Kwa nini usitaje ni huduma gani hasa ambazo mtu wa Rifiji analazimika kuzifuata Kibaha kila wiki (au hata kila mwezi) --ambazo hazipatikani wilayani kwako--ili serikali ilete ATM ya hizo huduma nyiiiiiiingi za Kimkoa zinazolazimisha makao makuu kujengwa kwa sababu hazipatikani wilayani kwako, ili tuokoe gharama za kujenga mijengo ya makao makuu ya mkoa mapya na kuajiri maFFU na watendaji wengine rundo kumsaidia mkuu wa mkoa wa Rufiji. Ni kipi wilaya zimeshindwa kufanya zilazimishe gharama hizo?
 
mimi nipo sekta binafsi Mkuu wangu. kwa hiyo mtizamo wa serikali upo mbali kidogo nami na sijui hasa wanachokiwaza zaidi ya taarifa za wazi kwenye magazeti na mitandaoni. Ila ninachojua ni kwamba serikali imekataa kuipa idhini Rungwe kuwa Mkoa kama walivyoomba wanaRungwe. Kwa nini wamekataa? hili sasa ni gumu kujua kwa sababu mie nipo nje ya system. Ninachoweza kufanya ni ku-extrapolate na kuweka dhana hisia kama nilivyofanya, kutokana na historia ya usambaratikaji iliyotokana na hisia za ukabila.

Jambo kubwa la kukumbuka hapa ni kwamba Rungwe Waliomba kuwa Mkoa. Chunya hawakuomba kuwa Mkoa, Ileje hawakuomba kuwa mkoa, Mbozi hawakuomba kuwa Mkoa, Momba hawakuomba kuwa Mkoa. Rungwe waliomba kuwa Mkoa.

Rungwe waliomba lini?
 
Mpashaji habari wangu hakunipa tarehe, lakini namwamini ni mkweli. Kwa hiyo ni Kweli Rungwe waliomba kuwa Mkoa lakini sina tarehe kamili ya ombi hili.

Mbona hii imekaa ki-udaku sana? Leta source na date
 
Hivi kuroka moshi kwenda arusha unatumia mda gani?? Hivi toka kibaha kwenda dar unatumia mda gani,. Huko chunya wanakopeleka mkoa wanawapelekea wakina nani?? Huko ni mapoli tu navoijua chunya, wakati kyela na tukuyu zina maeneo madogo lakini zina watu wengi wanaohitaji huduma nyingi za kimkoa
Kuomba kuwa mkoa si kigezo. Unaweza kuwa mchango wao katika kuwakumbusha watawala umuhimu wa kuwasogezea huduma watu wa Chunya. Sioni kabisa mantiki ya kuwa namkoa wa Rungwe mwendo wa nusu saa kutoka Mbeya tukawaacha watu wa chunya ambao lazima watumie siku tatu nje ya nyumbani ili kupata huduma mkoani. (Angalia kambi katoto).
 
Rungwe walitunyonya sana watu wa kyela ila kwa hili la mkoa tupo pamoja
Nilishawahi kuandika hapa kuwa wazo la kuugawa mkoa wa Mbeya lengo lake sio zuri...

Sina uhakika sana ni nani walioibua hii hoja pia hadi sasa sijajua vigezo walivyomulika kama sababu za kuugawa mkoa wetu...

Once Mbeya itapotengeneza mikoa mipya miwili, nina kila sababu ya kuamini vuguvugu zaidi za kujitenga zitaendelea...

Pale Mbeya kuna makabila huwa hayapatani kabisa sasa ukiyaweka mkoa mmoja si itakuwa kasheshe...

Wanyakyusa nje ya Mbeya ni ndugu, lakini ukishaingia Mbeya tu ndipo utajua kuwa kuna Wanyaki wa Kyela na wa Rungwe...na kuna wakati ndugu hawa huwa hawaivii chungu kimoja.
 
Dhana ya kugawa gawa mikoa ni ya kuwagawa watu kwa mabila yao. muasisi mkuu ni CCM.

Tukiendelea hivi haitakuja kushangaza huko mbeleni kila kabila likiwa na ka mkoa kake.

Geographically, Mbeya mjini ipo almost katikati ya makao makuu ya wilaya zote za mkoa wa Mbeya. Kwa bahati nzuri pia ni kwamba asilimia 80 zimeunganishwa na barabara za lami. ni ujinga sana kuzalisha mkoa mwingine kutoka mkoa huu labda ikiwa ni kwa sababu za kisiasa.

Nitakuwa mmoja wa wale wanaopinga ubaguzi huu mpya kupitia dhana ya mikoa mipya.
 
Mkuu samahani hizo km220 hazifiki ni 124 mpaka kwela mjini toka mbeya masahihisho madogo tu
Hasante kwa ufafanuzi mzuri kiongozi ila naomba kukusahihisha Mbeya mjini hadi Kyela sio 120km ni 210km ila zaidi naomba wanao taka kutugawa watumie buzara zaidi kuliko hisia za watu fulani kwani hata mimi sitaki hata kidogo mkoa wangu ugawanywe kwani hapo ni kuongeza maslahi ya watawala na sio wananvhi mfano ni Kyela mjini mji mzima hauna hata barabara ya kiwango cha rami ingawa ni mji mdogo sana so ishu sio ukubwa ishu ni commitment za watawala wetu kutuletea maendeleo. Leo hii watu wa Kyela wanadiliki kusema Mwakyembe sio mbuge wao bali ni mbuge wa Dar es salaam kutokana na kuwatelekeza kwake wana Kyela.
 
Hivi kuroka moshi kwenda arusha unatumia mda gani?? Hivi toka kibaha kwenda dar unatumia mda gani,. Huko chunya wanakopeleka mkoa wanawapelekea wakina nani?? Huko ni mapoli tu navoijua chunya, wakati kyela na tukuyu zina maeneo madogo lakini zina watu wengi wanaohitaji huduma nyingi za kimkoa

Mkuu, hivi kweli unaweza kusema kwa moyo kwamba Chunya hakuna watu ila Kyela na Tukuyu ndiko kuna watu wakuhitaji mkoa!. Uko sahihi kwa mawazo yako.

Ni kwa vigezo gani unaweza kulinganisha population za mikoa ya Arusha na Moshi ni sawa na Tukuyu na Kyela? Kyela kuwa mkoa ajili ya nini? Ka kijiji kale kenye vitongozi ipinda, kasumulu, kapwili, kalumbulu, Itunge, Ngyeke sijui wapi Usale, na Ipande sijui kwa wauaji ndiyo ipewe mkoa? Naomba jamani tuwe serious na hasa linapokuja suala la maendeleo ya taifa.

Roho ya ubaguzi wa huko Kyela mnataka sasa iingie katika mfumo wa taifa? Naomba usiwe mmoja wa wale wanaojiita wakumyetu wanaowish usiku na mchana kufukuza wageni wote, wabaki peke yao. Na sasa unataka kuhalalisha mupewe mkoa kwa sababu hata mkipewa mkoa bado nia ya kutaka kujibagua ama kubagua wengine haitatimia. Bado mtahitaji michango mbli mbali kutoka sehemu na watu wa sehemu zingine duniani.

Twende vizuri tu. Tujadiliane kwa hoja na amani tutafikia muafaka sahihi. Tukiendekeza u mimi , ukabila na ukwetu, tutaend up tena ku split na kuanza kupeana fursa kwa misingi ya koo, n.k.
 
Mbona hii imekaa ki-udaku sana? Leta source na date

Katika tasnia ya upashanaji habari kuna ngazi za kutumia kuamini jambo ni kweli ama uongo. Moja ni kupima nafasi ya chanzo cha udaku. Kama udaku ukiletwa na Kamishna wa Kodi za ndani kuhusu mambo ya kodi. Huo udaku unaweza kuwa ukweli. Hili nimelipata Halmashauri ya wilaya ya Rungwe. Kwa hiyo huu udaku unaweza kuwa ukweli. Unalo?
 
Highlander,
.
Ahsante sana ndugu yangu kwa kujali na pia kuwa mkweli. Ni kweli kwamba, ipo mantiki kubwa ya kuugawa mkoa wa Mbeya kutokana na ukubwa wa eneo, muundo wa ki jiographia na mfumo wake wa kiuchumi. Tatizo kubwa hapa ambalo ndugu zangu wakazi wa Mbeya ambalo hawalioni kwa haraka ni kwamba mipango yao inavutwa na hisia za ukabila zaidi bila kuzingatia madhara ya maamuzi ya jinsi hiyo kwa wanaMbeya wenyewe na serikali kwa ujumla.

Lengo kuu la dhana ya kugawa maeneo ya utawala ni kusogeza huduma za kibinadamu na maendeleo kwa wananchi. Kwa mtazamo wangu huu, napangua kipaumbele cha Rungwe kuwa mkoa na makao makuu ya mkoa mpya kwa sababu Rungwe na Mbeya ni karibu sana. Mbeya kwenda Kyela ni km zisizozidi 120 kufuata urefu wa barabara ambayo ni ya kiwango cha lami hadi Blantyre. Napendekeza Rungwe , Kyela na Ileje ziendelee kuwa chin ya Mkoa wa Mbeya ambapo ni karibu sana na panafikika kwa urahisi bila shida.

Pale kuMbozi, wanahitaji kupewa elimu ya utaifa ili waelewe ni kwa nini kwa sasa mlowo hapawezi kupewa kipaumbele cha kufanyika makao makuu ya mkoa mpya ulilinganisha na ndugu zao wa Chunya.

Chunya ni sehemu iliyojitenga ki jiographia na miundo mbinu. Ni sehemu yenye raslimali nyingi kama madini, mifugo, mazao ya chakula na biashara kwa wingi, lakini pia ni sehemu yenye utajiri mkubwa na miti ya mbao adimu. Umbali na miundo mbinu vinafanya mtu kwenda mkoani kupata hudumu muhimu na mkoa kwenda kutoa huduma chunya iwe shughuli maalumu.

Napendekeza Chunya ifanywe mkoa mpya, makao makuu yakiwa Makongorosi ili kusogeza huduma mbali mbali kwa wananchi wa maeneo hayo. Wazo la Mbozi kuimega iende chunya na sehemu za wilaya ya sikonge linaweza kuangaliwa. Chunya ikiwa mkoa, pamoja na kupeleka huduma kwa Watanzania wanaotabika, pia itaharakisha maendeleo ya miundo mbinu ambazo zitaongeza uzalishaji na pia usafirishaji wa bidhaa kutoka kusini mwa Tanzania kwenda kati kati, magharibi na sehemu zingine za nchi na vaisi vesa.Hii ni kuharakisha maendeleo ya taifa.

Kwa ufupi wanaochukua maamuzi ya jambo hili wasiamue kwa kuangalia influences za walio kwenye decision making functions na interest za ukwetu na ukabila. Waliangalie kwa mitazamo ya Utaifa na maendeleo ya nchi. Hakun sababu ya kurundika maendeleo sehemu moja wakati wananchi wa sehemu zingine wanaumia na huku nao wanatoa kodi kama wengine.

Nawasilisha.

Kulipa kodi sio issue kwa serikali yetu
 
Dhana ya kugawa gawa mikoa ni ya kuwagawa watu kwa mabila yao. muasisi mkuu ni CCM.

Tukiendelea hivi haitakuja kushangaza huko mbeleni kila kabila likiwa na ka mkoa kake.

Geographically, Mbeya mjini ipo almost katikati ya makao makuu ya wilaya zote za mkoa wa Mbeya. Kwa bahati nzuri pia ni kwamba asilimia 80 zimeunganishwa na barabara za lami. ni ujinga sana kuzalisha mkoa mwingine kutoka mkoa huu labda ikiwa ni kwa sababu za kisiasa.

Nitakuwa mmoja wa wale wanaopinga ubaguzi huu mpya kupitia dhana ya mikoa mipya.

Ile dhana ya umoja ni nguvu imekwisha kabisa nchi hii! Nawalaani kabisa JK na Pinda kuendekeza ubaguzi!
 
Mkuu, hivi kweli unaweza kusema kwa moyo kwamba Chunya hakuna watu ila Kyela na Tukuyu ndiko kuna watu wakuhitaji mkoa!. Uko sahihi kwa mawazo yako.

Ni kwa vigezo gani unaweza kulinganisha population za mikoa ya Arusha na Moshi ni sawa na Tukuyu na Kyela? Kyela kuwa mkoa ajili ya nini? Ka kijiji kale kenye vitongozi ipinda, kasumulu, kapwili, kalumbulu, Itunge, Ngyeke sijui wapi Usale, na Ipande sijui kwa wauaji ndiyo ipewe mkoa? Naomba jamani tuwe serious na hasa linapokuja suala la maendeleo ya taifa.

Roho ya ubaguzi wa huko Kyela mnataka sasa iingie katika mfumo wa taifa? Naomba usiwe mmoja wa wale wanaojiita wakumyetu wanaowish usiku na mchana kufukuza wageni wote, wabaki peke yao. Na sasa unataka kuhalalisha mupewe mkoa kwa sababu hata mkipewa mkoa bado nia ya kutaka kujibagua ama kubagua wengine haitatimia. Bado mtahitaji michango mbli mbali kutoka sehemu na watu wa sehemu zingine duniani.

Twende vizuri tu. Tujadiliane kwa hoja na amani tutafikia muafaka sahihi. Tukiendekeza u mimi , ukabila na ukwetu, tutaend up tena ku split na kuanza kupeana fursa kwa misingi ya koo, n.k.

Hili nalo ni neno Tabby, ingawa umenikwaza kidogo kuisahau TalaTala kwenye orodha ya maeneo muhimu Kyela;na Mmbasa, na Mbelele, na lopyu; olwa kyai kya lukama!
 
Ni heri hizo pesa za administration cost tukajenga lami na miondombinu na kuimarisha huduma za kijamii
 
Back
Top Bottom