Steven mushi mushi
JF-Expert Member
- Jul 25, 2016
- 533
- 741
Za jioni wapendwa,
Leo kuna stori moja hivi ambayo imetokea Nairobi nchini Kenya kuhusu jamaa mmoja ambaye amembwaga mchumba wake baada ya huyo binti kumwambia jamaa juu ya past yake kuwa alikuwa anafanya kazi ya kujiuza maeneo ya mombasa.
Kisa chenyewe kipo hivi huyu jamaa na mchumba wake wamedumu kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka miwili na binti anadai juzi alienda kumtembelea huyu mchumba wake ambaye yeye anaishi Nairobi sasa baada ya stori mbili tatu jamaa akaanza stori kwamba anataka kila mmoja amwambie mwenzake kuhusu past yake ndiposa binti akaanza kumsimulia huyu jamaa ambaye ni mchumba wake kuwa yeye zamani alikuwa prostitute huko mombasa.
Kutokana na ugumu wa maisha na anasema hiyo kazi alifundishwa na rafiki yake ambaye yeye alikuwa mzoefu wa hiyo kazi kwa mda mrefu, baada ya binti kumwelezea jamaa kila kitu ndipo sasa jamaa akahamaki na kuanza kumlaumu binti kwamba kwanini hakumwambia mapema, binti akamwomba samahani kuwa alifanya vile kutokana na shida ila jamaa hakumwelewa na akaamua kummwaga.
Huyu binti anadai amejaribu kumuomba jamaa msamaha kuwa ilikuwa past amsamehe na wasonge mbele ila jamaa amekataa katukatu kuendelea naye na huyu binti anadai ana mimba ya huyu jamaa na ina miezi mitatu ila jamaa amemwambia kama ni mimba atagharamikia na mtoto akizaliwa yuko tayari kumtunza lakini sio kuendelea kuwa naye kwenye mahusiano.
Huyu binti amelia sana na kujilaumu kwa kitendo chake cha kumweleza jamaa ukweli kuhusu past yake. Sasa swali ni je huyu jamaa alikuwa anatafuta kisingizio cha kumwacha huyu binti au alikuwa anampenda ila baada ya binti kumwambia ukweli kuhusu past yake akakasirika na kuamua waachane na ikumbukwe huyu jamaa ndiye alitaka huyu binti amwambie kuhusu past yake.
Leo kuna stori moja hivi ambayo imetokea Nairobi nchini Kenya kuhusu jamaa mmoja ambaye amembwaga mchumba wake baada ya huyo binti kumwambia jamaa juu ya past yake kuwa alikuwa anafanya kazi ya kujiuza maeneo ya mombasa.
Kisa chenyewe kipo hivi huyu jamaa na mchumba wake wamedumu kwenye mahusiano kwa kipindi cha miaka miwili na binti anadai juzi alienda kumtembelea huyu mchumba wake ambaye yeye anaishi Nairobi sasa baada ya stori mbili tatu jamaa akaanza stori kwamba anataka kila mmoja amwambie mwenzake kuhusu past yake ndiposa binti akaanza kumsimulia huyu jamaa ambaye ni mchumba wake kuwa yeye zamani alikuwa prostitute huko mombasa.
Kutokana na ugumu wa maisha na anasema hiyo kazi alifundishwa na rafiki yake ambaye yeye alikuwa mzoefu wa hiyo kazi kwa mda mrefu, baada ya binti kumwelezea jamaa kila kitu ndipo sasa jamaa akahamaki na kuanza kumlaumu binti kwamba kwanini hakumwambia mapema, binti akamwomba samahani kuwa alifanya vile kutokana na shida ila jamaa hakumwelewa na akaamua kummwaga.
Huyu binti anadai amejaribu kumuomba jamaa msamaha kuwa ilikuwa past amsamehe na wasonge mbele ila jamaa amekataa katukatu kuendelea naye na huyu binti anadai ana mimba ya huyu jamaa na ina miezi mitatu ila jamaa amemwambia kama ni mimba atagharamikia na mtoto akizaliwa yuko tayari kumtunza lakini sio kuendelea kuwa naye kwenye mahusiano.
Huyu binti amelia sana na kujilaumu kwa kitendo chake cha kumweleza jamaa ukweli kuhusu past yake. Sasa swali ni je huyu jamaa alikuwa anatafuta kisingizio cha kumwacha huyu binti au alikuwa anampenda ila baada ya binti kumwambia ukweli kuhusu past yake akakasirika na kuamua waachane na ikumbukwe huyu jamaa ndiye alitaka huyu binti amwambie kuhusu past yake.