Kuigawa Mbeya: Ushauri wa JF Kuhusu Mlowo

Kuigawa Mbeya: Ushauri wa JF Kuhusu Mlowo

Highlander

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2012
Posts
3,093
Reaction score
1,077


Wadau wa hapa Great Thinkers
ninalo ombi maalumu kwenu kuhusu tatizo la kuugawa mkoa wa Mbeya. Kuna kambi tatu zimezuka kule Mbeya kuhusu suala hili, kwa mujibu wa taarifa ambazo ninazo leo, na ni kambi zenye sura ya Ukabila. Ninaamini jamvi hili linao uwezo kuisaidia serikali yetu kufanya uamuzi ambao ni sahihi kufuta hii sura ya ukabila badala ya kustawisha taswira hiyo. Kambi moja inataka Rungwe kuwa ndo Mkoa mpya, Kambi ya pili inataka Chunya, na sasa Mbozi wanataka Kwao ndiyo kuwe Mkoa Mpya na makao makuu yawe Mlowo! Na kwamba wazo hili 'eti' linaungwa mkono ya WanaIleje.

BACKGROUND:
Miaka ya 1980 Mkoa wa Mbeya ulikuwa na Chama Kikuu cha Ushirika kikiitwa MBECU: Mbeya Co-operative Union. Wanambeya wanaotoka Kyela na Rungwe Waliomba wapewe uhuru kuunda chama chao. Walipewa idhini hiyo wakajitenga na kuunda chama chao kilichoitwa KYERUCU: Kyela-Rungwe Co-operative Union. Lakini baadaye wakazi wa Wilaya za Kyela na Rungwe walishindwa kukaa pamoja katika Chama hiki Kyerucu ikavunjika na kuunda vyama viwili tofauti zikazaliwa KYECU ya Kyela na RUCU ya Rungwe.

Angalizo ni kwamba Kusambaratika kwa mshikamano wa WanaMbeya kupitia MBECU ulianzia kwenye Ukanda wa Unyakyusa kutafuta kujitenga. MBECU bila Wanyakyusa ilichechemea kwa Muda fulani ikajifia taratibu baada ya Watu wa Mbozi, ambako makabila makubwa ni Wanyiha na Wanyamwanga walipoamua nao kujitenga na kuunda Vyama vyao vya Ushirika, kikiwepo chama kilichoitwa ISAYULA: Isansa-Iyula Co-operative Union.

HOJA YA KUIGAWA MBEYA ILIYOPO LEO
Taarifa nilizo nazo ni kwamba Wilaya ya Rungwe ndio waasisi wa wazo la Kuigawa Mbeya. Rungwe waliomba wapewe idhini kuwa mkoa. Katika Mtizamo huo, ilieleweka wazi kwamba mazingira ya ki-jiografia ya Mkoa huo yangelazimisha Wilaya za Rungwe na Kyela kuingia katika Mkoa huo wa Rungwe. Lakini Pia Ileje Ingeweza kuingia bila shida, na pengine sehemu fulani-fulani za Iringa ya Zamani kwenye maeneo ambayo pengine sasa ni Njombe. Wazo la Rungwe ndilo hasa msingi wa mgororo uliopo leo, ambao umeanzia kwenye msimamo wa Serikali kukataa Rungwe kuwa Mkoa: ambapo mimi pia nikiwa MwanaMbeya mwenye kutetea umoja na mshikamano wa Mkoa wetu nasita kukubali ombi hilo la Rungwe haraka-haraka kwa sababu ya historia niliyoiweka hapo juu.

MBOZI, MOMBA, ILEJE NA CHUNYA
Leo nimepewa taarifa ifuatayo: kwamba katika siku mbili tatu zilizopita, Full council ya wilaya ya Mbozi imepitisha Azimio kukataa Chunya kuwa Makao Makuu ya Mkoa Mpya dada wa Mbeya ambao unatakiwa kuitwa Mkoa wa Songwe. WanaMbozi wamepitisha azimio Mkoa Mpya Uwe Mbozi na Makao Makuu yawe Mlowo. Kwa mujibu wa taarifa hizo, wanaCCM wa wilaya za Ileje na Momba wanaafiki wazo hili kuweka makao makuu ya Mkoa Mpya kuwa Mlowo, Mbozi. Tatizo linalozuka ni hili: Chunya watapata shida sana kuja Mlowo.

My Take: Mkoa ubakie ulivyo!

Naomba mawazo yenu wadau tuisaidie Serikali yetu kufanya maamuzi sahihi.
-------------------
HITIMISHO
-------------------


Mjadala umeelekeza haja ya kuchukua hatua: Kwamba next week tuhamie Phase Two ya mjadala--ACTION. Wenzetu waliopo on the ground kule Mbozi na Ileje wameanza kuchukua hatua kwa mujibu wa taarifa ambazo ninazo.WanaIleje na Mbozi wamekataa kupelekwa Chunya, wakitaka Mkoa mpya uwe Mbozi kama kuna ulazima wa kuugawa Mkoa. Sisi katika intelligentsia ya Mkoa wa Mbeya tulioko katika Diaspora ya Mkoa tunapiga wazo zima la kuugawa mkoa kwa sababu hatuoni haja, umuhimu wala sababu ya kuridhisha ya kuugawa mkoa.

Mjadala unaelekeza sasa tuhamie kwenye vitendo, nionavyo mimi: Tunatakiwa sasa kuwaunga mkono wenzetu walioko on the ground kwa kuchukua hatua kuzuwia upuuzi huu. Tusiishie kupost-post tu maneno humu JF. Jaza Vocha kwenye laini yako, hamasisha madiwani, hamasisha wajumbe wa nyumba kumi, hamasisha Walimu wa shule za Msingi na Sekondari, hamasisha Mabibi shamba na Mabwana shamba, Manesi na Medical assistant wataopata shida sana kusafiri kutoka Itumba, Msia, Idunda na kwingineko, eti kwenda Mkwajuni kufuata huduma za Mkoa wapinge upuuzi huu. Wapatie maelezo yanayojitosheleza: Waelekeze kwenye petittion ambayo inaandaliwa kama hawa wenzetu chini ya RC Abbas Kandoro watajaribu kutekeleza upuuzi huu.

Wadau wa mjadala huu kama kuna mahala nimekosea katika hitimisho hili naomba marekebisho tafadhali.
 
mkuu nimekupata kutokana historia fupi ya vyama vya ushirika mbeya! labda ningeomba kujuzwa kwanini serikali inataka kuigawa mbeya? je ni kwasababu za kijiografia au kisiasa?
 
mkuu nimekupata kutokana historia fupi ya vyama vya ushirika mbeya! labda ningeomba kujuzwa kwanini serikali inataka kuigawa mbeya? je ni kwasababu za kijiografia au kisiasa?

mimi nipo sekta binafsi Mkuu wangu. kwa hiyo mtizamo wa serikali upo mbali kidogo nami na sijui hasa wanachokiwaza zaidi ya taarifa za wazi kwenye magazeti na mitandaoni. Ila ninachojua ni kwamba serikali imekataa kuipa idhini Rungwe kuwa Mkoa kama walivyoomba wanaRungwe. Kwa nini wamekataa? hili sasa ni gumu kujua kwa sababu mie nipo nje ya system. Ninachoweza kufanya ni ku-extrapolate na kuweka dhana hisia kama nilivyofanya, kutokana na historia ya usambaratikaji iliyotokana na hisia za ukabila.

Jambo kubwa la kukumbuka hapa ni kwamba Rungwe Waliomba kuwa Mkoa. Chunya hawakuomba kuwa Mkoa, Ileje hawakuomba kuwa mkoa, Mbozi hawakuomba kuwa Mkoa, Momba hawakuomba kuwa Mkoa. Rungwe waliomba kuwa Mkoa.
 
Kwa kifupi kuugawa mkoa wa Mbeya ni wazo la kifisadi na lisilo na tija. Kijiografia mkoa wa Mbeya haugawiki na hakuna sababu za msingi za kuugawa mkoa huo!

Uzoefu unaonyesha hata mkoa ukigawanywa hakuna rasilimali fedha zinazoongezeka mbali na kuanza kutumia fedha nyingi kwa ajili ya mambo ya utawala! Angalia mikoa ya Rukwa na Katavi, kinachofanyika ni kuzigawa fedha za maendeleo ambazo zamani zilikuwa za mkoa wote wa Rukwa ikiwemo Katavi katika sehemu mbili!

Hivyo kama shinikizo ni Chunya kuwa na mkoa basi wapewe, lakini kwa Ileje haitakuwa kuwatendea haki kwani Mkwajuni ambako ndipo panapendekezwa kuwa makao makuu ya mkoa wa Songwe hakutawafaa kabisa.

Wilaya ya Mpanda imeunda mkoa peke yake kwa kijitoa Rukwa hivyo si vibaya Chunya wakaunda mkoa wake peke yake!
 
mimi nipo sekta binafsi Mkuu wangu. kwa hiyo mtizamo wa serikali upo mbali kidogo nami na sijui hasa wanachokiwaza zaidi ya taarifa za wazi kwenye magazeti na mitandaoni. Ila ninachojua ni kwamba serikali imekataa kuipa idhini Rungwe kuwa Mkoa kama walivyoomba wanaRungwe. Kwa nini wamekataa? hili sasa ni gumu kujua kwa sababu mie nipo nje ya system. Ninachoweza kufanya ni ku-extrapolate na kuweka dhana hisia kama nilivyofanya, kutokana na historia ya usambaratikaji iliyotokana na hisia za ukabila.

Jambo kubwa la kukumbuka hapa ni kwamba Rungwe Waliomba kuwa Mkoa. Chunya hawakuomba kuwa Mkoa, Ileje hawakuomba kuwa mkoa, Mbozi hawakuomba kuwa Mkoa, Momba hawakuomba kuwa Mkoa. Rungwe waliomba kuwa Mkoa.
Rungwe hata kama waliomba haiwezekani wakubaliwe kwa kigezo cha idadi ya watu na eneo! Hivyo Rungwe kama waliomba mkoa walifanya hivyo kwa kutegemea kuwa wangeungwa mkono na wilaya za jirani!
 
Kwa kifupi kuugawa mkoa wa Mbeya ni wazo la kifisadi na lisilo na tija. Kijiografia mkoa wa Mbeya haugawiki na hakuna sababu za msingi za kuugawa mkoa huo!

Uzoefu unaonyesha hata mkoa ukigawanywa hakuna rasilimali fedha zinazoongezeka mbali na kuanza kutumia fedha nyingi kwa ajili ya mambo ya utawala! Angalia mikoa ya Rukwa na Katavi, kinachofanyika ni kuzigawa fedha za maendeleo ambazo zamani zilikuwa za mkoa wote wa Rukwa ikiwemo Katavi katika sehemu mbili!

Hivyo kama shinikizo ni Chunya kuwa na mkoa basi wapewe, lakini kwa Ileje haitakuwa kuwatendea haki kwani Mkwajuni ambako ndipo panapendekezwa kuwa makao makuu ya mkoa wa Songwe hakutawafaa kabisa.

Wilaya ya Mpanda imeunda mkoa peke yake kwa kijitoa Rukwa hivyo si vibaya Chunya wakaunda mkoa wake peke yake!

Umejenga hoja vizuri sana Ileje. Ila naona umesahau kipengele muhimu sana hapo. Chunya hawakuomba kujitenga. Walioomba kujitenga ni Rungwe! Hilo unalisemeaje?
 
Highlander,
.
Ahsante sana ndugu yangu kwa kujali na pia kuwa mkweli. Ni kweli kwamba, ipo mantiki kubwa ya kuugawa mkoa wa Mbeya kutokana na ukubwa wa eneo, muundo wa ki jiographia na mfumo wake wa kiuchumi. Tatizo kubwa hapa ambalo ndugu zangu wakazi wa Mbeya ambalo hawalioni kwa haraka ni kwamba mipango yao inavutwa na hisia za ukabila zaidi bila kuzingatia madhara ya maamuzi ya jinsi hiyo kwa wanaMbeya wenyewe na serikali kwa ujumla.

Lengo kuu la dhana ya kugawa maeneo ya utawala ni kusogeza huduma za kibinadamu na maendeleo kwa wananchi. Kwa mtazamo wangu huu, napangua kipaumbele cha Rungwe kuwa mkoa na makao makuu ya mkoa mpya kwa sababu Rungwe na Mbeya ni karibu sana. Mbeya kwenda Kyela ni km zisizozidi 120 kufuata urefu wa barabara ambayo ni ya kiwango cha lami hadi Blantyre. Napendekeza Rungwe , Kyela na Ileje ziendelee kuwa chin ya Mkoa wa Mbeya ambapo ni karibu sana na panafikika kwa urahisi bila shida.

Pale kuMbozi, wanahitaji kupewa elimu ya utaifa ili waelewe ni kwa nini kwa sasa mlowo hapawezi kupewa kipaumbele cha kufanyika makao makuu ya mkoa mpya ulilinganisha na ndugu zao wa Chunya.

Chunya ni sehemu iliyojitenga ki jiographia na miundo mbinu. Ni sehemu yenye raslimali nyingi kama madini, mifugo, mazao ya chakula na biashara kwa wingi, lakini pia ni sehemu yenye utajiri mkubwa na miti ya mbao adimu. Umbali na miundo mbinu vinafanya mtu kwenda mkoani kupata hudumu muhimu na mkoa kwenda kutoa huduma chunya iwe shughuli maalumu.

Napendekeza Chunya ifanywe mkoa mpya, makao makuu yakiwa Makongorosi ili kusogeza huduma mbali mbali kwa wananchi wa maeneo hayo. Wazo la Mbozi kuimega iende chunya na sehemu za wilaya ya sikonge linaweza kuangaliwa. Chunya ikiwa mkoa, pamoja na kupeleka huduma kwa Watanzania wanaotabika, pia itaharakisha maendeleo ya miundo mbinu ambazo zitaongeza uzalishaji na pia usafirishaji wa bidhaa kutoka kusini mwa Tanzania kwenda kati kati, magharibi na sehemu zingine za nchi na vaisi vesa.Hii ni kuharakisha maendeleo ya taifa.

Kwa ufupi wanaochukua maamuzi ya jambo hili wasiamue kwa kuangalia influences za walio kwenye decision making functions na interest za ukwetu na ukabila. Waliangalie kwa mitazamo ya Utaifa na maendeleo ya nchi. Hakun sababu ya kurundika maendeleo sehemu moja wakati wananchi wa sehemu zingine wanaumia na huku nao wanatoa kodi kama wengine.

Nawasilisha.
 
Umejenga hoja vizuri sana Ileje. Ila naona umesahau kipengele muhimu sana hapo. Chunya hawakuomba kujitenga. Walioomba kujitenga ni Rungwe! Hilo unalisemeaje?

Kuomba kuwa mkoa si kigezo. Unaweza kuwa mchango wao katika kuwakumbusha watawala umuhimu wa kuwasogezea huduma watu wa Chunya. Sioni kabisa mantiki ya kuwa namkoa wa Rungwe mwendo wa nusu saa kutoka Mbeya tukawaacha watu wa chunya ambao lazima watumie siku tatu nje ya nyumbani ili kupata huduma mkoani. (Angalia kambi katoto).
 
Hivi huu utaratibu wa kuivunja vunja mikoa na kuongeza idadi yake ndio kubana matumizi au? Mbona vipindi vya nyerere na mwinyi hapakua na utaratibu huu....!!!! mbona hata mikoa 20 tanzania bara ilishakua mengi mno, na ingekua busara kuipunguza hata kufikia kumi tu. Sasa kwa mpango huu basi (morogoro, pwani, shinyanga, lindi n.k.) nayo itakuja kuwa mikoa mikoa miwili miwili......:bored:
 
Nilishawahi kuandika hapa kuwa wazo la kuugawa mkoa wa Mbeya lengo lake sio zuri...

Sina uhakika sana ni nani walioibua hii hoja pia hadi sasa sijajua vigezo walivyomulika kama sababu za kuugawa mkoa wetu...

Once Mbeya itapotengeneza mikoa mipya miwili, nina kila sababu ya kuamini vuguvugu zaidi za kujitenga zitaendelea...

Pale Mbeya kuna makabila huwa hayapatani kabisa sasa ukiyaweka mkoa mmoja si itakuwa kasheshe...

Wanyakyusa nje ya Mbeya ni ndugu, lakini ukishaingia Mbeya tu ndipo utajua kuwa kuna Wanyaki wa Kyela na wa Rungwe...na kuna wakati ndugu hawa huwa hawaivii chungu kimoja.
 
Hivi huu utaratibu wa kuivunja vunja mikoa na kuongeza idadi yake ndio kubana matumizi au? Mbona vipindi vya nyerere na mwinyi hapakua na utaratibu huu....!!!! mbona hata mikoa 20 tanzania bara ilishakua mengi mno, na ingekua busara kuipunguza hata kufikia kumi tu. Sasa kwa mpango huu basi (morogoro, pwani, shinyanga, lindi n.k.) nayo itakuja kuwa mikoa mikoa miwili miwili......:bored:

Naona wazo la kugawagawa hii mikoa linakutia hadi usingizi naona unapiga miayo hapo. ha ha ha.... it really does not make sense at all!
 
Kuna huu mkoa wanaouita Mkoa wa Pwani....yaani mimi kama ningelikuwa ni mtawala basi huu ndio ungekuwa mkoa wa kwanza kuumega na angalau kutengeneza mikoa miwili hadi mitatu...

Jiografia ya mkoa huu imekaa kiajabu na namna yake hiyo imechochewa na uwepo wa Dar es Salaam...

Hivi huu utaratibu wa kuivunja vunja mikoa na kuongeza idadi yake ndio kubana matumizi au? Mbona vipindi vya nyerere na mwinyi hapakua na utaratibu huu....!!!! mbona hata mikoa 20 tanzania bara ilishakua mengi mno, na ingekua busara kuipunguza hata kufikia kumi tu. Sasa kwa mpango huu basi (morogoro, pwani, shinyanga, lindi n.k.) nayo itakuja kuwa mikoa mikoa miwili miwili......:bored:
 
Kaka JF hata mm nakuunga mkono. Kulingana na maelezo yako ni bora Mbeya ibakie kama ilivyo ila ninacho hofia ni kuwa kuna baadhi ya watu watakuwa wabamaslahi yao binafsi na kama wana nguvu serikalini watatuangusha tu.
That's what I am worried about.
 
Kuna huu mkoa wanaouita Mkoa wa Pwani....yaani mimi kama ningelikuwa ni mtawala basi huu ndio ungekuwa mkoa wa kwanza kuumega na angalau kutengeneza mikoa miwili hadi mitatu...

Jiografia ya mkoa huu imekaa kiajabu na namna yake hiyo imechochewa na uwepo wa Dar es Salaam...

Yeah! uko sawa kabisa, kwa udogo wa mkoa wa dar, hii pwani ingetosha kuunganisha na dar. kutokana na kasi ya maendeleo ya dar, haitapita siku nyingi mendeleo yatakua yameenea na kiasi kikubwa tu. Ila kuvunja vunja hapana..
 
Highlander,
.
Ahsante sana ndugu yangu kwa kujali na pia kuwa mkweli. Ni kweli kwamba, ipo mantiki kubwa ya kuugawa mkoa wa Mbeya kutokana na ukubwa wa eneo, muundo wa ki jiographia na mfumo wake wa kiuchumi. Tatizo kubwa hapa ambalo ndugu zangu wakazi wa Mbeya ambalo hawalioni kwa haraka ni kwamba mipango yao inavutwa na hisia za ukabila zaidi bila kuzingatia madhara ya maamuzi ya jinsi hiyo kwa wanaMbeya wenyewe na serikali kwa ujumla.

Lengo kuu la dhana ya kugawa maeneo ya utawala ni kusogeza huduma za kibinadamu na maendeleo kwa wananchi. Kwa mtazamo wangu huu, napangua kipaumbele cha Rungwe kuwa mkoa na makao makuu ya mkoa mpya kwa sababu Rungwe na Mbeya ni karibu sana. Mbeya kwenda Kyela ni km zisizozidi 120 kufuata urefu wa barabara ambayo ni ya kiwango cha lami hadi Blantyre. Napendekeza Rungwe , Kyela na Ileje ziendelee kuwa chin ya Mkoa wa Mbeya ambapo ni karibu sana na panafikika kwa urahisi bila shida.

Pale kuMbozi, wanahitaji kupewa elimu ya utaifa ili waelewe ni kwa nini kwa sasa mlowo hapawezi kupewa kipaumbele cha kufanyika makao makuu ya mkoa mpya ulilinganisha na ndugu zao wa Chunya.

Chunya ni sehemu iliyojitenga ki jiographia na miundo mbinu. Ni sehemu yenye raslimali nyingi kama madini, mifugo, mazao ya chakula na biashara kwa wingi, lakini pia ni sehemu yenye utajiri mkubwa na miti ya mbao adimu. Umbali na miundo mbinu vinafanya mtu kwenda mkoani kupata hudumu muhimu na mkoa kwenda kutoa huduma chunya iwe shughuli maalumu.

Napendekeza Chunya ifanywe mkoa mpya, makao makuu yakiwa Makongorosi ili kusogeza huduma mbali mbali kwa wananchi wa maeneo hayo. Wazo la Mbozi kuimega iende chunya na sehemu za wilaya ya sikonge linaweza kuangaliwa.
Chunya ikiwa mkoa, pamoja na kupeleka huduma kwa Watanzania wanaotabika, pia itaharakisha maendeleo ya miundo mbinu ambazo zitaongeza uzalishaji na pia usafirishaji wa bidhaa kutoka kusini mwa Tanzania kwenda kati kati, magharibi na sehemu zingine za nchi na vaisi vesa.Hii ni kuharakisha maendeleo ya taifa.

Kwa ufupi wanaochukua maamuzi ya jambo hili wasiamue kwa kuangalia influences za walio kwenye decision making functions na interest za ukwetu na ukabila. Waliangalie kwa mitazamo ya Utaifa na maendeleo ya nchi. Hakun sababu ya kurundika maendeleo sehemu moja wakati wananchi wa sehemu zingine wanaumia na huku nao wanatoa kodi kama wengine.

Nawasilisha.

Mkuu Tabby, maelezo yako ambayo nimeyaweka katika blu binafsi naona kama yana mashiko. Wilaya ya Mbozi kama kisehemu chake kikipelekwa Chunya sidhani kama linaweza kuleta shida hilo. Hata hivyo, naona umesahau kujadili mitizamo miwili muhimu sana ambayo wachangiaji wengi kwenye hizi mada za kuugawa mkoa wa mbeya wamekuwa wanalalamikia.

Moja ni kwamba migawanyiko hii inaongeza gharama za uendeshaji wa serikali.
Pili, kwamba kusogeza huduma kwa wananchi kunaweza kufanywa bila kuongeza ukubwa wa serikali kuu, kwa mfano linaweza kufanywa kwa kusogeza hizo huduma zinazohitajika kwenye maeneo husika--kama vile mabenki yanavyoweka ATM kwenye petrol station. Huduma ya benki inakuwa imesogezwa kwa watu bila kujenga benki hapo petrol station.

Haya naona umesahau kuyaongelea.
 
Kaka JF hata mm nakuunga mkono. Kulingana na maelezo yako ni bora Mbeya ibakie kama ilivyo ila ninacho hofia ni kuwa kuna baadhi ya watu watakuwa wabamaslahi yao binafsi na kama wana nguvu serikalini watatuangusha tu. That's what I am worried about.

hali ya kisiasa ilivyokaa si rahisi sana kuburuza watu kwenye jambo hawataki mkuu. lakini ngoja tuendelee kusikilizia lipi litazuka.
 
Mkuu Tabby, maelezo yako ambayo nimeyaweka katika blu binafsi naona kama yana mashiko. Wilaya ya Mbozi kama kisehemu chake kikipelekwa Chunya sidhani kama linaweza kuleta shida hilo. Hata hivyo, naona umesahau kujadili mitizamo miwili muhimu sana ambayo wachangiaji wengi kwenye hizi mada za kuugawa mkoa wa mbeya wamekuwa wanalalamikia.

Moja ni kwamba migawanyiko hii inaongeza gharama za uendeshaji wa serikali.
Pili, kwamba kusogeza huduma kwa wananchi kunaweza kufanywa bila kuongeza ukubwa wa serikali kuu, kwa mfano linaweza kufanywa kwa kusogeza hizo huduma zinatohitajika kwenye maeneo husika--kama vile mabenki yanavyoweka ATM kwenye petrol station. Huduma ya benki inakuwa imesogezwa kwa watu bila kujenga benki hapo petrol station.

Haya naona umesahau kuyaongelea.

Unajua kiongozi, suala hili la kugawa maeneo linaweza kufanyika kwa misingi ya kisiasa ama ki uchumi. Sikuzungumzia suala la serikali kupeleka attentions zake karibu na watu popote pale walipo kwa sababu serikali ya ccm haina utamaduni wala jadi ya uwajibikaji wala kujali.

Suala la cost implication halina ubishi kabisa kiongozi. Ni dhahiri kwamba gharama za uendeshaji zinazidi kuwa kubwa. Ni kweli kabisa kwamba gharama za kuanzisha na kuendesha mikoa mipya zinaweza kufanya kazi kubwa sana kwa maendeleo ya watu iwapo tu serikali ingekuwa na huo utamaduni.

Sukuyangelea haya kwa sababu huduma za maendeleo ya wananchi wa TZ huwa hayaji kwa sababu ya mipango thabiti. Ni kwa kuoneana aibu tu. It is as if mtu akikaa na watu akawa anawaonaona wanavyoteseka na wakamwangalia macho ya huruma, basi anawahurumia na kushughulikia miradi ya maendeleo kama misaada vile na wala si haki yao.

Ingekuwa serikali ina mifumo sahihi ya mipango ya maenendeleo yenye usimamizi mahususi inayoendeshwa kwa misingi ya sheria na utawala bora, agenda za kugawa maeneo ya utawala wa mikoa ingekuwa ni kwa miji michache sana Tanzania yenye misongamano ya watu.

Lakini, ninachangezea ni kwamba serikai isifanye maamuzi haya kwa sasa mda wa lala salama. Maamuzi yag kugawa mikoa yafanyike baada ya uchaguzi 2015 kwa kuwa tutakuwa na serikali makini inayojali wananchi. Hapo ninajua kabisa watu watapata huduma za maendeleo bila haja ya kuwa na mikoa mipya.
 
Unajua kiongozi, suala hili la kugawa maeneo linaweza kufanyika kwa misingi ya kisiasa ama ki uchumi. Sikuzungumzia suala la serikali kupeleka attentions zake karibu na watu popote pale walipo kwa sababu serikali ya ccm haina utamaduni wala jadi ya uwajibikaji wala kujali.

Suala la cost implication halina ubishi kabisa kiongozi. Ni dhahiri kwamba gharama za uendeshaji zinazidi kuwa kubwa. Ni kweli kabisa kwamba gharama za kuanzisha na kuendesha mikoa mipya zinaweza kufanya kazi kubwa sana kwa maendeleo ya watu iwapo tu serikali ingekuwa na huo utamaduni.

Sukuyangelea haya kwa sababu huduma za maendeleo ya wananchi wa TZ huwa hayaji kwa sababu ya mipango thabiti. Ni kwa kuoneana aibu tu. It is as if mtu akikaa na watu akawa anawaonaona wanavyoteseka na wakamwangalia macho ya huruma, basi anawahurumia na kushughulikia miradi ya maendeleo kama misaada vile na wala si haki yao.

Ingekuwa serikali ina mifumo sahihi ya mipango ya maenendeleo yenye usimamizi mahususi inayoendeshwa kwa misingi ya sheria na utawala bora, agenda za kugawa maeneo ya utawala wa mikoa ingekuwa ni kwa miji michache sana Tanzania yenye misongamano ya watu.

Lakini, ninachangezea ni kwamba serikai isifanye maamuzi haya kwa sasa mda wa lala salama. Maamuzi yag kugawa mikoa yafanyike baada ya uchaguzi 2015 kwa kuwa tutakuwa na serikali makini inayojali wananchi. Hapo ninajua kabisa watu watapata huduma za maendeleo bila haja ya kuwa na mikoa mipya.

Nimekuelewa vizuri Mkuu Tabby. Nikubaliane nawe hapa kwamba mtindo ambao umetumika kuigawa mikoa yetu, au hata wilaya zetu, kama ambavyo wewe unabainisha, kwa kweli umeacha maswali mengi sana kuhusu tija ya maamuzi hayo. Najua kwamba hili la kuugawa mkoa wa Mbeya lina sura nyingi, ikiwepo ya kustawisha tatizo la ukabila. Wakati huo huo naiona haja ya kusogeza huduma kwa wananchi kama ulivyosema awali--hasa Chunya--ingawa kwa kusema hivyo unatakiwa pia kusema hilohilo kuhusu Ileje. Sidhani kama jibu la tatizo hili ni kuugawa mkoa huu fastafasta. Kama uharaka huo watu waliopo CCM wanautaka, bas pengine wawazie la kuipa wilaya ya Chunya hadhi ya Mkoa--labda hilo; lakini si vinginenvyo. Mtu aliyepo Vwawa yupo karibu zaidi na Mbeya mjini kuliko Mtu aliyeko Ikombe Kyela. Hoja za jiografia zinapinga ugawaji wa mkoa huu, hoja za kimanejiment na prudence katika matumizi ya fedha za umma vinakataza kuugawa mkoa, hoja zinazolenga kutochochea ukabila zinakataza kuugawa mkoa huu. The only reason would be kusogeza huduma Chunya na Ileje. Hapo sasa swali muhimu linakuwa je, jibu la kusogeza huduma za kiserikali Chunya na Ileje ni kuugawa mkoa? jibu ni NO! There are too many contradictions and constraints; too many. Mkoa ubaki ulivyo.
 
Highlander,
.
Ahsante sana ndugu yangu kwa kujali na pia kuwa mkweli. Ni kweli kwamba, ipo mantiki kubwa ya kuugawa mkoa wa Mbeya kutokana na ukubwa wa eneo, muundo wa ki jiographia na mfumo wake wa kiuchumi. Tatizo kubwa hapa ambalo ndugu zangu wakazi wa Mbeya ambalo hawalioni kwa haraka ni kwamba mipango yao inavutwa na hisia za ukabila zaidi bila kuzingatia madhara ya maamuzi ya jinsi hiyo kwa wanaMbeya wenyewe na serikali kwa ujumla.

Lengo kuu la dhana ya kugawa maeneo ya utawala ni kusogeza huduma za kibinadamu na maendeleo kwa wananchi. Kwa mtazamo wangu huu, napangua kipaumbele cha Rungwe kuwa mkoa na makao makuu ya mkoa mpya kwa sababu Rungwe na Mbeya ni karibu sana. Mbeya kwenda Kyela ni km zisizozidi 120 kufuata urefu wa barabara ambayo ni ya kiwango cha lami hadi Blantyre. Napendekeza Rungwe , Kyela na Ileje ziendelee kuwa chin ya Mkoa wa Mbeya ambapo ni karibu sana na panafikika kwa urahisi bila shida.

Pale kuMbozi, wanahitaji kupewa elimu ya utaifa ili waelewe ni kwa nini kwa sasa mlowo hapawezi kupewa kipaumbele cha kufanyika makao makuu ya mkoa mpya ulilinganisha na ndugu zao wa Chunya.

Chunya ni sehemu iliyojitenga ki jiographia na miundo mbinu. Ni sehemu yenye raslimali nyingi kama madini, mifugo, mazao ya chakula na biashara kwa wingi, lakini pia ni sehemu yenye utajiri mkubwa na miti ya mbao adimu. Umbali na miundo mbinu vinafanya mtu kwenda mkoani kupata hudumu muhimu na mkoa kwenda kutoa huduma chunya iwe shughuli maalumu.

Napendekeza Chunya ifanywe mkoa mpya, makao makuu yakiwa Makongorosi ili kusogeza huduma mbali mbali kwa wananchi wa maeneo hayo. Wazo la Mbozi kuimega iende chunya na sehemu za wilaya ya sikonge linaweza kuangaliwa. Chunya ikiwa mkoa, pamoja na kupeleka huduma kwa Watanzania wanaotabika, pia itaharakisha maendeleo ya miundo mbinu ambazo zitaongeza uzalishaji na pia usafirishaji wa bidhaa kutoka kusini mwa Tanzania kwenda kati kati, magharibi na sehemu zingine za nchi na vaisi vesa.Hii ni kuharakisha maendeleo ya taifa.

Kwa ufupi wanaochukua maamuzi ya jambo hili wasiamue kwa kuangalia influences za walio kwenye decision making functions na interest za ukwetu na ukabila. Waliangalie kwa mitazamo ya Utaifa na maendeleo ya nchi. Hakun sababu ya kurundika maendeleo sehemu moja wakati wananchi wa sehemu zingine wanaumia na huku nao wanatoa kodi kama wengine.

Nawasilisha.

Hasante kwa ufafanuzi mzuri kiongozi ila naomba kukusahihisha Mbeya mjini hadi Kyela sio 120km ni 210km ila zaidi naomba wanao taka kutugawa watumie buzara zaidi kuliko hisia za watu fulani kwani hata mimi sitaki hata kidogo mkoa wangu ugawanywe kwani hapo ni kuongeza maslahi ya watawala na sio wananvhi mfano ni Kyela mjini mji mzima hauna hata barabara ya kiwango cha rami ingawa ni mji mdogo sana so ishu sio ukubwa ishu ni commitment za watawala wetu kutuletea maendeleo. Leo hii watu wa Kyela wanadiliki kusema Mwakyembe sio mbuge wao bali ni mbuge wa Dar es salaam kutokana na kuwatelekeza kwake wana Kyela.
 
Hili suala ni la msingi kujadiliwa, hata hivyo utata lazima utakuwa sawa na ilivyokuwa wakati wa kuigawa mikoa mingine iliyo tangulia. Naomba watu wa kutoka hiyo mikoa wajitoe pia kuchangia uzi huu na watoe maoni yao kuleta picha kamili ya mchakato wa kuigawa Mbeya.

Hata hivyo ingefaa wale wanaopigania kuugawa mkoa wangekuja na hoja, waseme wenyewe nia yao ya kuugawa mkoa imetokana na nini, na ni nini wananchi wenyewe wanasema kuhusu hili. Hapa ndo tunapata kujua tu kuwa lazima kuna kundi la watu wakiwa wamelewa, na lazima wanafaidi, huwa wanaibua kwa makusudi kuigawa hii mikoa. Mkoa wa Mbeya usigawanywe, na wenye nia ya kuugawa waje na sababu kimaandishi watueleze wananchi. Na zaidi kama sababu ni za kukosekana kwa utolewaji sawia wa huduma za msingi pia wasema kwa nini imekuwepo hvyo na wakubali kuwajibishwa.

Nainua macho juu, nikitazamia majimbo ambayo ndo yatakuwa suluhisho pekee kwa maendeleo ya Watz.
 
Back
Top Bottom